WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 24, 2013

Shein: Siiongozi Z'bar kwa shinikizo la mtu

 
Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.
Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, amesema hatoongoza serikali yake kwa shikinikizo la mtu au kiongozi yeyote.
Aidha, amewashangaa wanaohoji sababu za yeye kutowateua wakuu wa wilaya na mikoa wapya tangu achaguliwe kuwa Rais mwaka 2010.
 
Rais Shein aliyasema hayo wakati akiwahutubia wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika Amani Mkoa wa Mji Unguja.
 
Alisema kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, yeye ndiye Rais baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na ndiye aliyewateua Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais kuwa wasaidizi na washauri wake.
 
Aidha, alisema kutokana na nguvu za kikatiba na kisheria alizonazo, anaweza kumuondoa yeyote katika uteuzi wake bila ya kuvunja na kikuika sheria ikiwa hataridhishwa na utendaji wa kiongozi aliyemteua.
 
Kauli ya Dk. Shein, ilionekana ni kama kumpiga `kijembe' Makamu wake wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye aliwahi kutamka katika mkutano wa hadhara Fuoni katika uwanja wa Magirisi kuwa hawezi kufukuzwa kazi na Rais.
 
“Mimi ndiye mshindi wa urais wa Zanzibar mwaka 2010, nimeunda serikali na kuteua Makamu wa Kwanza na wa Pili ili kunisaidia kazi na kunipa ushauri, nimetengeneza wizara na kuteua mawaziri na naibu mawaziri bila ya kupangiwa na mtu na wakati wowote naweza kumuondoa yeyote,” alisisitiza.
 
Tangu kuchaguliwa kwake, Dk. Shein ameendelea kubakia na wakuu wa mikoa na wilaya wale wale aliowateua Rais wa awamu ya sita, Amani Abeid Karume na kufanya mabadiliko madogo katika Wilaya ya Kati na Kaskazini `B’ kati ya wilaya 10 za Unguja na Pemba.
 
Kutowateua wakuu wa wilaya na mikoa, kumewahi kuhojiwa mara kadhaa na baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa nyakati tofauti wakiwa kwenye vikao vya Baraza. Rais Dk. Shein alisema ana uzoefu na maarifa ya kutosha katika masuala ya uongozi na anapenda kuheshimu Katiba na kufuata sheria na hapendi kukurupuka au kusema kutokana na watu wanavyosema mitaani na kwenye majukwaa ya kisiasa.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment