WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, April 8, 2013

Dk Salim ataka Serikali kukomesha vurugu

 
Na Nuzulack Dausen, Mwananchi

 Dar es Salaam. Mwanadiplomasia mkongwe nchini, Dk Salim Ahmed Salim amesema amesikitishwa na vitendo vya vurugu za dini zinazoendelea na kuzitaka mamlaka husika kudhibiti hali hiyo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, baada ya kumalizika Kumbukumbu za mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda miaka 19 iliyopita, Dk Salim alisema hali hiyo inatakiwa kudhibitiwa mapema kabla amani haijatoweka.

Dk Salim ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU), alisema kila Mtanzania ana wajibu kuhakikisha anadhibiti uchochezi na vurugu za kidini, ili kulinda amani ya nchi ambayo imedumu kwa muda mrefu.

“Vurugu za dini ni jambo la kusikitisha na hatari sana, nchi hii ni ya Watanzania wote bila kujali itikadi za imani, hivyo tunatakiwa kulitatua tatizo hili mara moja,” alisisitiza Dk Salim.

Alisema Serikali, viongozi wa vyama vya siasa, taasisi za dini, taasisi za kiraia na wananchi hawana budi kukaa pamoja kuhakikisha wanalitatua tatizo la migogoro ya dini linalotaka kuvuruga amani ya nchi.
Alisema kuna haja ya kuendeleza jitihada za kulitatua tatizo hilo mara nyingi zaidi ya hatua iliyofikiwa, ili kulinda mustakabali wa nchi.

Wakati huohuo, Dk Salim alizitaka nchi za bara la Afrika kuwa chachu ya kutatua matatizo ya ndani ya bara lao, badala ya kutegemea watu kutoka nje.
Dk Salim alisema nchi za Afrika zinatakiwa kuwajibika ipasavyo kwa matendo yao, kwa kutafuta suluhu haraka iwezekanavyo siyo kutegemea taasisi kutoka nje ya bara.

“Lazima watafute suluhu za matatizo ambabyo yanawakabili, wahakikishe wanayadhibiti haraka ipasavyo kabla hayajafikia mahali pabaya” alisisitiza.
Kwa upande wake, Balozi wa Rwanda nchini, Dk Benjamin Rugangazi alisema maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya halaiki ni salamu kwa ulimwengu mzima katika harakati za kudumisha amani na upendo, ili kuzuia mauaji kama hayo yasitokee tena. 
 
source: mwananchi

No comments:

Post a Comment