WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, October 28, 2013

Balozi Isaac Sepetu afariki dunia

Mke wa marehemu Balozi Sepetu,Mariamu Sepetu
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Balozi Isaac Sepetu, amefariki dunia jana alfajiri jijini Dar es Salaam.
Alikutwa na mauti hayo katika hospitali ya TMJ alipokuwa akipatiwa matibabu.

Akizungumza na NIPASHE jana nyumbani kwa marehemu Mwenge, jijini Dar es Salaam, mke wa marehemu Balozi Sepetu, Mariamu Sepetu, alisema mumewe alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na kiharusi.

Alisema Agosti 21, mwaka huu, marehemu alipatwa na ugonjwa wa kiharusi na kulazwa katika hospitali tiba Mbadala, Zanzibar.

“Baada ya kupokea taarifa kwamba amepata ‘stroke’ nilikwenda Zanzibar kumuangalia na nilivyoona hali yake hairidhishi, nikawasiliana na watoto, tukakodi ‘charter’ (ndege) na kumleta hapa kwa matibabu zaidi,” alisema.

Alisema baada ya kupatiwa matibabu na kufanyiwa ya mazoezi ya viungo, na hali yake ilionekana kuimarika.

Jaji Mkusa Sepetu akizungumza na NIPASHE kwa niaba ya watoto wa marehemu, alisema mipango ya mazishi inafanyika, huku wakiwasubiri watoto wengine wa marehemu waliopo nje ya nchi ili tukubaliane, lakini marehemu atazikwa Unguja Mbuzini, Zanzibar.

Naye Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mkumbwa Ally, alisema serikali inasubiri kupewa taarifa za taratibu za mipango ya mazishi kutoka kwa ndugu wa marehemu.

Balozi Sepetu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje miaka ya 1970 katika serikali ya awamu ya kwanza.

Kadhalika aliwahi kuwa balozi wa Tanzania nchini Urusi tangu mwaka 1982 na hadi anafariki alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA).

Marehemu ameacha wajane wawili Angelika Sepetu na Mariamu Sepetu pamoja na watoto tisa.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment