WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, December 9, 2013

Tumejifunza nini kutoka kwa NELSON Mandela?



GREAT MAN OF ALL TIMES;

Dunia nzima imeshitushwa na kifo cha shujaa wa Africa Raisi wa kwanza Mweusi na mpiganiaji haki wa Afrika kusini na dunia kwa ujumla hayati Nelson Mandela;

Swali la kujiuliza kwa nini kifo chake kimevuta hisia za mataifa yote duniani?

Kwa ufupi Nelson Rolihlahla Mandela alizaliwa tarehe 18 Julai,mwaka 1918. Ni Rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia Nchini Afrika Kusini. Alikuwa Mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa za ubaguzi katika Afrika ya Kusini.


Mandela alianzisha kampeini ya kuhujumu serikali. Hatimaye alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kuwa na njama ya kuipindua serikali. Kutokana na kosa hilo Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka 27, alifungwa katika kisiwa cha Robben; jela lenye ulinzi mkali mjini Cape, Table Bay
Mwaka 1990, .W. de Klerk, alitangaza kuondoa marufuku dhidi ya chama tawala ANC hatua ambayo iliwezesha Mandela, hatimaye alichiliwa huru.
 
Kufuatia kuachiwa huru mwaka 1994 chama na ANC kilipata fursa ya kushiriki uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia, na ambao uliwahusisha wazungu na waafrika,na hatimaye chama cha ANC kilishinda uchaguzi huo na Nelson Mandela kuapishwa kuwa Raisi wa kwanza Mweusi kuongoza Afrika ya kusini.

FIKRA TIMILIFU:

Tunafahamu kuwa Mandela alilikuwa kiongozi mpinanaji ambaye hakupenda siasa za ubaguzi wa rangi ambazo zilikuwa zikiendeshwa na makaburi waliotawala Africa kusini pamoja na washirika wake; kwa maneno mengine Mandela alikuwa kiongozi mwenye si tu hekima  bali pia aliweza kuongozi kwa kuzingatia uadilifu.

Tunachojifunza sasa ni kuwa viongozi wengi ambao walikuwa waadilifu kama Mandela ndio wamekufa, na wengine wanaendelea kufa; hata waliobaki, tuliokuwa tunawategemea, wameanza kutukatisha tamaa.

UONGOZI WENYE TIJA

Mandela aliongoza Taifa lake kwa kipindi kimoja tu; na aliacha madaraka kwa furaha na upendo  mkubwa na kuwapisha wengine nao waongoze; baada ya kukaa gerezani kwa miaka 27 hakuwa na uchu wa madaraka baada ya kuwaunganisha wanasouth Afrika pamoja na kuondoa zana ya ubaguzi kati ya makaburu na wananchi wazalendo wa Afrika kusini; ni kiongozi wa ajabu ambaye alipigania usawa na umoja bila kujali rangi na dini;

2004

Thabo Mbeki alichukua mamlaka kutoka kwa Mandela kama kiongozi wa chama tawala ANC na hata kushinda uchaguzi wa mwaka 1999.Mandela alimuoa Graca Machel, mjane wa aliyekuwa rais wa Msumbiji, akiwa na miaka 80. Aligunduliwa kuwa na saratani ya Tezi Kibofu na hivyo kuanza matibabu.Mnamo mwaka 2004, alitangaza kujiuzulu, akisema kuwa anataka maisha ya kimya nyumbani kwake na familia yake. Kwa mzaha aliwaambia wandishi wa habari wasimpigie simu.
 
Mandela baada ya kutoka gerezani na wakti huu akiwa raisi wa Afrika ya kusini aliweza kuendesha mijadala, mikubwa ya kisomi yenye kutafakari ya njia sahihi  ya kuleta umoja wa wana afrika kusini na hivyo kuyaonyesha mataifa makubwa kuwa hata Africa tunajua nini maana ya demokrasia na kuvumiliana na si tabia ya  kulipiza kisasi.

Mandela ndiye aliyekuwa na nguvu za kiutawala tangu lakini alitoa fursa kwa wengine pia nao waweze kuonyesha uwezo wao na vipaji vyao katika kuongoza, hakuwa mbinafsi alikuwa ni kisima cha hekima ambacho alitamani wengine ambao wanataka kuchota maarifa wafaidike.

Historia inatuambia kwamba viongozi wengi waliofanikiwa ni wale ambao walikuwa na wafuasi wa kweli, wafuasi ambao walikuwa tayari hata kupoteza maisha yao ili kulinda na kutetea itikadi na harakati zilizoanzishwa na viongozi wao. Na hapa sizungumzii madikteta waliolazimisha itikadi zao kwa wafuasi wao kwa mkono wa chuma na kumwaga damu.
Mandela atakumbukwa sana kwa kuweka maslahi ya taifa  lake mbele. Pamoja na Hatati Mwalimu Nyerere, Nkwame Nkuruma Moses Macheli ni viongozi ambao kwa pamoja walisimamia na kutetea sana haki za wana Afrika. Hakutetea hata siku moja siasa za  ubeberu, walizipinga kwa nguvu zote na kwa gharama yeyote ile.

