WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, October 25, 2013

Shujaa wa Tanzania,Mwl.Nyerere

184495_288229154613280_419551865_n_df9ee.png
Shujaa wa Tanzania, Afrika na Dunia,anatembea kwa miguu si kwa kukosa usafiri wa gari au hercopter anajua anataka kufanya anachojua hasubiri ripoti,hajavaa suti wala sare ya chama cha mapinduzi kwa kuwa si mtumwa wa chama au tangazo la chama ni mtumwa wa watanzania na tangazo la watanzania,kavaa gwanda anajua yuko katika mapambano,ameshika fimbo mkononi kwajili ya kuchunga,kuongoza kondoo wake ambao anajua wana kiu na njaa lakini pia kuchapa wenye viburi,warafi,wakorofi,wanyonyaji na wengine wenye tabia kama hizo.(P.T)

''Mwalimu Julias Kambarage Nyerere,Baba wa Taifa wa kwanza katika Taifa hili,ulijitolea kwa moyo wako wote kwajili yetu,ulipigania usawa,uhuru na haki,kuimalisha ujamaa na upendo miongoni mwetu,ulipigana na ujinga,maradhi na umaskini na ulimanisha kwa vitendo,leo haupo kimwili lakini bado unaishi katika vichwa na mioyo yetu,binafsi sijawahi kukusahau na kamwe abadani asilani sitakusahau''

HEADER

Guest
0Guest2013-10-25 10:29#1
Amen! huyu mzee nadhani alishushwa na mungu ili aje kutukomboa.laki ni sasa tumebakiwa na viongozi warafi,wanaopen da kujinufaisha nafsi zO.

Hakuna mwenye nia thabiti ya kutetea wanyonge. Tanzania inahitaji kiongozi anaeweza kuthubutu kumwambia mtu akufukuza kazi leo, lakini wapi kila mtu anaangalia vx yake ina mafuta baada ya kustaafu atakua na nini mwisho.inauma saaana

Mungu ibariki Tanzania
Mnukuu
Guest
0Guest2013-10-25 11:41#2
Mungu huwainua viongozi kama Nyerere kwa nadra. Yawezekana vikapita vizazi vingi sana hadi kumpata kiongozi mwingine kama Nyerere. Katika kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere 14/10/2013 TBC TV hawakuandaa 'documentary' nzuri kuhusu Mwalimu aliyeandaa ni kama hakujipa umakini wowote. Si TBC TV bali vituo vyote vya TV kama ITV, STAR TV, EAT TV n.k. havikujishughul isha kuandaa 'makala' zenye mashiko kuhusu Mwalimu. wangefanya BBC au DW hata kama ni kuwa 'biased' bado wangetoa makala nzito. Picha hiyo hapo juu inasema mengi kuliko makala ya TBC siku hiyo.
Mnukuu
Guest
0Guest2013-10-25 18:06#3
Tulioteseka na hayo mashamba ya ujamaa bila kunufaika na mazao yake hamtuuzii hizo story ng'o! Unamuona yule Jombi wa kushoto kabisa, shati lake lilivyojaa viraka? Unayajua makatambuga weye?
 
source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment