WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, January 30, 2014

YANGA WAMEMNUNUA WAPI EMMANUEL OKWI?




Na BARAKA MBOLEMBOLE
Wakati ligi kuu ikianza, mchezaji mwenye thamani kubwa zaidi, Mganda, Emmanuel Okwi amekuwa mmoja wa watazamaji mwenye thamani kubwa. Je, Yanga wameingia ' mkenge' katika usajili wake?. Hili linaweza kuwa swali ambalo majibu yake yapo wazi. Kwanza, Okwi ni mchezaji wa Etoile du Salehe ya Tunisia ambao walimnunua kutoka timu ya Simba.

Kwa nini yupo Yanga?. Alikuwa akiichezea timu ya SC Villa ya kwao Uganda kwa mkataba wa mkopo wa miezi sita akitokea Etoile. Narudia tena, alikuwa akiichezea Villa kwa mkopo. Fifa ilimruhusu Okwi kucheza Villa kwa muda wakati kesi tatu zinazomuhusu Mganda huyo zikitafutiwa mhuafaka. Okwi kwa upande wake anadai kuwa Watunisia hao walivunja mkataba kwa kushindwa kumlipa pesa zake kama ilivyotakiwa. Simba nao wanadai malipo yao kutoka kwa Etoile.

Okwi aliruhusiwa kuichezea Villa ili kulinda kiwango chake, na wala hakuwa mchezaji anayemilikiwa na timu hiyo. Alizuiwa kuichezea timu ya Taifa ya Uganda katika michuano inayoendelea ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani, CHAN, kwa kuwa alikuwa Villa kwa mkopo kutoka timu ya ng'ambo. Ila, ni Villa ndiyo wanaosemekana kumuuza Okwi kwa timu ya Yanga. Kwa mamlaka gani?. Hadi hapa Yanga watakuwa wameliwa. Kwa kuwa Okwi ni mchezaji wa Etoile si Villa.

Yanga wamemsaini Okwi huku wakijiaminisha kuwa wapo sahihi. Wanaamini Okwi ni mchezaji huru au wa Villa. Ila, alitakiwa kucheza Villa kwa miezi sita, lakini akaitumikia miezi isiyozidi miwili tu na kununuliwa. Caf, Shirikisho la soka Afrika wamemuhidhinisha Okwi kuichezea Yanga. Kamati ya sheria na hadhi ya wachezaji imemzuia matumizi yake hadi watakapopata ufafanuzi kutoka FIFA, Shirikisho la soka ulimwenguni. 
Ndiyo, wapo sahihi kwa kuwa FIFA, ndiyo waliosema mchezaji huyo acheze Villa kwa miezi sita wakati kesi zake zikishughulikiwa. 

FIFA, wanaweza kumruhusu Okwi kuchezea Yanga kwa maslai ya kipaji chake. Ila, wanaweza pia kumzuia endapo watajua kuwa mchezaji huyu amekiuka maagizo yao ya awali ambayo walimwambia acheze Villa. Inawezekana mchezaji huyo akaonekana tapeli, kwa kuwaadaa Yanga wakati akijua fika mkataba wake upo Etoile. Wapo wachezaji walioshinda vita kama hii ya Okwi, ila wapo pia walioingia katika vifungo vya FIFA. 

Huenda Yanga wakamtumia Okwi siku za mbele, ila kwa sasa ni uhalali wa mchezaji huyo. Kama, Etoile wataendelea kushikilia msimamo wao kuwa hawajui mchezaji wao mahali alipo, Okwi ataoneka ni mtoro. Endapo, Okwi ataonekana ni halali madai yake anaweza kulipwa fidia na Etoile, ila kasheshe ni wapi ambapo Villa walipata kibali cha kumuuza Okwi kwa timu ya Yanga?

Kila upande udai una wanasheria wake. Duh!. Lakini mwanasheria wa Okwi anaweza kuwa mjanja zaidi, mwenye akili zaidi, kwa kuweza kupata saini na mamillioni ya Yanga kwa ufafanuzi wake wakati akimpigia debe mteja wake kuwa hana tatizo. Kama sheria iliwekwa ili ivunjwe, na kama mikataba siku zote inaweza kutenguliwa, Yanga watamtumia Okwi, ila tusije kushangaa FIFA, wakisema mchezaji huyo mali ya Etoile. Yanga walimnunua wapi Emmanuel Okwi? Labda hapa ndipo kuna hoja ya msingi.

Source: shaffih Dauda blog

No comments:

Post a Comment