WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, September 23, 2013

Amisi Tambwe ang'ara Simba ikishikwa

Mshambuliaji aliye katika kiwango cha kucheka na nyavu kama ananawa Amisi Tambwe, alifikisha jumla ya mabao sita katika mechi mbili za ligi kuu ya Bara jana, lakini akaangushwa na matokeo baada ya Simba kulazimishwa sare ya 2-2 na Mbeya City katika mechi ya kusisimua, kwenye Uwanja wa Taifa.
Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 11 kutokana na michezo mitano, pointi tano mbele ya Yanga ambao wana mchezo mmoja mkononi hata hivyo huku City iliyopanda daraja ikiwa pointi moja juu ya mabingwa watetezi hao.
Richard Peter aliyeingia kutoka benchi aliifungia City iliyotawala mchezo huo kwa muda mwingi bao la kusawazisha dakika 10 tangu aingie uwanjani kuchukua nafasi ya Mwagane Yeya katika dakika ya 60, alipounganisha mpira wa adhabu ndogo wa Anthony Matogolo.
City ambayo ilitoka sare ya 1-1 na Yanga katika raundi ya tatu, ingeweza kuibuka na ushindi dhidi ya kigogo kingine cha ligi kuu jana kama si uhodari wa Abel Dhaira aliyepangua mpira hatari wa Peter na kuwa kona katika dakika ya 72.
Tambwe ambaye alifumania nyavu mara nne katika mchezo dhidi ya Mgambo JKT katikati ya wiki, aliifungia Simba bao la kuongoza na lake la tano katika michezo miwili nusu saa tangu kuanza kwa mchezo huo.
Mkali huyo aliyesajiliwa kutoka Vital'O ya Burundi katika dirisha lililopita la usajili, alifunga bao hilo baada ya kupokea pasi ya Harun Chanongo na kupiga shuti lililomshinda David Baruani katika lango la City.
Kuchukuliwa kwa Tambwe kulikuwa ni jitihada za dakika za majeruhi za Simba kumaliza tatizo la ufungaji linaloikabili tangu Januari ilipomuuza Mganda Emmanuel Okwi ambaye jana alikuwa mmoja wa watazamaji uwanjani hapo kwa Etoile du Sahil ya Tunisia.
Ilimchukua mfungaji bora wa Kombe la Kagame la klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Tambwe dakika tatu zaidi kuipatia Simba bao la pili, akitumbukiza wavuni mpira kutokana na pasi ya Betram Mwombeki.
Shangwe za Simba zilitulizwa japo kwa muda katika dakika ya 37 baada ya City, ambayo ilitawala dakika 20 za kwanza na 10 za mwisho za kipindi cha kwanza, kupata bao kupitia kwa Paul Nonga kutokana na shuti kali.
Timu zilikuwa:
SIMBA: Abel Dhaira, Wiiliam Lucian, Issa Rashid, Gilbert Kaze (Hassan Khatib dk.65), Joseph Owino, Jonas Mkude, Twaha Ibrahim (Ramadhani Chombo dk.50), Amri Kiemba (Ramadhani Singano dk.79), Betram Mwombeki, Amisi Tambwe, Harun Chanongo.
CITY: David Baruani, John Kabanda, Hassan Mwasapili, Deo Julius, Yohana Morris, Anthony Matogolo, Mwagane Yeya (Richard Peter (dk.60), Steven Mazanda, Paul Nonga, Deus Kaseke, Yusuph Wilson.    
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

No comments:

Post a Comment