 “Kama kuna kitu  cha muhimu alichokifanya  Mandela basi ni kuhimiza wanaafrika kusini wawe kitu kimoja na kuutokomeza ugaguzi.

Hebu tujikumbushe matukio makuu ambayo Marehemu Nelson Mandela amepitia:

Februari 11, 1990
BAADA ya miaka 27 jela, Nelson Mandela, hatimaye aachiwa na serikali ya makaburu wa Afrika ya Kusini iliyokuwa ikiongozwa na Rais Fredrick Willem de Klerk.

Tukio hilo ni miongoni mwa matukio makubwa katika historia ya Afrika Kusini maana lilimaanisha kwamba makaburu wameanza kutambua kwamba hawawezi kushindana na nguvu ya umma.

Julai 5, 1991

Chama cha African National Congress (ANC) chamchagua kuwa Rais wa Afrika Kusini. Mandela alipewa nafasi hiyo akichukua nafasi ya swahiba wake wa kisiasa, Oliver Tambo, aliyefariki dunia.
Wadhifa huo ndio uliomwezesha kuchaguliwa na chama chake kuwania urais wa Afrika Kusini baadaye.

Aprili, 1992

Atangaza kuachana na aliyekuwa mkewe, Nomzamo Winnie Madkizela Mandela, baada ya uhusiano wao wa zaidi ya miaka 30 uliotawaliwa na misukosuko mingi.
Inadaiwa Mandela alimuacha Winnie kutokana na mwanamama huyo kudaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na vijana wadogo mbalimbali ndani ya ANC aliokuwa akifanya nao kazi.

Oktoba 15, 1993

Atunukiwa tuzo ya Nobel kwa pamoja na De Klerk kutokana na mchango mkubwa katika kuleta upatanishi na maelewano nchini Afrika Kusini.

Mei 10, 1994
Achaguliwa kwa kura nyingi kuwa Rais wa Kwanza Mweusi katika Uchaguzi wa Kwanza wa Kidemokrasia nchini Afrika Mashariki. Urais wake unaashiria kumalizika rasmi kwa zama za ubaguzi wa rangi nchini humo.

Julai 18, 1998

Akiwa ziarani nchini Canada, ofisi yake yatangaza kwamba anamuoa Graca Machel, mke wa rais wa zamani wa Msumbiji, Samora Machel.
Ndoa hiyo inaelezwa kumaliza upweke aliokuwa nao Mandela kutokana na uamuzi wake wa kumuacha Winnie miaka saba nyuma.

Mwaka 1999

Baada ya miaka mitano ya urais, Mandela alitangaza kutowania nafasi hiyo katika uchaguzi unaofuata na badala yake akamuachia makamu wake, Thabo Mvyelwa Mbeki, kuwania nafasi hiyo.
Mandela aliachia ngazi wakati bado akipendwa na wananchi wake. Hatua yake ya kuachia ngazi ilikwenda kinyume na viongozi wengi wa Afrika ambao hupendelea kung’ang’ania madaraka.

Mwaka 2000

Achaguliwa kuwa msuluhishi wa mgogoro wa Burundi akichukua nafasi ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliyefariki dunia mwaka mmoja nyuma.

Kazi hiyo aliifanya hadi alipoanza kudhoofu kiafya na akamwachia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye sasa ndiye rais wa nchi hiyo.

Mwaka 2001
Baada ya vipimo vya kitabibu, Mandela alibainika kuwa na ugonjwa wa kansa ya tezi ya kiume ya uzazi (prostate cancer).
Taifa la Afrika Kusini lilipatwa na mshtuko mkubwa kutokana na na habari hizo za kushtusha kumhusu kiongozi wao mpendwa.

Mwaka 2003
Kutokana na hatua ya Marekani na washirika wake kuivamia Irak kwenye vita ya pili ya Ghuba ikidai ina silaha za maangamizi, Mandela azungumza hadharani na kukemea sera za nje za taifa hilo kubwa duniani.

Mwaka 2004
Mandela atangaza kurejea kijijini kwake Qunu na kusema hatakuwa akionekana tena hadharani mara kwa mara. Aomba aachwe apumzike na wajukuu zake.

Aprili 19, 2009
Mandela atoa hotuba ya mwisho ya kisiasa baada ya kuongea kupitia hotuba iliyorekodiwa kwenye mkutano wa hadhara wa ANC wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini.

Kulikuwa na utata kuhusu iwapo Mandela amependezewa na hatua ya ANC kumchagua Jacob Zuma kuwa mgombea wake wa urais badala ya Mbeki.

