WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, December 22, 2012

Dk Slaa amwagiza Lema ‘ambane’ Pinda bungeni


 Dk Willibrod Slaa
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemuagiza Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya chama hicho, Godbless Lema wakati atakapokwenda Bungeni, kufufua hoja kuhusu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kulidanga Bunge Febuari 10 mwaka huu.

Dk Slaa alitoa agizo hilo jana makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na wafuasi walioandamana wakishangilia Lema kurejeshewa ubunge wake jana na Mahakama ya Rufaa.

Dk Slaa alisema huu ni wakati wa Lema kwenda kufufua hoja ya kwamba Waziri Mkuu alilidanganya Bunge kwani tayari udhibitisho wa jambo hilo ulikuwepo.
“Nakuagiza sasa Lema utakapo kwenda Bungeni uende ukambane Waziri Mkuu kwa kulidanganya Bunge kwani Spika wa bunge alisema hoja hiyo imefungwa kwa sababu ya wewe kutokuwepo bungeni,” alisema Slaa.

Waziri Mkuu Pinda akijibu swali bungeni aliseme chanzo cha vurugu zilizosababisha vifo mjini Arusha ni ni uamuzi wa madiwani wa Chadema kutokubali kushindwa katika uchaguzi wa jiji hilo.

Pinda alitoa kauli hiyo Febuari 10 mwaka huu wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliyetaka kujua msimamo wa Serikali kuhusu mauaji ya raia yaliyofanywa na Polisi wakati wa vurugu zilizotokea Arusha.

Kutokana na majibu hayo, Lema kabla ya ubunge wake kutenguliwa na mahakama, aliomba kupewa mwongozo wa spika akidai kwamba Pinda alikuwa amelidanganya Bunge.

Spika wa Bunge Anne Makinda hajawahi kutoa mwongozo kuhusu suala hilo na aliwahi kusema kuwa suala hilo limefungwa kwani aliyeuliza hayupo tena bungeni.

CHANZO:MWANANCHI

No comments:

Post a Comment