WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, August 28, 2013

Kumbe! Jeuri , kiburi cha Kagame vinatoka kwa wakubwa!


kagame_48210.jpg

Aliyekuwa Rais wa Marekani Bill Clinton, hivi majuzi amemtetea Kagame kutokana na tuhuma zinazomkabili za kuwasaidia waasi wa M23 nchini DRC.

Kwa muda wa miezi takriban minne kumekuwa na maneno ya kejeli kutoka kwa Serikali ya Rwanda na kwa hakika maneno hayo yanatoka mdomoni mwa Rais Paul Kagame na maofisa wa ngazi za juu katika Serikali yake

Kagame amekuwa mbogo baada ya Rais Jakaya Kikwete kumshauri afanye mazungumzo na wapiganaji wa Kihutu waliokimbilia Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) baada ya kutuhumiwa kufanya mauaji ya kimbari nchini mwake mwaka 1994.

Inakadiriwa kuwa Watutsi na Wahutu 800,000 wenye msimamo wa wastani waliuawa wakati huo, ingawa takwimu hizo zina utata, kwani wako wanaodai kuwa nchi hiyo wakati huo ilikuwa na idadi ndogo ya watu ambao idadi hiyo inasemekana ndio waliouawa.

Pia, wapo wale ambao wanaweza kushangaa kwa nini Kagame amekuwa hivyo na kuikosea heshima Tanzania, nchi ambayo imekuwa mstari wa mbele kupokea wakimbizi wake toka miaka ya 1960 na kwa nini Rais Kikwete alitoa ushauri huo.

Kagame hakupendezwa na ukweli huo kwani kila mara amekuwa akikataa kuwa hana mkono katika mapigano yanayoendeshwa na vikundi vya msituni vinavyoanzishwa nchini DRC kila inapotokea hali kutulia.

Kikwete amekuwa akijua jambo hili kwa muda mrefu kwani amekuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa kipindi cha miaka kumi na amekuwa akihudhuria mikutano ya kutafuta amani ya DRC bila mafanikio kwa sababu kila kikundi kinapoingizwa katika jeshi la DRC na kudai kuwa kimemaliza vita kinazuka kikundi kingine ambacho nacho kinaanzisha mapambano dhidi ya serikali.

Kofi Annan, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa (UN) alikuwa mkuu wa shughuli za kijeshi za umoja huo kabla hajapanda cheo na kuwa katibu mkuu wa umoja huo, alipotembelea Rwanda baada ya kumalizika kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe, msafara wake ulirushiwa nyanya.

Hiyo ilikuwa ni kama kumpa ujumbe kuwa hakuna alichofanya wakati ule Watutsi walipouawa na Wahutu mwaka 1994.

Masikini! Annan angefanya nini wakati alipokuwa akiyaomba mataifa makubwa kuingilia kati ili kusitisha mauaji kila moja lilikuwa likiangalia maslahi yake na ulikuwepo mpango wa uchelewashaji wa makusudi.

Baadaye Annan alipokuwa akigombea Ukatibu Mkuu wa UN ni Rwanda pekee katika nchi za Afrika ndiyo iliyopinga na hata alipokuwa akiomba kuongezewa muda ni nchi hiyo iliyokuwa kinara wa kumpinga wakati ukweli ni kuwa mambo yote yaliyokuwa yakifanyika wakati huo Kagame alikuwa akiyajua.

Aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Rwanda, Meja Jenerali Kayumba Nyamwasa, alinukuliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) akiwa uhamishoni Afrika Kusini akithibitisha kuwa vikundi vyote vimekuwa vikianzishwa na Kagame kwa nia ya kuhakikisha kuwa Wahutu na jeshi la zamani la nchi hiyo ambalo kwa sehemu kubwa linaundwa na waliokuwa vijana wa Inteharamwe hawapati muda wa kujijenga.

Kwa maneno mengine, Kagame ameifanya ardhi ya DRC kama uwanja wa mapambano kati yake na wapinzani wake ambao wako mashariki mwa nchi hiyo.

Jenerali Nyamwasa, ambaye kabla ya kukimbilia Afrika Kusini alikuwa Balozi wa Rwanda nchini India anasema kuwa Kagame ndiye aliyeamrisha kutunguliwa kwa ndege iliyokuwa imebeba ujumbe wa nchi hiyo pamoja na Rais Juvenal Habyarimana na Cyprian Ntyaramira wa Burundi ambao ulikuwa umetokea Tanzania kwenye mkutano wa kujadili amani ya nchi hiyo.

Baada ya vita kumalizika na hatimaye RPF kuchukua uongozi, Ufaransa, mtawala wa zamani wa Rwanda ilimtuhumu Kagame kwa kusababisha mauaji ya kimbari kwani Wahutu wasingianzisha chinja chinja ya Watutsi kwa wakati huo kwani mazungumzo yale yalikuwa yanaelekea ukingoni na hatua ya mwisho ingekuwa kwa RPF kuwa chama cha kisiasa ambacho kingeshiriki kwenye uchaguzi.

Nia ya Kagame ilikuwa ni kuchukua uongozi Rwanda kwa nguvu kwa sababu kwa mizania ya siasa za nchi hiyo ambazo zimejikita zaidi kwenye ukabila ingekuwa vigumu kwa Watutsi walio wachache kushinda.

