WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 27, 2013

Miaka 49 Ya Muungano Uwanja wa Uhuru

 


 Sehemu ya wananchi waliojitokeza kushuhudia sherehe hizo.
 Rais Jakaya Kikwete, akiingia uwanja wa Uhuru akiwa ndani ya gai la wazi wakati alipowasili uwanjani hapo kwa ajili ya kuwaongoza wananchi katika shambra shambra za sherehe za miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange. Katika kuadhimisha sherehe hizo, Rais Kikwete, ametoa msamaha kwa wafungwa wapatao 4180 kwa nchi nzima, huku msamaha huo ukiwa hauwahusu, Wafungwa wanaotumikia kifungo cha maisha, Kifungo cha ubakaji, wezi wa magari, Rushwa, Matumizi mabaya ya Madaraka na Kunyongwa.

 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride la heshima wakati wa sherehe za miaka 49 ya Muungano kwenye Uweanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam jana
Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume (kulia) akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa
 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idii (kulia) akisalimiana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Othmani Makungu
Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein (kulia), Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Shalif Hamad wa pili kutoka (kulia), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Othmani Ramadhani Makungu wakiwa katika maadhimisho   hayo.
 Rais Jakaya, akisalimiana na baadhi ya viongozi baada ya kuwasili uwanjani hapo.pichani akisalimia na makamu wa Rais Dr Gharib Bilal
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bila, Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, Mama Karume na baadhi ya viongozi wakisimama kumpokea Rais Kikwete wakati akiwasili uwanjani hapo.
 
 Viongozi wa kiatifa wakimba wimbo wa Taifa. Kutoka kushoto, Rais mstaafu, Ali Hassani Mwinyi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, Rais Jakaya Kikwete, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange, Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Rais mstaafu Benjamin Mkapa na  Mama Fatma Karume.
 Askari wa Jeshi la Magereza wakipita mbele ya jukwaa kuu kwa mwendo wa haraka na kutoa heshima. 


   Jeshi la Wanamaji (Nevy)

 Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Kikwete jana.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais na Issa Michuzi-IKULU

No comments:

Post a Comment