WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, September 15, 2013

Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City;

kavu_kichwa_a987b.jpg

Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya wenyeji timu ya Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliochezwa jioni ya leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Young Africans wakati wakiingia uwanjani washabiki wa Mbeya City walilirushia mawe na chupa za bia bus la wachezaji hali iliyopelekea kuvunja kioo cha upande wa kulia mwa dereva na kumjeruhi dereva Maulid Kiula aliyekua akiliendesha gari hilo.
Mara baada ya tukio hilo viongozi wa timu ya Yanga walichukua jukumu la kuwatuliza wachezaji na kuendelea kuwapa morali ambapo walituliza munkari wa kujeruhiwa na kuingia ndani kujiandaa na mchezo wenyewe.
Dakika za mwanzo Said Bahanuzi na Didier walishindwa kuzitumia nafasi za wazi na kiujumla hali ya mchezo ilikua sawa kwa timu zote huku washabiki wakikosa radha ya mchezo kutokana na ubovu wa uwanja.
Mbeya City walifanya mashambulizi langoni mwa timu ya Yanga lakini umakini wa walinzi na mlinda mlango Ally Mustapha 'Barthez' ulikuwa kikwazo kwa washambuliaji hao kuziona nyavu za watoto wa Jangwani.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Mbeya City 0 - 0 Young Africans.
Kipindi cha pili kilianza kwa wenyeji kufanya shambulizi langoni wa timu ya Yanga na dakika ya 46 ya mchezo waliweza kujipatia bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji Paul Nonga kwa kichwa aliyeukwamisha mpira wavuni kwa kichwa.
Kocha wa Yanga alifanya mabadiliko ya kuwaingiza Jerson Tegete na Oscar Joshua waliongia kuchukua nafasi za Said Bahanuzi na Nizar Khalfani ambao waliongeza nguvu na kubadili hali ya mchezo.
Dakika ya 60 Didier Kavumbagu aliipiatia Yanga bao la kusawazisha kufuatia golikipa wa Mbeya City kuuchezea mpira na Didier kuukwamisha wavuni lakini katika haliya ajabu mwamuzi alilikataa bao hilo.
Didier Kavumbagu aliipatia Young Africans bao la kusawazisha dakika ya 71 kwa kifua akimalizia mpira uliopigwa na mlinzi Mbuyu Twite na kumkuta mfungaji aliyeukwamisha wavuni bila ajizi.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika Young Africans 1 - 1 Mbeya City
Mara baada ya mchezo wakati timu ikielekea hotelini washabiki wa timu ya Mbeya City wameendelea kuzirushia mawe gari zilizokuwa katika msafara huo ambapo wamevunja vioo vya bus kubwa tena na gari ndogo kioo cha nyuma chote.

source: mjengwa blog

No comments:

Post a Comment