WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, February 24, 2014

Kuhusu Milipuko Ya Mabomu Zanzibar...

Mji wa kitalii wa Zanzibar wa Stone Town ambako raia wawili wa Uingereza wamemwagiwa tindi kali
Ndugu zangu,
Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko habari juu ya matukio ya milipuko ya mabomu mawili ya kutengenezwa nyumbani; moja jirani na kanisa na lingine kwenye mgahawa ambao pia ni maarufu kwa watalii wa kigeni. Hakuna aliyepoteza maisha.
Naungana na ndugu zetu wa Zanzibar kulaani vitendo hivi vya kishenzi na vyenye kutishia uhai wa raia wema na wasio na hatia.
Na hakika, habari hizi hazitoi taswira njema ya Zanzibar na nchi yetu kimataifa. Tayari habari za tukio la mabomu limesharipotiwa kwenye vyombo vya habari kimataifa, http://www.dn.se/nyheter/varlden/bomber-exploderade-pa-zanzibar/,hivyo basi, ni athari mbaya ya moja kwa moja kwa biashara ya utalii ambayo pia ni moja ya mihimili ya uchumi wa Zanzibar.
Ni matumaini yetu, kuwa wahusika na ulipuaji wa mabomu hayo watasakwa popote walipo na kutiwa nguvuni.
Maggid,
Iringa.(P.T)

No comments:

Post a Comment