WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, April 13, 2014

Azam FC kutangazwa mabingwa leo?



Dar es Salaam. Ligi Kuu Bara imefikia patamu huku Azam FC na Yanga zikipigana kufa au kupona kuwania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu, ambapo mechi zao za leo ndiyo zitakozotoa picha ya ubingwa msimu huu.
Azam itaingia dimbani leo kukipiga na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya huku Yanga ikicheza dhidi ya JKT Oljoro leo kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha. Azam yenye pointi 56 itaingia uwanjani leo kutafuta pointi tatu muhimu na kutangazwa mabingwa kwani ushindi wowote utawasaidia kufikisha pointi 59 ambazo hazitafikiwa na timu yoyote katika Ligi Kuu Bara kwani Yanga yenye pointi 52 ikishinda michezo miwili iliyobakiza ukiwamo wa leo itafikisha pointi 58.
Mbali na mechi hizo pia Simba itacheza leo na Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa, wakati Mtibwa itacheza na Ruvu Shooting Uwanja wa Manungu na Mgambo itawakaribisha Kagera kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Katika mechi zilizochezwa jana, JKT Ruvu iliichapa Coastal Union 1-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani wakati Rhino Rangers ilichapwa na Tanzania Prisons 4-3 kwenye Uwanja wa Sokoine na hivyo kushuka rasmi daraja. Imeandaliwa na Vicky Kimaro, Godfrey Kahango na Bulhan Yakub

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment