WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, December 25, 2012

Mandela Kusalia Hospitalini Krismasi



Serikali ya Afrika Kusini imetangaza kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Nelson Mandela atasalia hospitalini msimu huu wa Krismasi.

Bwana Mandela ambaye ni rais mweusi wa kwanza nchini Afrika Kusini, alilazwa hospitali wiki mbili zilizopita kufuatia maambukizi ya mapafu na uvimbe au mawe kwenye kibofu.
Kuna wasi wasi mkubwa nchini Afrika kuhusu afya yab rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 94.

Mandela alifungwa miaka 27 baada ya kupatikana na hatia ya kuongoza uasi dhidi ya serikali ya Wazungu walio wachache nchini humo.

Raia wengi wa nchi hiyo wanamuona kama baba wa taifa kutokana na juhudi zake ya kupigania uhuru wa taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na serikali, Bwana Mandela atasherehekea siku kuu ya Krismasi akiwa hospitalini.

Mwandishi wa BBC, mjini Johannesburg, anasema kila kukicha kuna hali ya wasi wasi kuhusu afya ya rais huyo wa zamani.

Awali kulikuwa na matumaini kuwa Bwana Mandela huenda akaruhusiwa kwenda nyumbani, lakini madaktari wake wanasema hawako tayari kumruhusu Bwana Mandela kwenda nyumbani.

Licha ya rais Zuma kutangaza kuwa Afya ya rais huyo wa zamani sio nzuri sana, Rais Zuma amesema anaendelea kupata nafuu.

Serikali ya Afrika Kusini imesema Mandela anatibiwa kufuatia maambukizi ya Mapafu katika hospitali moja mjini Pretoria.

                            BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment