WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 2, 2014

BUNGE LA KATIBA NA FALSAFA YA MPE KAISARI YALIO YA KAISARI:



  • TIMIZA WAJIBU WAKO KWA JAMII YA TANZANIA KWA MAISHA YAO BORA na KWA VIZAZI VIJAVYO- falsafa ya kaisari;


Dhana ya uongozi wa namna yeyote ile unafaa uanzie nyumbani kwa kila mtu  uongozi ni uwezo wa kuweza kuyakabili kwanza yako mwenyewe na kufanya maamuzi sahihi bila kushawishiwa na mtu mwingine yeyote yule.

kwa kufanya hivyo utakuwa umefanikiwa kuyatawala maisha yako kulingana utaratibu ambao wewe mwenyewe umejiwekea kuanzia ndani ya familia yako;  ukifanikiwa hili unakuwa umefaulu katika mtihani huu wa kwanza wa uongozi ndipo jamii inapoanza kukuona kuwa hata ukipata nafasi ya  kuwaongoza wao pia utaweza kufanya maamuzi sahihi. 

 Kwa maneno mengine ni uwezo au njia ya kuweza kuwashawishi watu ili waweze kufanya kitu au kufikia lengo fulani la kikundi kwa ridhaa yao wenyewe. ili uongozi uwe bora ni lazima kuwe na kiongozi anayeongoza kundi fulani la watu au jamii husika.

Katika kila jamii kuna umuhimu wa kuwa na kiongozi kunatokana na ukweli kwamba watu wanapaswa kuwa na namna ya kuunganisha nguvu zao ili kufikia malengo yao. Katika  kila jamii, ni lazima kuwepo na mikakati ya kuunganisha nguvu, vipaji, uwezo na stadi mbalimbali za wana jamii. 

Wajibu wa msingi wa kiongozi yoyote ni kusaidia kuunganisha uwezo wa watu, kuratibu, kusimamia shughuli za watu, na kila inapobidi aonyeshe njia itakayosaidia kufikia lengo. Hii ndio dhana ya Bunge letu la Katiba ambalo limejengwa na watu wenye sifa na uzoefu tofauti tofauti ili watuletee katiba iliyo bora ambayo itaweza kudumu kwa vizazi;

Kwa dhana ya Plato uongozi ni dhana  au taaluma inayompa muhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale wanaoongozwa kuunganisha nguvu, stadi na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia malengo yao. Kuongoza ni kujua lengo la wale wanaoongozwa na njia ya kufikia lengo lao.

Uongozi bora una mchango mkubwa sana katika uimara wa jamii. Lakini tufahamu kuwa Ubora wa kiongozi unachangiwa na vitu vingi lakini tusisahau kuwa vile vile uongozi au kiongozi bora hutoka kwa Mungu. hivyo ndugu zetu wajumbe wa Bunge maalum la Katiba mjue kuwa mna dhamana nzito kwani mkiwatendea watanzania ndivyo sivyo adhabu yenu itatoka pande mbili kwa Mungu na kwa jamii iliyowachagua.

Leo hii wajumbe wa Bunge maalum la katiba ninyi ni viongozi muhimu sana ambao mtaingia katika vitabu vya kumbukumbu ya Taifa hili kuhusu katiba bora au mbaya kwa Taifa letu.  

swali la kuwauliza wajumbe wa bunge hili je wanajitahidi kumpa Kaisari yaliyo ya Kaisari au kuwatumikia wananchi waliowaweka katika nafasi hizo ambazo wanajivunia leo?

Je wajumbe  hawa wa bunge maalum kama viongozi muhimu wa Taifa hili leo hii  wanafahamu ukubwa na umuhimu wa maamuzi yao kwa jamii ya Tanzania?

Je Wajumbe wetu wa Bunge Maalum wanamalengo ya kufikia hatua ya juu kabisa ya ubora wa kutupatia Katiba Bora.? Inatakiwa wakumbuke kuwa Ni wajibu wa kiongozi kuwaongoza wana taasisi ili wafikie malengo yao. Kwa hiyo, kiongozi ni lazima aweze kubuni mikakati na mbinu zitakazoiwezesha taasisi anayoingoza kufikia malengo yake.

