WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 24, 2013

Wagombea binafsi watokane na vyama

 
CHARLES Montesque ni mwanafalsafa mkongwe aliyezaliwa mwaka 1689 nchini Ufaransa. Ndiye  aliyejenga hoja ya kuwa na dola yenye mihimili mitatu huru.

Kwa mujibu wa Montesque, Dola haina budi kutenganisha mamlaka ya taasisi hizi tatu. Ni muhimu kwa mihimili hii mitatu kuwa huru. Ifanye kazi kwa kujitegemea. Kuwepo pia na mazingira ya mikono yote mitatu kudhibitiana.

Mihimilimitatu ya dola ni; Utungaji sheria (Bunge) Utawala (Serikali) na Hukumu (Mahakama). Kuna wenye hoja ya kwamba mikono hii mitatu iwe na ushirikiano wa karibu.

Montesque anapingana na hoja hiyo, anaamini kutenganisha mamlaka ya mihimili hii mitatu ya dola kunaipa  uhuru kamili wa kufanya kazi zake bila kuingiliana. Hilo ni muhimu ili kuwepo na utawala bora uliojengeka katika misingi ya haki.

Katika nchi zetu hizi tunahitaji rais (serikali) yenye nguvu za kikatiba, bunge lenye nguvu za kikatiba na mahakama huru yenye nguvu za kikatiba. Mahakama zenye majaji wasioteuliwa na rais. Kwamba mikono hii mitatu iwe huru na yenye majukumu ya kudhibitiana kwa maslahi ya nchi. Tuandae katiba yenye kulipa bunge  uwezo zaidi wa kufanya maamuzi ya kikatiba. Bunge ndilo mwakilishi wa wananchi.

Tuwe na Mahakama Kuu Huru ya Katiba. Mahakama yenye jukumu la kutafsiri sheria na maamuzi yote yaliyofikiwa na Bunge. Mahakama ya Katiba iwe ni chombo cha juu kitakachoshughulikia mashauri ya ukiukaji wa sheria na maamuzi ya Bunge. Iwe na uwezo wa kisheria wa kupitisha hukumu kwa kuzingatia sheria za nchi bila kuathiriwa na Serikali au Bunge.

Kwa mujibu wa Montesque, kama bunge halitakuwa na nguvu, kuna hatari ya bunge hilo kuchukua nafasi ya serikali na kwa maana hiyo utaratibu mzima wa mgawanyo wa madaraka ya dola kwa mihimili hii mitatu utakufa.

Montesque anabainisha pia; kuwa endapo mawaziri ambao ni watekelezaji wa maamuzi ya bunge watatoka miongoni mwa wabunge, basi, hakutakuwa tena na uhuru, kwani serikali yenye mamlaka ya utekelezaji itakuwa imechanganyika na bunge.

Rais apewe madaraka ya kuchagua mawaziri, lakini, watoke nje ya bunge. Hata kama rais atamteua waziri ambaye pia ni mbunge, basi, mbunge alazimike kuachia kiti chake cha ubunge na atafutwe mwakilishi mwingine wa wananchi. Haiwezekani kutumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja.

Na kuna hoja hii ya kuwapo ama kutokuwapo kwa wagombea binafsikatika chaguzi zetu.  Tunapaswa kujiuliza;je, ni wakati sasa wa kuwa na wagombea binafsi? Swali hilo linatutaka kuumiza zaidi vichwa vyetu. Maana, maamuzi yatokanayo na vifungu vya sheria ya vitabuni ni jambo moja, lakini hali halisi katika jamii tunayoishi ni jambo jingine kabisa.

Kwa kuziangalia jamii nyingine na kulinganisha na hapa kwetu, mimi nadhani,kuwa nchi yetu haijawa tayari kuruhusu wagombea binafsi katika utaratibu usiotokana na vyama vya siasa.

Nasema hivi kwa kuzingatia kuwa nchi yetubado ni changakidemokrasia. Demokrasia hukua kulingana na hali halisi ya nchi.Ni vema na ni busara kwawagombea binafsi wakatokana na vyama na waruhusiwe tu katika nafasi ya udiwani, ubunge na useneta, na si katika nafasi ya urais. 

Kwa kuweka msisitizo; kusiwe na mgombea binafsi katika nafasi ya urais. Mgombea urais kikatiba atokane na chama cha siasa. Apitishwe na idadi ya wanachama itakayokubalika, mathalan, awe ni Mtanzania aliyepigiwa kura na kupitishwa na wanachama wa chama chake wasiopungua 1,000.

Tusiruhusu mazingira ya Mtanzania aamke tu Kamachumu au Masaki na amwambie mkewe au mumewe kuwa; “ Naenda kuchukua fomu ya kugombea urais!”.Katika mazingira ya nchi zetu hizi, huko ni kukaribisha uwendawazimu, na mwishowe ikulu zetu zitakaliwa na wendawazimu au watu wasio hata na uwezo wa kuongoza klabu ya soka lakiniwana pesa, umaarufu na mbinu za kufika ikulu.

Hivyo basi, Katiba ijayo ingewekautaratibu wa kuruhusumgombea binafsi anayetokana na chama cha siasa katika ngazi ya udiwani, ubunge na useneta, si urais.

Katika utaribu huu wanaonawania ubunge katika jimbo X watapigiwa kura na wanachama wenzao katika idadi ya wanachama itakayokubalika. Atakayeongoza katika kura atakuwa ni mgombea ubunge kuwakilisha chama chake.Huyo atapewa pia msaada wa kukampeni na chama chake ikiwamo fedha za kampeni.

Mgombea ubunge huyo atatambuliwa rasmi na chama chake. Lakini wagombea wengine walioshindwa katika kura wana hiari ya kusimama wenyewe kama wagombea binafsi. Wajinadi wenyewe na kwa gharama zao na bila kupigiwa debe na chama chao. Wakibahatikakuchaguliwa na wananchi na kuingia bungeni, basi, wataingia bungeni kama wagombea binafsi lakini wakiwakilisha itikadi na sera za vyama vyao.

Utaratibu wa wagombea binafsi wanaotokana na vyamautasaidia pia kuimarisha vyama vya siasa. Tumeamua kuingia katika mfumo wa vyama vingi na si mfumo wa wagombea wengi binafsi. Chama ni wanachama na vikao vya chama. Ni itikadi na sera.

Kuruhusu mgombeabinafsi asiyetokana na chama ni kuhujumuna kupoteza maana nzima ya uwapo wa siasa za vyama vingi. Na swali ni je, hatuoni kuwa umefika wakati wa kuondokana na uchaguzi wa rais na badala yake rais atokane na chama kilichopata kura nyingi? Hili nalo linajadilika.

source: Raia Mwema :Maggid





 

No comments:

Post a Comment