WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, September 23, 2013

Seif: Viongozi watawala wanasababisha vurugu

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Maalim Seif Sharif Hamad
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Maalim Seif Sharif Hamad amesema matatizo mengi ya uvunjifu wa amani na yanayoashiria kuzuka kwa  vurugu yanasababishwa na viongozi watawala katika baadhi ya nchi duniani.
Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Kibaha  kwa niaba yake na Mwenyeki wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Ramadhan Madabida kwenye kongamano la amani lililoandaliwa na Jumuiya ya akina mama waislamu (Juwakita) Mkoa wa Pwani.

Maalim Seif ambaye alikuwa mgeni  katika kongamano hilo,  alisema ikifuatiliwa kwa undani itabainika kuwa  chanzo cha mifarakano hiyo ni dhuluma wanayofanyiwa watawaliwa.

Alisema kwa sasa kuna  viongozi wengi duniani ambao wamekuwa wakiongoza umma kwa utashi wao na kusahau kuwa jukumu hilowalipewa na jamii kwa sababu tu ya kuwaamini.

Madabida ambaye alimlimwakilisha Maalim Seif baada ya kupatwa na msiba wa mtoto wa ndugu yake, alisema katika maeneo mengi ulimwenguni mambo mengi yanayozungumzwa ni uongozi katika nyanja mbalimbali.

Alkisema  watawala wake wanalalamikiwa kuwadhulumu watawaliwa kwa njia tofauti na hivyo kuzusha mifarakano kwa jamii.

"Dhambi kubwa ambayo haisameheki mbinguni hadi uliowakosea wanakusamehi ni hii ya dhuluma, jamani wapo baadhi ya viongozi duniani wamekuwa chanzo cha mifarakano aina mbalimbali kwa sababu tu ya dhuluma zao, si lazima dhuluma hizo ziwe za fedha,mali ama chakula lakini hata ya utoaji taarifa sahihi kwa watawaliwa ama utoaji ufafanuzi wa majambo yanayotokea"alisema madabida

"Jamani ndugu zangu JUWAVITA, kuna mambo yanatokea ya uvunjifu wa amani, yanatokea si kwa sababu watu hawataki bali wamechoka na mtawala wao, hili nalo lazima liangaliwe kiundani katika maeneo mengi duniani, inaweza ikawa ni taarifa tu ya uweli hujawapa unaoowaongoza, na unasahau nyuma yako wapo wenye akili na uadilifu zaidi yako wanajua kila kitu undani wake,,lazima itatokea vurugu, "aliongeza.

Aliwataka viongozi nchini kudumisha amani, wasichezee watekeleze majukumu yao wakijua wazi hivi sasa wanaoongozwa ni wasoni,wenye akili, waadilifu  na pia wenye sifa za uongozi na hivyo wanafatilia kila jambo.

Awali Mkurugenzi wa Taasisi ya Kiislamu ya World Islamic Call Society ya nchini Libya Sheik,Mohamed Qusuri ambaye pamoja na mabo mengine aliwasisitiza wanawake kuhubiri amani na upendo kwani amani haiwezi kuchezewa , ni tunu ambayo haiwezi kufanyiwa utani popote ulimwengu maana ikipotea inaleta madhara hata kwa familia na siyo adui tu.

Kadhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani,  Sheikh Ramadhan Mtupa alitaja mada zilizojadiliwa  katika kongamano hilo kuwa ni kudumisha amani nchini,  kuishi kwa kuvumiliana, nafasi ya mwanamke wa kiislamu katika kuleta na kudumisha amani, machango wa vyama vya siasa ,vyombo vya dola na jamii kudumiosha amani.

Akifunga  kongamano hilo, Katibu wa JUWAKITA wa Mkoa huo,  Azama Masasa aliwataka   wanawake kudumisha amani kuanzia watoto na wawaletee kwa maadili ya kumuoga Mungu ili kuondokana na taifa lenye vijana wadogo wanaojihusisha na dawa za kulevya na mambo mengine ya uvunjifu wa amani
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment