WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, July 7, 2013

Daktari: Moyo wa Mandela ulisimama


mandela 20073 

KUHARIBIKA kwa gari la wagonjwa lililombeba Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, kulisababisha moyo wa shujaa huyo kusimama kwa dakika 40.

Hayo yalibainishwa na daktari wa moyo anayemtibu shujaa huyo wa Afrika Kusini, kwamba Juni 8, mwaka huu, wakati akipelekwa hospitali gari lililombeba lilipata hitilafu njiani na kukwama kwa muda.

Daktari huyo wa moyo anayeheshimika nchini Afrika Kusini, (jina linahifadhiwa) alisema jana kuwa gari la wagonjwa lililokuwa likimpeleka Mandela hospitali liliharibika katika njiapanda ya Gauteng na kusababisha wasubiri gari lingine kwa zaidi ya dakika 45. (HM)

“Moyo wake ulisimama kabisa tukiwa ndani ya gari, ikatubidi tumfufue kwa mashine (resuscitate),” alithibitisha daktari huyo bingwa.
Ripoti inaeleza kuwa gari hilo la wagonjwa linalomilikiwa na jeshi, liliharibika wiki tatu zilizopita kati ya Pretoria na Johanersburg.

Chombo cha habari cha Marekani, CBS kiliripoti jana kuwa moyo wa Mandela ulisimama kwa dakika kadhaa kabla gari lingine halijaletwa na kumpeleka Mandela katika hospitali ya Medi-Clinic.

Wakati moyo wa Mandela uliposimama, nje kulikuwa na baridi kali kiasi cha nyuzi joto sita tu, hali ambayo inaelezwa kuwa ilichangia kuharibu zaidi mapafu ya Baba wa Taifa la Afrika Kusini.

“Mke wa Mandela, Graca Machel, alikuwa amechanganyikiwa kwa dakika hizo 40, ambazo tulikuwa tukisubiri gari lingine,” kilisema chanzo hicho.
Ingawa msemaji wa Rais Jacob Zuma, Mac Maharaj alisema kuwa madaktari wamethibitisha kuwa Mandela hakupata madhara makubwa kutokana na baridi hiyo, madaktari wengi wameonyesha kupingana naye.
Daktari wa moyo, David Janekelow alisema, kutokana na hali yake, ucheleweshaji wa aina yeyote ile lazima ulisababisha madhara.

“Unahitaji kupata matibabu ya dharura haraka iwezekanavyo. Kama mtu tayari alikuwa anafufuliwa, ucheleweshaji wa kumpeleka hospitali lazima ulete madhara,” alisema Janekelow.

Daktari mwingine wa moyo, Richard Nethonde alisema, Mandela angekufa pale barabarani wakati wanasubiri gari la wagonjwa liletwe, imekuwa ni kama bahati hakufa.

Wakati huohuo, gazeti la the Sunday Times limeeleza kuwa Graca, mke wake analala katika chumba kilicho pembeni ya chumba anacholala Mandela, kwa siku zote, tangu Mandela alazwe.

Wakati huohuo, wakili wa mjukuu wa Mandela, Mandla Mandela, amesema atafungua mashtaka kwa baadhi ya wanafamilia ya Mandela kwa kuidanganya mahakama kuhusu hali ya shujaa huyo.

Wakili huyo, Gary Jansen alisema kuwa wanafamilia hao walipeleka hati yenye maneno ya uongo mahakamani wakieleza kuwa Mandela yu mahututi, jambo ambalo limekanushwa na Rais, Jacob Zuma aliyemtembelea juzi.

“Tutapeleka malalamiko ambayo yatatokana na hati ya kiapo iliyopelekwa mahakamani na wanafamilia 15 wa Mandela, kwa ajili ya kufukua miili ya watoto wa Mandela,” alisema Jansen.

Wakili huyo alisema kuwa, wanafamilia hao walipeleka hati hiyo wakiitaka mahakama ichukue uamuzi wa haraka kwani afya ya Mandela ni mbaya, jambo ambalo ni la uzushi.

“Lazima tufanye uchunguzi wa kutosha kwa sababu mwanasheria wa familia hiyo, ametumia hati ya kiapo vibaya” alisema Jansen.

Wakati hayo yakiendelea, wananchi wengi Afrika Kusini wanaendelea kukusanyika katika viwanja vilivyopo karibu na Hospitali alikolazwa Rais Mandela kumuombea ili apate nafuu mapema.

Habari kutoka ndani ya familia ya Mandela zinaeleza kuwa huenda mgogoro mkubwa zaidi ukaibuka endapo Mandla atatimiza azima yake ya kufungua kesi nyingine. 

Chanzo: mwananchi

No comments:

Post a Comment