Je viongozi wetu wa bunge maalum wametawaliwa na maadili gani katika utendaji wa kazi yao hii Muhimu? Ili wakuliane katika hoja ni lazima wazingatia maadili ya msingi ya kufanikisha muafaka wa kitaifa kwa kujiepusha na unafiki kuficha hisia zao na kuwa kweli waaminifu katika hoja za msingi.

Je wajumbe wetu wa Bunge la katiba wamekuwa mifano miongoni mwao? Njia pekee ya kuonyesha ufano bora ni uwezo wa kuvumiliana katika hoja hata kama hoja hiyo huitaki tafuta jibu lililo bora, na sio kukataa hoja kwa kuzomea au kwa matusi huu sio msingi mzuri kwa kufikisha hoja au kufifisha hoja; 

kwa upande mwingine wajumbe wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kutimiza wajibu badala ya kujali maslahi yao binafsi yatokanayo na itikadi au faida ambayo wanafikiria wao tu watanufaika nayo;

  • Je wajumbe wa bunge maalum wanajifahamu mwenyewe au wanaburuzwa buruzwa tu kufuatia itikadi wananzofuata?

  • wanafahamu wananchi wanatamani nini au katiba iwe vipi?

  • wanajua namna katiba hii itaweza kustawisha maisha ya wananchi wao na kuendelea kudumisha amani iliyopo katika pande zote mbili za jamuhuri ya Muungano?

Hebu tujikumbushe Busara za Baba wetu wa Taifa  Mwalimu Nyerere alipozungumzia dhana ya uongozi, Mwalimu Nyerere alisema, “uongozi ni kuonyesha njia.” Kwa maana hiyo, viongozi shurti wafahamu vema matokeo ya uongozi wao. Wasome imani za wanaowaongoza na nyakati zilizopo ili kutambua matumaini ya umma kimaisha.

TATIZO LA WAJUMBE WA BUNGE  MAALUM LA KATIBA NI NINI ?

  • Wanaelekea zaidi kwenye propaganda za kisiasa zilizojaa kuchafuana huku wakiacha mijadala ya maana bila kuipa kipaumbele. Wamesahau kuwa  la msingi hapa ni kuwa kiongozi yeyote anayekuwa tayari kuongoza na anapochaguliwa  kuongoza popote, ajuwe anabeba jukumu la kubadilisha hali za watu kuwa nzuri. Atumie stadi za uongozi mwema kuonyesha njia.

  •  Inaelekea wajumbe wetu wa bunge bunge maalum wamejikita zaidi katika  kufikiria zaidi maslahi binafsi.  Wanaepuka kutumia stadi za uongozi kusimamia haki za waliowa wafikisha hapo hasa wanyonge. na. Wajikumbushe kuwa kupewa uongozi ni kuchukua ahadi ya kutenda kwa haki.

Mwalimu Nyerere aliandika miongozo mizuri katika Azimio la Arusha miongoni mwao  akisema kwamba ili tuendelee tunahitaji Siasa Safi na Uongozi Bora. Alitambua mchango wa mambo hayo katika maendeleo ya mwanadamu. Kupitia siasa safi kila kitu cha kunufaisha wananchi hupatikana. Bali ni muhimu viongozi wanaotarajiwa kufanikisha ustawi wa wanadamu, wapatikane kwa njia ya haki. Watokane na ridhaa ya watu wenyewe wanaotaka kuongozwa.

Hitimisho

Bunge maalum la Katiba lisitawaliwe na  malumbano ya mara kwa mara na matumizi ya lugha za kejeli na matusi; kwa kuendekeza tabia hiyo wananchi wanawaona wajumbe hawa wa bunge maalum wako zaidi kim kimasilahi na kiitikadi na kuto kubadilisha misamamo yao hata pale ukweli unapokuwa wazi.

Tunaendelea kuona kuwa wajumbe wengi waliochangia hoja wanafikiri malumbano yasiyo na msingi kwa Taifa letu leo hii na katika kipindi hiki muhimu sana. Itakuwa ni jambo nzuri kama wajumbe watajua matumizi ya muda ili kuepusha  mabaya ya rasilimali. Wanatakiwa kuweka mbele uzalendo wa Taifa hili na sio maslahi binafsi au ya kiitikadi.

MWENYEZI MUNGU IBARIKA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA UTUPATIE KATIBA ILIYO BORA KABISA KWA VIZAZI VYETU VIJAVYO.


No comments:

Post a Comment