WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, August 31, 2013

Museveni aombwa kumaliza mgogoro Rwanda, Tanzania


 Rais wa Uganda, Yoweri Museveni 

Dodoma. Mgogoro wa kidiplomasia ulioibuka kati ya Rwanda na Tanzania, jana ulitinga bungeni huku Rais Jakaya Kikwete, akimuomba Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuwa msuluhishi wa mgogoro huo.

Hata hivyo, Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alionyesha kutoafiki kuombwa kwa Rais Museveni akisema naye yuko katika kundi linaloitenga Tanzania.

Kauli ya kwamba Tanzania kupitia kwa Rais Kikwete imemuomba Rais Museveni kuwa msuluhishi wa mgogoro huo,ilitolewa jana bungeni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Waziri Mkuu alikuwa akijibu swali la papo kwa hapo aliloulizwa na Mbowe akitaka kupata kauli ya Serikali juu ya kuibuka kwa mgogoro huo wa kidiplomasia na dalili za Tanzania kutengwa.

Katika swali lake la msingi, Mbowe alisema mvutano huo wa kidiplomasia umesababisha Tanzania kutengwa katika shughuli ambazo zilipaswa kuwa za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu alikiri kuwapo kwa hali ya  kutoelewana na kwamba hata baada ya kauli ya Rais Kikwete kuwa Tanzania haina uhasama na Rwanda, mvutano unaendelea.

“Mimi ninavyojua Rais (Kikwete) amemuomba Rais wa Uganda Yoweri Museveni ajaribu kuona ni namna gani jambo hili linaweza kusuluhishwa na maneno haya yakapungua,” alisema Pinda.

Waziri Mkuu alisema anaamini busara zitatumika ili kuona jambo hilo linakwisha vizuri lakini kama litaendelea na kuonekana dalili za Tanzania kutengwa busara zaidi itahitajika. Katika swali la nyongeza, Mbowe alisema kinachoonekana, Rwanda wameweza kuwavuta Waganda na Wakenya katika mikakati ya kiuchumi ambao kwa hali ya kawaida ingekuwa ni ya jumuiya

Alisema viongozi wa mataifa hayo wamekutana Kampala na Kenya bila kuwapo kwa Tanzania

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment