WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, April 2, 2013

Nahodha awatolea uvivu mafisadi Zanzibar

 
Na Mwinyi Sadallah
 
Waziri Kiongozi mstaafu wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha, amesema hoja ya kuwapo au kutokuwapo kwa hati ya Muungano kusifute azma ya kuwashughulikia viongozi wanaokabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na ubadhirifu wa mali za umma Zanzibar .
Nahodha aliyasema hayo jana wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Mzalendo Mkoa wa Mjini Magharibi visiwani hapa.
Alisema ameshangazwa na baadhi ya viongozi wakitunisha misuli kuhoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wakati baadhi yao wakikabiliwa na tuhuma za unadhirifu ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka.
Alisema Zanzibar inakabiliwa na matatizo makubwa ya matumizi mabaya ya ardhi kwani viongozi wengi walijimegea kwa maslahi binafsi na wanajulikana.
Akifafanua zaidi alikiri kuwa kero za Muungano zipo na zinaeleweka ingawa alisema baadhi ya watu wakiwamo viongozi wanatumia mwanya huo ili kuficha tuhuma za ufisadi, uporaji na kujipatia utajiri usioelezeka.
"Kuhoji kuwapo au kutokuwepo kwa hati ya muungano baada ya miaka 49 kupita ni sawa na mtu kupatwa shaka kuhusu uhalali wa cheti cha ndoa ya wazazi wake, je ikiwa kimepotea kinaweza kubatilisha ndoa na uhalali wa mtoto,?"alihoji Nahodha
Alisema wanaotaka Muungano wa mkataba nia na lengo lao ni kuvunja muungano uliopo ili wapate nafasi ya kuatamia utajiri waliopata kwa kupora mali za wananchi na serikali yakiwamo majengo ya umma kinyume na sheria.
Aidha, aliwataka viongozi wa serikali na wanasiasa kujenga utashi na ujasiri wa kuhoji kwa nguvu ya hoja na kukemea vitendo vya ufujaji vilivyokithiri na kusababisha uchumi wa Zanzibar kutoimarika.
Alisema bado kuna vitendo hatarishi katika taasisi za serikali hivyo ni jukumu la kila mwenye ujasiri akapaza sauti yake badala ya kutumia muda mwingi kujificha kwenye kivuli cha hati ya Muungano.
Nahodha ambaye pia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa alisema Serikali ya CCM itaendelea kutetea msimamo wake wa muundo wa Serikali mbili na kushughulikia kasoro na utatuzi wa kero zilizopo katika Muungano bila kuyumbishwa na kundi lolote.
Akizungumzia upotevu wa Sh. bilion 20 katika Shirika la Umeme Zanzibar(zecco), alisema fedha hizo ni nyingi na zingeweza kutumika kusukuma maendeleo ya kisekta na badala yake akasema zimepotea katika mazingira ya kutatanisha.
"Tusijifiche chini ya kivuli cha hati ya muungano wakati baadhi yetu mikono yetu inachuruzika michirizi ya uporaji, wizi na ubadhirifu wa mali za umma na uvunjaji wa sheria,"alisema Nahodha huku akishangiliwa.
Akilizungumzia suala la vijana kukosa ajira, alisema ni hatari kulisahau kundi hilo la vijana kwa kuwa ndiyo lenye nguvu na ushawishi.
"Chama chetu kihakikishe kinachemsha bongo na kulishika kundi hilo, lipewe nafasi katika medani za uongozi wa leo, kujengewa uwezo ili liwe jeshi imara litakalokabili mapambano na kuwashinda maadui,"alisema Nahodha .
Matamshi ya Nahodha yamekuja huku Serikali ikiwa bado haijatekeleza ripoti tatu za Baraza la Wawakilishi za kuchunguza matumizi mabaya ya madaraka na ubadhirifu ikiwamo uuzaji wa ardhi kwa maslahi binafsi na majengo ya Serikali.
Ripoti ya kwanza ilihusu uuzaji wa majengo katika hifadhi ya mji wa urithi wa dunia katika mji mkongwe aa Zanzibar, kisiwa cha changuu kilichokodishwa kwa bei ya kutupa,ubadhirifu katika Zecco na Baraza la Manispaa Zanzibar.
Ingawa ripoti zote zimesema kuna viongozi na watendaji wanaotakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kuuza mali za serikali kwa kutozingatia sheria ya manunuzi na ugavi lakini hadi sasa hakuna kigogo yeyeto aliyefikishwa mahakamani
 
Chanzo - Nipashe

No comments:

Post a Comment