WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 2, 2014

BUNGE MAALUM LA KATIBA MPYA LIMETAWALIWA NA LONGO LONGO ZA KIITIKADI:




Wakati Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya baada ya tume ya Jaji warioba kuwasilisha rasimu ya pili ya katiba mpya na mheshimiwa Rais wa Jamuhuri kuwatangaza rasmi wajumbe  zaidi ya 600 ambao ni wawakilishi wa wananchi wa Tanzania katika upatikanaji wa Katiba hiyo Mpya.

Safari hii ya maandalizi ya kuandaa katiba mpya kwa kweli imekuwa haionyeshi mwelekeo mzuri ambao unaleta matumaini kwa taifa letu. Tunafahamu fika kuwa Mheshimiwa Rais kupitia washauri wake ametuteua watu wazuri na ni tegemeo letu kuwa wawakilishi hao ni watu wenye hekima na uwezo mzuri wa kutuandalia Katiba Bora kwa vizazi vijavyo.

Kutangazwa kwa bunge hili la katiba kwa upande mmoja iliamsha matumaini ya wananchi kuwa kazi hii itakuwa nyepesi na yenye tija nzuri kwa maendeleo ya Taifa na wananchi wake ndani ya miezi mitatu ambayo  Bunge hili limepewa ili kukamilisha kazi yake kuanzia February  2014.

Lakini cha kushangaza mpaka niandikapo waraka huu, inasikitisha kuwa  kuwa mwendo wa bunge hili ni wa kusuasua.  Kwa maneno mengine hakuna mwelekeo mzuri ambao bunge hili maalumu limeonyesha baada yake bunge limepewa majina ambayo hayaendani na wadhifa wake.

Bunge lililojaa mizengwe , malumbano, kashfa, mivutano na kadhalika.

Kama wananchi tuna mengi ya kujiuliza hawa waheshimiwa wabunge wanafanya haya yote kwa faida ya nani?

Je waheshimiwa wajumbe wanaelewa nini wanatakiwa wafanye kwa faida ya Taifa hili?

Je kupitisha kanuni za kuendesha bunge maalum  ni lazima watukanane?

Ni ukweli ambao haufichiki kuwa  hata Aristotle katika maelekezo yake kuhusu Demokrasia alikuwa anahimiza katika Majadiliano ya hoja; na sio kuzomeana na kutukanana; lakini ukifilisika kifikra matokeo yake ni kuzomea au kutukanana.

Na kutika kufikia hitimisho lazima kuwe na mshindi ambaye atapatikana kwa uwingi wa kura kama kura itatumika kama kigezo, hii ndio demokrasia; Lakini wachache wanaweza kuwa na hoja nzito ambazo zinaweza kulegeza msimamo wa wengi. Lakini sio kufikia hitimisho kwa malumbano na matusi.

Wajumbe wanatakiwa wafahamu kuwa  misimamo binafsi na ya kichama hapa sio mahali pake; kama mwandishi mmoja alivyoandika kuwa “Inasikitisha kuona baadhi ya wajumbe wakitoa kauli zisizo na staha, wakishindana kwa hoja zisizo na mashiko na hata kusisitiza misimamo yao binafsi kwa ajili tu ya kukomoana, kutokana na tofauti za kiitikadi”.

 
Kwa kufanya hivi tuelewe fika kuwa waheshimiwa wajaumbe wa Bunge maalum watakuwa hawajefanikiwa kukonga roho za watanzania ambao kiu ya kupata katiba mpya na Bora;

Ni kweli kuwa wajumbe hawa walichaguliwa kutokana na ubora wao? Au wamechaguliwa kutokana na misimamo yao na vitisho ambavyo wamekuwa wakivionyesha kwa serikali ili kuwazima mdomo? Ndio maana tunashuhudia longo longo zaidi kuliko busara ya kiutendaji? Tulitegemea kuwa wangeanza safari hii ya miezi Mitatu kwa busara na hekima, kwa kuheshimiana na kwa kuzingatia zaidi hoja na kujadiliana kwa staaha na undugu na sio longo longo..

Kinachoendelea Dodoma ni kutegemea sana busara za wajumbe wachahce ambao wanaweza kulivusha bunge hili salama kama sio hivyo  liataendelea na longo longo na kupoteza mwelekeo.

Mwandishi mmoja aliwahi kuandika kuwa “Sisi kama watanzania tunatamani kujua viongozi wetu wanasimaia wapi na tujue mitazamo yao kisiasa.” Kinachopiganiwa na watanzania ni hiki  hoja ya wengi lazima iwe hoja yenye maslahi ya taifa na sio kunufaisha itikadi Fulani au kundi Fulani tu.

Itakuwa vizuri kuwa wajumbe watakao simama upande wa wengi  wahakikishe kuwa  wanantetea haki za wote na tuweke misingi itakayohakikisha kuwa maslahi binafsi au ya kichama hayatawali. Kwaq msingi huu nguvu ya walio wengi isiwe ya ubabe na dhuluma, bali iwe ni nguvu ya kweli na yenye kujitambua inayotaka kujenga utaifa na kujali raia wote na haki zao.

Longo longo  hizi zitokanazo na wajumbe ambao sisi tunawaona kuwa wana busara zinazoendelea kutolewa ndani na nje ya Bunge haziashirii mwisho mzuri. 

Kauli ya mheshimiwa Freeman Mbowe, ambayo aliitoa wakati longo longo na mabishano inaendelea imeonyesha busara “amesema kwamba bado wataendelea kushiriki kwenye vikao, ingawa wataendelea kupigania mageuzi ya msingi kwenye uendeshaji wa Bunge hilo ambalo linatakiwa kutoka na Katiba Mpya itakayopigiwa kura ya maoni ndani ya kipindi kisichozidi miezi miwili kutoka sasa”.

 Tatizo la wanansiasa na vyama vyao  kama mwandishi mmoja alivyoandika “Vyama vya kisiasa vimekuwa vinafikia muafaka katika mambo mbalimbali na kutoa taswira kwamba kuna muelekeo mzuri, lakini baadae wanasiasa haohao wanabadilika na kuyabadili maridhiano hayo na kuanzisha mijadala mipya inayoturudisha nyuma.”
 

Waheshimiwa wajumbe tunawaomba sana achane hizi  longo longo za kiitikadi ambazo hazina faida kwa Taifa na Amani yetu ambayo imedumu kwa miaka 50 sasa.

No comments:

Post a Comment