WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, October 2, 2013

Papa John Paul kutangazwa mtakatifu Aprili mwakani

zzzzzzzzzzzzpope_25f2f.jpg

Papa John Paul II na John XXIII wanatarajiwa kutangazwa watakatifu Aprili 27 mwakani, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkuu wa sasa wa kanisa Katoliki, Papa Francis.

Taarifa ya uamuzi huo imetolewa leo kwenye mkutano wa makadinali unaoendelea mjini Vatican, ikiwa ni hatua mihimu ya kuthibitisha tangazo lake la Julai mwaka huu kwamba atawapa heshima viongozi hao wawili wa juu wa Kanisa waliopita katika karne ya 20.

Katika taarifa iliyonakiliwa kutoka kwenye gazeti la mtandaoni la Daily Mail, alisema wakuu hao wa Kanisa Katoliki duniani ambao kwa sasa ni marehemu waliweza kutumia karama zao kwa uamunifu na kuonyesha matendo makuu.

Wachambuzi wa masuala ya Kanisa hilo alieleza kwamba inaonekana umuzi huo ni wa makusudi ikiwa ni hatua ya kujaribu kuliunganisha kanisa hilo ambalo lina mkanganyiko kwa sasa.

Kila mmoja ana watu wanaomuunga mkono na wanaompinga, ambapo kwa sasa Francis anaonekana kuungwa mkono na wote wa pande zote mbili hivyo kuwa kichocheo cha kuunganisha na kufuta makovu yaliyolikumba Kanisa hilo kwa miaka ya hivi karibuni.

source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment