WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, December 28, 2013

SMZ haina uwezo kifedha-Nahodha

“Kama Muungano unavunjika leo, Wazanzibari laki tatu waliokuwepo katika mikoa ya Tanzania Bara watakwenda kuishi wapi,” Nahodha 
Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi

Zanzibar. Waziri Kiongozi mstaafu Shamsi Vuai Nahodha amesema mfumo wa Muungano wa Serikali tatu unaweza kutetemesha misingi yake na kusababisha kuvunjika, kwa vile Zanzibar haina uwezo wa kirasilimali kuchangia uendeshaji wake.
Nahodha ameyasema hayo kwenye mkutano wake wa hadhara uliofanyika kwenye Viwanja vya Alabama, Mwembeshauri, ambao ni wa kwanza tokea uteuzi wake wa wadhifa wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa utenguliwe.
Nahodha alisema kwamba kutokana na vyanzo vya mihimili ya uchumi wa Zanzibar kuwa vichache haitaweza kuchangia gharama za uendeshaji na kutoa mfano wa bajeti ya wizara moja ya Ulinzi inayotumia Sh1.2 trilioni, wakati Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ikitumia Sh800 bilioni kwa mwaka kunakopita bajeti nzima ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambayo hutumia Sh600 bilioni kwa mwaka.
Nahodha alisema kama Zanzibar ingekuwa na uwezo wa kumudu gharama hizo ingeweza kuboresha mishahara ya askari wake wa Vikosi vya SMZ na kuwapa mikopo ya elimu ya juu wanayoomba kila mwaka kutaka kuendelea na masomo.
“Vyanzo vya Zanzibar kimapato ni hafifu tusijidanganye, ziko wapi fedha za kumudu gharama za uendeshaji kama zipo ni kipi kinachozuia tusilipe mishahara minono kwa vikosi vyetu na kuwapatia maisha bora, mfumo wa Serikali tatu una viashiria vya kutaka kuvunja muungano,” alisema Nahodha akishangiliwa na wananchi waliokuwepo mkutanoni.
Alisema wakati huu wa mjadala wa uundwaji wa Katiba Mpya ni wakati mwafaka wa kushughulikiwa kwa maeneo yenye kasoro za kimsingi na siyo kufikiria kubadilisha mfumo wa Muungano kama inavyohitajiwa na baadhi ya wanasiasa kwa utashi na matakwa binafsi.
“Ndugu zangu, kama leo hii tukivunja Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wazanzibari tujue tutajuta na kusaga meno, nasema wenye wazo hilo ni wapuuzi ila msiwapuuze,” alisema.
Alisema Muungano umeleta faida kubwa kwa pande mbili na kutoa mfano wa Wazanzibari kuweza kulitumia soko la kiuchumi la Bara lenye watu zaidi ya milioni 44, kupata huduma za matibabu katika hospitali za Tanzania Bara, ulinzi na usalama na mambo mengine ambayo Zanzibar hakuna.
source: mwananchi

No comments:

Post a Comment