WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, January 29, 2013

NENO LA LEO: HATA KIBOGOYO ANAWEZA KUKUUMA!


1 21de5

Ndugu zangu,
Nchi yetu inapita kwenye kipindi kigumu.  Kuna moto unafukuta, tumeshauona moshi mkubwa, ni ishara ya moto mkubwa. Tukikaa chini na kuitanguliza busara na hekima, basi, tuna nafasi ya kuizuia dhahma kubwa inayokuja. Na katika kuifanya kazi hii, bahati mbaya, muda si rafiki yetu. Muda unakwenda haraka.
Kibogyo ni binadamu asiye na meno. Hata hivyo, utafanya kosa kubwa kumdharau kibogoyo, kuwa hana uwezo wa kukudhuru kwa kutumia mdomo wake. Ukweli ni huu, kibogoyo akijawa na hasira, basi, anaweza kukuuma na hata  kukuachia alama mwilini.


Kuna hata wanadamu wenzako watakaokuuliza;
" E bwana, hii alama umeumwa na nini?". Na ukweli lazima utajulikana, hata kama utajaribu kuuficha. Kuwa umetiwa adabu na kibogoyo!
Mnyonge mwogope hata katika unyonge wake. Mara nyingi huwa hana cha kupoteza. Ukimkandamiza sana. Basi,  hata katika unyonge wake, anaweza kukutemea sumu kali. Ni sawa na mjusi. Ni kiumbe mdogo, lakini, mjusi ukimwandama sana anaweza kugeuka nyoka. Atakudhuru.
Ndugu zangu,
Wanadamu tumeumbwa na mdomo mmoja, macho mawili na masikio mawili. Aliyetuumba alikuwa na maana yake; kuwa tusiongee sana, bali, tuangalie zaidi. Tusikilize zaidi. Na wa kuwaangalia na kuwasikiliza zaidi ni wanadamu wenzako,, bila ya kuwabagua.
Na kwa kiongozi, ni wale unaowaongoza. Hata kama miongoni mwao kuna vibogoyo.
Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid Mjengwa,
Iringa.

No comments:

Post a Comment