Sababu ya pili ambayo ndiyo iliyowafanya RPF wakatae au watumie nguvu ilikuwa ni juhudi ya Marekani ambayo ilikuwa mfadhili mkuu wa RPF kuhakikisha kuwa ushawishi wa Ufaransa katika eneo la Maziwa Makuu unaondoshwa kwa gharama yoyote.
Hii inathibitishwa katika kitabu Global Intelligence; the world's secret services today ambacho kimeandikwa na waliberali, Paul Todd na Jonathan Bloch.

Waandishi hao wanabainisha kuwa wakati huo kulikuwa na vita vya kijasusi baina ya Marekakani na Ufaransa ambavyo baadaye vilibadilika na kuwa ni vita vya kijeshi.

Kagame alikuwa Mkuu wa Idara ya Usalama wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda kabla ya kujiunga na RPF.
Ufaransa ikimsaidia Habyrimana na Marekani ikiwasaidia RPF ambao tayari walikuwa wakisaidiwa na Uganda walijipatia taarifa za kijasusi kutoka kwa Serikali ya Rwanda na wapiganaji wake.

Majasusi wa Marekani ambao walikuwa wakitumia njia za kijasusi za siri za kunasa taarifa za mawasiliano katika eneo la Afrika Mashariki walifanikisha mipango ya RPF katika uwanja wa mapambano.

Marekani ilikiri kuwa kuanzia 1994 ilikuwa ikiwasaidia RPF kwa kuwapatia silaha na Kagame alipewa simu ya satelaiti aina ya Motorola INMARSAT ambayo licha ya kufungwa kitaalam (encryption) ili mawasiliano yake yasinaswe na wapiganaji wa Serikali ya Rwanda au yeyote yule, kwa bahati mbaya shirika la Ujasusi la Kimataifa la Ufaransa, DGSE (Direction Generale de la Securite Exteriure) lilifanikiwa kunasa mawasiliano yale na Ufaransa iliituhumu Marekani kwa kutoa kombora lililoiangusha ndege iliyokuwa imembeba Rais Habyarimana.

Kwa maana nyingine, ni kuwa Kagame hawezi kukwepa mkono wa sheria wakati utakapofika kwani taarifa muhimu za namna mambo yalivyokuwa yakienda katika uwanja wa mapambano, mawasiliano yake yamehifadhiwa na taasisi hiyo ya kijasusi ya Ufaransa.

Waandishi hao wamebainisha kuwa kwa kuwa Rais Mobutu Seseseko wa Zaire (sasa DRC) alikuwa akimsaidia Jonas Savimbi ambaye Wamarekani walikuwa wameishamchoka na walimtaka aache vita ili utulivu urejee Angola, nao wavune madini na mafuta huko wakiwa na sababu ya kumwondoa Mobutu madarakani ili kukata mizizi ya usaidizi aliokuwa akiupata Savimbi, ambaye wakati huo alikuwa kiongozi wa UNITA, iliyokuwa ikipigana vita vya msituni dhidi ya Serikali ya Angola chini ya MPLA.

Sababu nyingine ilikuwa kwa Mobutu kuwasaidia Wahutu ambao walikuwa kipenzi cha Ufaransa ilibidi aondolewe ili kuhakikisha kuwa Wamarekani wanalishika na kulidhibiti eneo lote la Maziwa Makuu.

Ikumbukwe kuwa wakati huo Rais Bill Clinton ambaye hivi majuzi amemtetea Kagame kutokana na tuhuma zinazomkabili za kuwasaidia waasi wa M23 nchini DRC, ndiye aliyekuwamadarakani wakati huo na alifanya juhudi kubwa kuhakikisha kuwa shughuli za kijasusi zinaendeshwa katika mtindo ambao utakuwa na manufaa zaidi kiuchumi na siyo kisiasa kama ilivyokuwa wakati wa vita baridi.

DRC ilikuwa muhimu kwa majasusi wa Marekani, hasa kwa uzarishaji wa madini ya coltan ambayo hutumika kutengenezea simu za mkononi, madini hayo hayapo sehemu nyingine yoyote duniani zaidi ya DRC.

Clinton alihakikisha kuwa anafanya kila awezalo kuondoa ushawishi wa Ufaransa nchini Sudan kwa kuwataka viongozi wa SPLA wakati huo, Kanali John Garang na wengine wadai uhuru kamili na siyo utawala wa shirikisho kutoka Sudan ili mradi Ufaransa ikose mafuta yaliyokuwa yakichimbwa kutoka Sudan Kusini.

Waandishi hao wamebainisha kuwa Marekani ilitoa dola 100 milioni ili kumsaidia Laurent Kabila kuanzisha jeshi la watoto waliokuwa wakijulikana kama Kadogoo wakiwa na malengo ya kumwondoa Mobutu.

Kufikia mwaka 1997, Shirika la Kijasusi la Marekani (NSA) lilikuwa imejenga vituo vya kuendesha shughuli za kijasusi ili kunasa taarifa za mawasiliano kupitia simu, nukushi, redio katika sehemu mbalimbali za eneo la Maziwa Makuu kama vile, Fort Portal nchini Uganda, Kigali Rwanda na Kongo Brazaville.

Ufaransa ambayo ilikasirishwa na jinsi Marekani ilivyofanikisha kuwaondoa vibaraka wake katika DRC na Rwanda ilihakikisha kuwa inawaandaa wanajeshi ambao walimpindua Rais Pascal Lissouba wa Congo Brazaville ambaye alikuwa ni kipenzi cha Marekani.

Chanzo:Mwananchi

No comments:

Post a Comment