WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, February 14, 2014

OKWI RUKSA YANGA


emosting_37d10.jpg
Mshambuliaji wa kimataifa wa timu ya Taifa Uganda na klabu ya Young Africans Emmanuel Arnold Okwi leo ameruhiswa ramsi kuanza kuitumikia timu yake katika michezo ya Ligi Kuu na Mashindano ya klabu Bingwa Barani Afrika kufuatia shirikisho la soka nchini TFF kuiandikia barua klabu ya Young Africans.
Okwi ambaye alisajiliw aa Young Africans mwishoni mwa mwaka jana na kucheza michezo ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya, alisimamishwa na Shirikisho la Soka la Nchini TFF wakati wakisubiria kupata udhibitisho wa usajili wake kutoka FIFA.

Mara baada ya barua hiyo, Okwi anatarajiwa kuungana na wenzake mwishoni mwa wiki mara timu itakaporejea kutoka Visiwa vya Comoro na ataanza kuonekana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Ruvu Shooting siku ya jumamosi Februari 22 mwaka huu.

Uongozi wa Young Africans unawashukuru wanachama, wapenzi na wadau kwa ujumla kwa kuwa wavumilivu wakati wa suala na hili na hatimaye limepatiwa ufumbuzi.

chanzo: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment