WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, August 24, 2013

Kikwete azindua baraza la ‘vigogo’


 


Dodoma. Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete jana alizindua Baraza la Ushauri linalounda na wenyeviti na makamu wenyeviti wastaafu na baadaye baraza hilo likamchagua Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwa mwenyekiti wake wa kwanza huku katibu wake akiwa Pius Msekwa.

Katika hafla ya uzinduzi wa baraza hilo, iliyohudhuriwa na wazee hao isipokuwa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk Salmin Amour kwa sababu za kiafya, Rais Kikwete aliwamwagia sifa marais wastaafu, Mwinyi na Benjamin Mkapa kuwa ni sawa na kamusi ya mageuzi makubwa yaliyotokea nchini nyakati uongozi wao.

Kuhusu Mwinyi, Kikwete alisema ni mwasisi wa mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi kwa kuwa aliwezesha taifa kuondoka katika uchumi wa dola kuingia uchumi soko, huku Mkapa akipokea mabadiliko hayo na kuyaendeleza katika mfumo wa vyama vingi.

Baada ya uzinduzi huo, wazee hao walikaa kwenye kikao chao cha kwanza kujadili “mambo ambayo wangeona yanafaa”, ambako waliwachagua Mwinyi na Msekwa kuwaongoza.

Waliohudhuria uzinduzi huo ni Mkapa, Mwinyi, Msekwa, John Malecela na Amani Abeid Karume.

Baraza hilo tayari linatambuliwa ndani ya Katiba ya CCM, lilitokana na mapendekeo ya Kamati ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama iliyoundwa mwaka 2011.

kwa lengo la kushauri namna ya kufanya mageuzi mbalimbali ndani ya chama.

Rais Kikwete alisema wao ndani ya chama , hawana hofu ya kuwatumia wazee hao kwa njia hiyo kwa kuwa itakuwa njia mwafaka ya kutoa ushuri wao kwa namna watakavyoona inafaa.

Alipuuza madai kwamba wazee hao wanaondolewa kwenye vikao vya uamuzi, akisema mbali na mapendekezo ya Kamati ya Mukama, pia wazee hao walikuwa wanachoka kuitwa mara kwa mara kwenye vikao.

“Tumekuwa tukiwaita kwenye vikao vyetu na wao wanahoji, ’kwanini mnatusumbua nyinyi hamuwezi kuamua wenyewe, wanasema kama kuna jambo la muhimu sana…wanasema ‘sisi tumeshatimiza wajibu wetu na nyingi timizeni wajibu wenu,” alisema.

Alisema hata kwenye vikao, wastaafu hao walikuwa wanaona taabu kuzungumza kwa kuhisi kuwa wangeweza kuonekana wanamwingilia mwenyekiti, jambo ambalo halitakuwapo wakiwa peke yao, kwa kuwa watakaa na kuamua nini cha kushauri na namna ya kushauri.

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment