WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 13, 2013

YANGA YAUKARIBIA UBINGWA



mashabiki-wa-yanga1 0beea
Yanga imezidi kujichimbia kileleni katika mbio za kusaka ubingwa wa Ligi Kuu baada ya wachapa JKT Oljoro mabao 3-0. Aliefungua kitabu cha magoli alikuwa Nadir Haroub 'Cannavaro' katika dakika ya 5 ya mchezo. Simon Msuva aliandika bao la pili kabla ya Hamis Kiiza kuandika bao la tatu na kuifanya Yanga iende mapumziko ikiwa mbele kwa mabao matatu. Kipindi cha pili kilishuhudia Said Bahanuzi akiingia kuchukua nafasi ya Didier Kavumbagu na Nizar Khalifan kuchukua nafasi ya Simon Msuva katika dakika ya 78 lakini JKT Oljoro ilionekana kuimarisha safu yake ya ulinzi na hadi mwisho matokeo yakisomeka 3-0

source: Mjengwa blog

No comments:

Post a Comment