WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, December 31, 2012

SALAMU ZA MWAKA MPYA 2013 KWA TAIFA LETU.


  • KUTHUBUTU KWA VIONGOZI WETU KWA FAIDA YA WANANCHI


 


Kauli ya Baba Wa Taifa Mwalimu Nyerere "TUMUACHE BADO AKUWE KIDOGO"

  • Inatufundisha nini katika maendeleo ya taifa hili na viongozi ambao wanashindwa kuchukua uamuzi mara moja?


Ili tuweze kuendelea tunahitaji, pamoja na mambo mengine yote  swala la uongozi bora ni muhimu sana;

  • Je viongozi wetu wako tayari kutoa maamuzi magumu kwa faida ya watanzania bila woga?


  • Je Viongozi wetu bado wana Utamaduni wa kuogapa kuwajibika katika utoaji maamuzi kwa ajili ya kikundi fulani cha watu?


  • Je Viongozi wetu wanaweza kuthubutu wakati wanapo takiwa kuwajibika kufanya mambo kwa kuangalia masilahi watanzania walio wengi hata kama yatawauzi na kuwakwera wachache wenye nguvu kama alivyokuwa akifanya Hayati Edward Moringe Sokoine?


Ni ukweli ambao haupingiki tukiangalia maelekezo ya Wanafalsafa kuwa “kukaa kimya bila kutolea msimamo wako katika jambo fulani maana yake ni kwamba unakubali au unapinga ila unao woga wa uwazi”.  Na kama viongozi wetu wana tabia hii ni kasoro kubwa; kama wahenga walivyotuambia kuwa; “ngoja ngoja huumiza matumbo” tukingoja kufanya maamuzi tunaruhusu mawazo mabaya toka kwa wamanchi wenye hasira pale ambapo kuna kuwa na tatizo. 

  • Mwalimu J.K.Nyerere aliwahi sema  "Hatuwezi tukawa kweli chama cha watu ikiwa hatujishughulishi na shida za   kawaida za watu wetu".Tujiulize,Je viongozi tulionao ambao hawajishughulishi na shida zetu, wapo kwa ajili ya nani?


Ni ukweli kuwa “Hekima na busara huzaa mafanikio ya uongozi bora, lakini machafuko ni udhaifu wa uongozi”

Mkongwe wa siasa Mahatma Ghandi, aliwahi sema,   “tufikirie kesho lakini tutende kwa ajili ya leo.Hivyo mustakbali wa maisha yetu ya kesho yatategemea maamuzi sahihi ya leo”.
Kama taifa nini tunahitaji?

  • vyama vya siasa vyenye nguvu na vyenye kuheshimu demokrasia,

  • Bunge lenye nguvu za hoja lisilitawaliwa na itikadi ya chama chochote! Viongozi wenye kufikiri kwa faida ya wananchi


  • Viongozi wanaweza kusimamia sheria


Rais Mstaafu awa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa aliwahi kutamka hili kuwa sisi watanzania ni wagumu wa kufikiri;

Swali langu hapa Mheshimiwa Mkapa kama Rais mtaafu nini kilimsukuma yeye kutoa kauli hii?

Je ni ugumu wa kuyakabili matatizo ya maisha au kama ndugu yetuJuvenalis Ngowi alivyowahi andika kuwa “Bahati mbaya ni kwamba inawezekana uvivu wetu huu wa kusoma mambo magumu ndio unatuingiza “mkenge” hata kwenye mambo muhimu ya kitaifa kama mikataba. Inafika mahali tunaingia mikataba ya kusikitisha kiasi cha kujiuliza hivi Mwenyezi Mungu aliwapa watu hao ubongo wa nini? Maana uti wa mgongo pekee ungewatosha watu hao”.

  • Ndipo tunapoukumbuka wosia wa baba wa taifa’ "TUMUACHE BADO AKUWE KIDOGO" 


Kama wananchi ambao ni sehemu ya kuwachagua hawa viongozi nafikiri inatupasa tuondoe uvivu wetu wa kufikiri, tuamke sasa na tuache itikadi za kuwaacha kuwapa madaraka mtu yeyote ambaye inaonekana wazi kuwa bado hajapata utashi wa kuwa kiongozi bora wa kuwatumikia wananchi wake.

Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema - Ukiweka dodoki kwenye maji safi litanyonya maji safi! Ukiliweka kwenye maji taka, kadhalika litanyonya maji taka! Hapo ndipo tulipo! Uvivu wetu wa kufikiri pengine huleta tatizo hili.

Sisi wadau wa kuwaweka madarakani tukisimamam imara tutawafanya viongozi wetu kuweza kuthubutu au kuchukua maamuzi ambayo watawasaidia na kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi na kulinda  mali ya umma kwa nguvu zote, bila kujali kitu chochote. 

 Nafikiri viongozi wetu wa sasa  wanatakiwa kufuata busara na umakini ambao marehemu Sokoine alikuwa nao katika uongozi wake Kwanini, wasikubali kujifunza kwake waone matokeo yake? Kama kuna maamuzi magumu inatakiwa wayafanye; mbona Sokoine alifanya na kuwafanya wahujumu uchumi kuiogopa serikali na kusalimu amri?

Viongozi wetu wanaweza kwani tunaimani kuwa kwa sasa wameshakuwa kifikra na utendaji unaozingatia misingi ya haki na kujali maendeleo ya watanzania wanyonge ndio maana tumewakabidhi nchi;

Mungu libariki Taifa letu hasa katika mwaka huu qa 2013 kwa faida ya watanzania wote na sio kikundi kidogo cha watu ndani ya Taifa.

No comments:

Post a Comment