WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 24, 2013

Msigwa: Kigogo wa CCM anauza pembe za ndovu




Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, Iringa.  
 Mbunge wa Mbeya mjini- Joseph mbilinyi aka Sugu akiunguruma kwenye mkutano mkubwa  wa hadhara wa chadema kwenye viwanja vya  Uwanja wa Mwembetogwa iringa jana
  Mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika akihutubia mamia yawatu waliofurika katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika vinwaj vya Mwembetogwa mjini Iringa
 Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Slaa Akiunguruma mbele ya mamia ya wafuasi wa chadema kwenye mkutano mkubwa wa hadhara kwenye viwanja vya Uwanja wa Mwembetogwa iringa jana
 Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Slaa Kushoto akipitia katiba kwenye mkutano mkubwa wa hadhara uliyofanyika iringa jana kulia kwake ni mbunge wa jimbo la ubungo Mh John Mnyika
 Sehemu ya mamia ya wafuasi wa chadema wakisiliza hotuba mbalimbali kutoka kwa viongozi mbalimbali wa chama hicho viwanja vya Uwanja wa Mwembetogwa iringa jana. Picha Zote na Chadema na Said Ng’amilo


Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, Iringa. Picha na Said Ng’amilo 

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amemlipua kigogo mmoja wa juu wa CCM (jina tunalihifadhi kwa kuwa hakupatikana kujibu tuhuma hizo), kuwa ndiye kinara wa biashara haramu ya pembe za ndovu na utoroshaji wa wanyama nchi za nje.
Akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Mwembetogwa, Iringa jana, Mchungaji Msigwa alisema anashangaa Serikali ya CCM kushindwa kumchukulia hatua.
Mchungaji Msigwa alidai kuwa tembo wapatao 75 wamekuwa wanauawa kila siku kutokana na tatizo hilo kufumbiwa macho na Serikali.
Alidai kuwa pamoja na Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige kujiuzulu mwaka jana kutokana na kashfa ya kutorosha twiga, Serikali ilitakiwa kuwafuatilia wahusika wote.
“Kinara wa biashara haramu ya uuzaji wa pembe za ndovu anajulikana, sasa inakuwaje Serikali inashindwa kumkamata?” alisema Msigwa na kuahidi kulipua mabomu zaidi atakaporudi bungeni kwa maelezo kuwa anao ushahidi wa suala hilo.

Huo ulikuwa mkutano wa mwendelezo wa wabunge wa Chadema waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kuwapasha wananchi sababu ya kuchukuliwa hatua hiyo.
Wabunge hao walisimamishwa na Naibu Spika, Job Ndugai kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuwazuia askari wa Bunge kumtoa nje ya ukumbi, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu. Wabunge waliosimamishwa pamoja na Lissu ni Godbless Lema (Arusha Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini), Ezekiah Wenje (Mwanza Mjini) na Msigwa.

Hata hivyo, Lema na Lissu hawakuwapo katika mkutano huo wa jana ambao pia ulihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.

Mnyika kutoa hoja binafsi
Katika mkutano huo, Mnyika aligawa fomu kwa wananchi kuomba aungwe mkono wakati atakapotoa hoja binafsi bungeni juu ya mfumuko wa bei na umaskini nchini.
Mbunge huyo alisema wananchi wanakabiliwa na maisha magumu kutokana na hali mbaya ya uchumi.

“Napata uchungu ninavyoona Watanzania wakiishi maisha magumu kwa hiyo naandaa hoja binafsi ya kuwasilisha bungeni ili umma uelewe umuhimu wa suala hili,” alisema Mnyika na kuongeza kwamba atagawa fomu hizo kila atakapohutubia mikutano ya hadhara.

Dk Slaa na Usalama wa Taifa
Katika mkutano huo, Dk Slaa alidai kuwa maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa wamegawanyika kutokana na makundi ya wanaotaka kuwania Urais mwaka 2015 kupitia CCM.

Dk Slaa alisema mgawanyiko huo ndiyo chanzo cha siri nyingi za idara hiyo kuvuja.
Aliwatuhumu baadhi ya wanachama wa CCM akidai kuwa wamekuwa wakiwavuta baadhi ya maofisa katika idara yao ili kuwasaidia kwenye harakati zao.
 
source: mwananchi

No comments:

Post a Comment