WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, April 5, 2013

Taasisi ya Sayansi za Bahari cha Buyu chahitaji bilioni 14



 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo kwa Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi ya Sayansi ya Bahari Dkt Narriman Jiddawi juu ya Utunzaji wa Samaki Aquarium wakati wa Ziara ya waziri huko Zanzibar
 
 Mhadhiri Mwandamizi wa Tasisi ya Sayansi ya Bahari ya Chua Kikuu cha Dar es Salaam Dkt NarrimanJiddawi akimuonyesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan aina ya Kasa katika chumba cha Kutunzia samaki[AQUARIUM}wakati wa Ziara ya Kutembelea Tasisi za jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja .
 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo juu ya Ujenzi wa Kituo cha tasisi ya Sayansi za Bahari kilichopo Chukwani Unguja kwa Kaimu Mkurugenzi Dkt Christophet Muhando wakati waziri alipofanya Ziara ya Kutembelea Tasisi za Jamhuri za Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja [PIcha na Ali Meja]   
 
Kaimu Mkurugemzi waTaasisi ya Sayansi ya Bahari ya chuo kikuu cha Dar es Salaam Dkt Christopher Muhando akimtembeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Jengo la Taasisi ya Sayansi ya Bahari huko Chukwani Mjini Unguja wakati wa Ziara yakutembelea taasisi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

ZAIDI ya shilingi bilioni 14 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa chuo cha Taasisi ya  Sayansi za Bahari kilichopo Buyu wilaya ya Magharibi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Hayo yamesemwa leo huko Forodhani mjini Zanzibar na Muhadhiri Dkt. Ntahondi Nyandwi wakati alipokuwa akisoma ripoti ya chuo hicho na rasilimali zake mbele ya Waziri anae shughulikia masuala ya Muungano Samia Suluhu Hassan aliyekuwa katika mfulilizo wa ziara yake kuzitembelea Taasisi za muungano hapa Zanzibar.

Amesema fedha hizo zitahitajika ili kukamilisha ujenzi wa  jengo lote na miundombinu  ikiwemo vifaa vya maabara, sehemu za wanafunzi wa uzamili, zamivu, kumbi za mikutano, ofisi za programu za kimataifa, ofisi za wageni wa kimataifa na mengineyo.

Dk. Nyandwi amesema kupatikana kwa fedha  hizo kutakamilisha mahitaji hayo na mengine ambapo kwa sasa ujenzi huo umefikia  hatua nzuri  na wameshatumia zaidi ya bilioni nne  kwa kujenga miundo mbinu mbalimbali ikiwemo  ofisi za viongozi na madarasa.

“Kwa vile pesa za kumlipa mkandarasi hazikupatikana kwa wakati na hakukuwa na uhakika kuzipata, ujenzi ulisimama Agosti 2008 na mkandarasi aliondoka lakini kwa sasa ujenzi unaendeleo taratibu”alisema Nyandwi . Aidha alifahamisha kuwa ujenzi huo unaendelea kidogo kidogo  kadri fedha zinavyo patikana baada ya kumuomba mkanda rasi awapunguzie gharama na kuweza kumaliza mipango ya awamu ya kwanza na ya pili. 

Nae Waziri wa  Nchi Afisi ya Makamu wa Rais,  Muungano  Samia Suluhu Hassan  amesema kuwa atamuagiza Mkuu wake wa kazi kuja Zanzíbar  kujionea na yeye   Jengo hilo hatua ilio fikiwa.

Aidha alisema kua ujenzi huo utaendelea kidogokidogo mpaka utapomalizika. Maendeleo ya ujenzi wa Taasisi ya sayansi Baharini ni moja ya Taasisi za Chuo  Kikuu cha Dar-es Salaam kampasi  ya Mwalimu Nyerere ambapo umuhimu wa Taasisi hiyo ulianza kujitokeza Mwaka 1978 chini ya sheria Na. 12 ya 1970 ya chuo kikuu cha Dar-slamu kwa tamko la Serikali Na. 34 lililo pitishwa tarehe 16 march 1979.

Chuo hicho kumalizika kwake kufanya kazi za kutafiti nyanja zote za Sayansi za Baharini, kutoa mafunzo ya uzamivu, uzamili katika sayansi ya Bahari ,kutoa ushauri wa kitalamu ,kutoa mafunzo ya Shahada ya kwaza  kwa kulingsana na mahitaji ya  Taifa la Tanzania   kama sehemu ya Taluma kwa vitendo.


IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR LEO 5/4/2013

No comments:

Post a Comment