WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, November 21, 2013

Yanga yatikisa nchi nzima

yanga_a573c.jpg

WATAALAMU wa hesabu wana usemi wao wanaoupenda 'Namba haziongopi'. Ukirudisha usemi huo kwenye tathimini ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, lugha nyepesi unayoweza kusema ni kwamba 'hakuna kama Yanga'.

Sahau kwamba imemaliza ikiwa kileleni na pointi zake 27. Takwimu za Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL), zimethibitisha kwamba Yanga imeongoza takwimu zote kuanzia mapato mpaka idadi ya mashabiki walioingia uwanjani.

Takwimu zilitolewa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPL, Silas Mwakibinga, ni kuwa Yanga imekusanya kiasi cha Sh334.2 milioni katika mechi 13 za mzunguko huo. Katika takwimu hizo, Simba SC ni ya pili kwa kupata Sh304 milioni huku timu iliyopanda daraja msimu huu, Mbeya City, ikiipiku Azam FC kwa kushika nafasi ya tatu kwa kujikusanyia Sh83.8 milioni. Azam imekusanya Sh67.1 milioni.(P.T)
Nyingine na fedha zilizokusanya katika mabano ni Coastal Union (Sh65. 7 milioni), Mtibwa Sugar (Sh49.9 milioni), Ruvu Shooting (Sh46.1 milioni), Tanzania Prisons (Sh38.1milioni), JKT Ruvu (Sh36.1 milioni), Ashanti United (Sh35.7 milioni), Rhino Rangers (Sh31.1milioni), Mgambo JKT (Sh25.8 milioni), Oljoro JKT (Sh20.8 milioni) na Kagera Sugar (Sh18.5 milioni).

"Huu ni mwanzo tu wa kusimamia ligi na mpaka sasa hatujafikia lengo letu, tunataka kuona kila timu inakuwa na uwiano sawa wa makusanyo na kama kuzidiana, basi iwe kiasi kidogo, tumefurahishwa na mwenendo wa Mbeya City ambao wamefanya mambo makubwa japo wapo katika msimu wa kwanza," alisema Mwakibinga.

Kwa upande wa mashabiki walioingia viwanjani, Yanga pia imekuwa kinara kwa kuingiza mashabiki wengi katika mechi. Jumla ya mashabiki 107,890 wa timu hiyo wameingia katika mechi na kufuatiwa na Simba ambao wameingiza mashabiki 97,364 mpaka mwisho wa mzunguko huo.

Timu ya Mbeya City imezidi kung'ang'ania nafasi ya tatu na kuendelea kuitambia Azam FC kwa kuingiza mashabiki 43,439 tofauti na Azam ambao mpaka sasa wameingiza mashabiki 30,236.
Nyingine ni Coastal Union (mashabiki 27,880), Mtibwa Sugar (20,794), Rhino Rangers (20,263), Prisons (19,923), Ruvu Shooting (19,000), JKT Ruvu (16,095), Ashanti United (16,093), Mgambo (11,726) na JKT Oljoro (10,430).

Kwa mujibu wa Mwakibinga, jumla ya Sh 2.4 bilioni zimekusanywa katika mzunguko huo wa kwanza. Kiasi hicho ni ongezeko la Sh599. 5 milioni katika mzunguko wa kwanza wa msimu uliopita.
"Hii ni historia na hasa ukizingatia kuwa baadhi ya mechi zimekuwa zikionyeshwa 'laivu' katika televisheni na baadhi ya mashabiki kuangalia kupitia luninga zao, lakini bado tumezidi kupata makusanyo makubwa," aliongeza Mwakibinga.

"Haya ni matokeo mazuri ya kuzinadi mechi za ligi na mfano mzuri mechi ya Yanga na Mbeya City ambayo iliweka historia kwa kuingiza Sh100 milioni na huku tiketi zikiwa zimemalizika kufikia saa 5:00 asubuhi ya siku ya mchezo."

Kwa upande wa viwanja, Uwanja wa Taifa unaongoza kwa kukusanya fedha nyingi mpaka sasa ambapo kiasi cha Sh1.8 bilioni kimepatikana hapo, kiwango hicho ni sawa na asilimia 75 ya mapato yote ya mzunguko wa kwanza.
Uwanja wa Sokoine wa Mbeya umeshika nafasi ya pili kwa kukusanya Sh260.5 milioni na kufuatiwa na Mkwakwani wa Tanga Sh105.264 milioni.

Viwanja vingine na mapato yake ni Ali Hassan Mwinyi wa Tabora (Sh100.2 milioni), Sheikh Amri Abeid wa Arusha (Sh57.4 milioni), Azam Complex wa Dar es Salaam (Sh32.1 milioni), Kaitaba wa Bukoba (Sh26.1 milioni), Manungu wa Turiani, Morogoro (Sh9.4 milioni) na Mabatini wa Mlandizi, Pwani (Sh3.584 milioni).

Chanzo:Mwanasport mtandaoni

No comments:

Post a Comment