WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, September 23, 2013

Azam yaichakaza Yanga


Wachezaji wa Yanga wakiwa hawaamini kilichotokea baada ya kufungwa bao la tatu katika dakika ya 90 na Azam. Picha na Michael Matemanga. 

Azam ilifunga bao dakika ya kwanza na dakika ya 90.
Dar es Salaam / Tanga. Mshambuliaji chipukizi, Joseph Kimwaga aliingia akitokea benchi na kuifungia Azam bao la ushindi hivyo kuichapa Yanga kwa mabao 3-2 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kimwaga aliyeingia katika dakika ya 73 kuchukua nafasi ya Farid Musa, aliwakata maini mashabiki wa Yanga waliojitokeza kwa wingi uwanjani hapo baada ya kufunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Azam waliuanza vizuri mchezo huo na kupata bao la kuongoza katika dakika ya kwanza kupitia kwa mshambuliaji John Bocco, lakini Yanga walisawazisha kupitia Didier Kavumbagu kabla ya Hamisi Kiiza kupachika bao la pili katika dakika ya 65, lakini dakika nne baadaye Azam walisawazisha kwa penalti ya Kipre Tchetche baada ya Haruna Niyonzima kushika mpira eneo la hatari.

Wakati mashabiki wakiamini mechi hiyo itamalizika kwa sare 2-2, Azam walifanya shambulizi la kushtukiza na Kimwaga alimalizia vizuri kwa shuti kali lililojaa wavuni katika dakika ya 90 na kufanya mchezo huo kumalizika kwa 3-2.
Kocha wa Azam, Stewart Hall amewasifu wachezaji wake kwa kutumia nafasi chache walizopata kupata ushindi huo.

“Yanga walicheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini vijana wangu walitumia nafasi chache walizozipata kupata ushindi huu,” alisema Hall.
Yanga watajilaumu wenyewe kwa kipigo hicho baada ya washambuliaji wake Jerryson Tegete na Haruna Niyonzima kupoteza nafasi nyingi za kufunga wakiwa wao na kipa Aishi Manula. 

Katika michezo mingine JKT Ruvu na Ruvu Shooting wamepokea vipigo vya kwanza msimu huu baada ya kufungwa bao 1-0  na Oljoro JKT na Coastal Union.
Tanga. Coastal Union wakiwa kwenye uwanja wao wa Mkwakwani walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting. Kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ aliwainua mashabiki wa Coastal dakika ya 80 akiunganisha vizuri krosi ya  Keneth Masumbuko.

Chamazi, JKT Ruvu walikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Oljoro JKT shukrani kwa goli la Paul Malipesa.

source: mwananchi

No comments:

Post a Comment