Kwenye hotuba hiyo, Mandela aliweka hadharani msimamo wake wa kumuunga mkono Zuma na ANC. “Nitakuwa na ANC hadi kufa kwangu,” alisema Mandela.

Januari 26, 2011
Alazwa hospitali kutokana na kile kilichoelezwa kuwa matatizo katika mfumo wake wa kupumua.
Matatizo haya ndiyo yalikuwa kama yamefungulia njia ya yeye kuanza kuumwa mfululizo.

Februari 25, 2012 
Alazwa hospitali kutokana na kusumbuliwa na maumivu makali ya tumbo.

Desemba 8, 2012 hadi  Januari 6, 2013
Anakimbizwa hospitalini na kulazwa kwa takribani mwezi mmoja baada ya kukutwa na mawe kwenye kongosho lake. Huu ndiyo muda mrefu zaidi kwa kiongozi huyo kukaa hospitali tangu apatwe na matatizo ya kiafya.

Machi 28 hadi April 6, 2013
Mandela alazwa tena hospitali kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kichomi (Pneumonia).

Juni 8, 2013
Alazwa hospitali kutokana na matatizo katika mapafu.


DECEMBER 5 2013- Afariki Dunia
Mzee Nelson “Madiba” Mandela amefariki dunia kwa mujibu wa CNN mzee Madiba amefariki dunia tarehe 05/12/2013 akiwa na umri wa miaka 95.Kwa mujibu wa Rais wa rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema mzee Mandela amefariki Ijumaa usiku baada ya kuugua kwa muda mrefu.Anatarajiwa kuzikwa tarehe 15/12/2013.

MWENYEZI MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI: SISI TULIMPENDA SANA SHUJAA WETU LAKINI MWENYEZI MUNGU AMEMPENDA ZAIDI; AMEN
NELSON MANDELA INSPIRATIONAL QUATATIONS

"I was made, by the law, a criminal, not because of what I had done, but because of what I stood for, because of what I thought, because of my conscience.” Mandela, 1962.

“Social equality is the only basis of human happiness.”  Mandela, 1970

"Great anger and violence can never build a nation. We are striving to proceed in a manner and towards a result, which will ensure that all our people, both black and white, emerge as victors” - Mandela 1990.

“When a man has done what he considers to be his duty to his people and his country, he can rest in peace” - Mandela, 1994.

"Reconciliation means working together to correct the legacy of past injustice.” -  Mandela 1995.

"If you want to make peace with your enemy, you have to work with your enemy. Then he becomes your partner." - Mandela 1995.

"I like friends who have independent minds because they tend to make you see problems from all angles." - Mandela

"I hate race discrimination most intensely and in all its manifestations. I have fought it all during my life; I fight it now, and will do so until the end of my days." - Mandela

“A leader. . .is like a shepherd. He stays behind the flock, letting the most nimble go out ahead, whereupon the others follow, not realizing that all along they are being directed from behind.” —Long Walk to Freedom: The Autobiography of Nelson Mandela

“No one is born hating another person because of the color of his skin, or his background, or his religion. People must learn to hate, and if they can learn to hate, they can be taught to love, for love comes more naturally to the human heart than its opposite.” —Long Walk to Freedom: The Autobiography of Nelson Mandela

“I have walked that long road to freedom. I have tried not to falter; I have made missteps along the way. But I have discovered the secret that after climbing a great hill, one only finds that there are many more hills to climb. I have taken a moment” - Mandela
“The greatest glory in living lies not in ever falling, but in rising every time we fall.” - Mandela

“Difficulties break some men but make others. No axe is sharp enough to cut the soul of a sinner who keeps on trying, one armed with the hope that he will rise even in the end.” —From a letter to Winnie Mandela, 1975

Today we are entering a new era for our country and its people. Today we celebrate not the victory of a party, but a victory for all the people of South Africa… The task at hand on will not be easy. But you have mandated us to change South Africa from a country in which the majority lived with little hope, to one in which they can live and work with dignity, with a sense of self-esteem and confidence in the future. –mandela- Inaugural speech, May 9, 1994

No one truly knows a nation until one has been inside its jails. A nation should not be judged by how it treats its highest citizens but its lowest ones. –Mandela Long Walk to Freedom

I have walked that long road to freedom. I have tried not to falter; I have made missteps along the way. But I have discovered the secret that after climbing a great hill, one only finds that there are many more hills to climb. I have taken a moment here to rest, to steal a view of the glorious vista that surrounds me, to look back on the distance I have come. But I can rest only for a moment, for with freedom comes responsibilities, and I dare not linger, for my long walk is not yet ended. –Mandela Long Walk to Freedom

RIP NELSNON  MANDELA THE GREAT MAN OF ALL TIMES

No comments:

Post a Comment