WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, January 6, 2014

Mwigamba, Kitila 'out' Chadema

 
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa akitoa tamko la Kamati Kuu ya chama hicho kwa waandishi wa habari, Dar es Salaam jana. PICHA:SELEMANI MPOCHI
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewatimua, Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba, huku kikiwataka wanachama kutoshiriki mikutano ya nje na ya ndani au shughuli nyingine yoyote ya kisiasa itakayofanywa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe na mawakala wake kwa jina la Chadema.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alitangaza uamuzi wa Kamati Kuu jana mbele ya waandishi wa habari na wanachama wa chama hicho, iliyokutana Januari 3 hadi 4, mwaka huu kujadili masuala mbalimbali likiwamo la wanachama hao.
ZUIO LA ZITTO
Mwishoni mwa wiki, Zitto kupitia wakili wake, Albert Msando, aliiomba mahakama asijadiliwe katika kikao cha CC cha Januari 03, mwaka huu, kuhusu uanachama wake hadi hapo rufani yake itakapotolewa uamuzi na Baraza Kuu.
Wakati Dk. Slaa akisema hayo, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, alisema uanachama na Ubunge wa Zitto utaendelea kuwapo kutokana na kesi iliyopo mahakamani na si kwa matakwa ya Chadema.

MASHITAKA DHIDI YAO
Dk. Slaa alisema washtakiwa wote walishtakiwa kwa mashtaka 11 yanayohusu ukiukwaji wa vifungu mbalimbali vya katiba ya chama, kanuni za uendeshaji kazi za chama, kanuni za kusimamia shughuli, mwenendo na maadili ya wabunge wa chana na mwongozi wa kutangaza kusudio la kuwania nafasi ya uongozi kwenye chama, mabaraza na serikali.

Alisema mashtaka yote yalitokana na watuhumiwa kuandaa kile kinachoitwa mkakati wa mabadiliko, 2013, uliojikita katika kukashfu viongozi wakuu wa chama, kutokuwa wakweli na wawazi kwa kushirikiana na vikundi vya majungu kwa kuanzisha na kuratibu mtandao wa siri ulioitwa ‘mtandao wa ushindi’ nje ya utaratibu wa chama ili kumwezesha Zitto kutwaa nafasi ya Mwenyekiti wa chama Taifa.

Mengine ni kutoa tuhuma za uongo dhidi ya viongozi wa chama na bila kupitia vikao halali vya chama, kujihusisha na vikundi nyenye misingi ya ukabila, udini na ukanda vyenye makusudi ya kubaguana ndani ya chama na miongoni mwa jamii, kujihusisha na vikundi na vitendo vya kuchinganisha au kuzua migogoro ndani ya uongozi wa chama na wanachama wake.

Kuandaa na kutekeleza mpango wa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama Taifa bila kutangaza kusudio la kufanya hivyo kwa mujibu wa mwongozo wa chama, kutengeneza makundi na mitandao haramu ya kuwania uongozi ndani ya chama kinyume na mwongozo wa chama, kuwachafua viongozi na wanachama wenye nia au kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama kinyume cha mwongozi wa chama.

MWIGAMBA AINGIA MITINI
Alisema aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha, Mwigamba, hakutokea katika kikao hicho licha ya kuthibitisha kushirikia kwenye CC kwa ajili ya kujitetea kwa mdomo.

DK. MKUMBO AJITETEA
Alisema aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk. Mkumbo alihojiwa kwa mdomo na CC na kukiri baadhi ya makosa na mengine aliyakana huku akikataa kumtaja Mhusika wa Pili (M2) katika waraka wa mkakati wa mabadiliko 2013, uliodaiwa kuandaliwa nao hadi atakapopata ridhaa yake. Katika utetezi wake wa maandishi, alikanusha na kukataa tuhuma zote za kukiuka katiba ya chama, kanuni na mwongozo na kwa maneno yake mwenyewe alikanusha na kwamba mashtaka si ya kweli.

USHIRIKI WA ZITTO KATIKA MKAKATI HUO
Alisema licha ya Ziito kukanusha kuufahamu mkakati huo, lakini Dk. Mkumbo katika mahojiano na CC alikiri kuwa walimpa taarifa juu ya makakati huo na alikuwa anaufahamu.

“Ukweli huu unathibitishwa na mawasiliano ya barua pepe iliyotumwa na Zitto kwa mtu anayejiita Chadema Mpya 2014 wa Oktoba 27, mwaka 2013, ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya kikao cha CC kilichowavua madaraka,” alisema.

Alisema kuhusu tuhuma za ufisadi ndani ya chama licha ya Dk. Mkumbo kuonyeshwa taarifa mbalimbali ambazo yeye na Zitto walishiriki kupitisha kwenye CC, nyaraka za manunuzi, hakuweza kuthibitisha kwa namna yoyote.

MAAMUZI YA CC
Dk. Slaa alisema mkakati huo haukuwa na lengo la kumwezesha Zitto kutwaa nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama pekee, bali ulikuwa na malengo makubwa zaidi ya kukibomoa chama kwa kukichafua kwa wananchi na kuwachafua viongozi wake wa juu kwa kutumia tuhuma za uongo za ufisadi.

Alisema kwa maoni ya CC, chama cha siasa ambacho viongozi wake wa juu wanatuhumiwa kwa ufisadi hakiwezi kuaminiwa na wanachama kama tumaini lao la ukombozi.

Alisema CC imeridhika kwa ushahidi wa nyaraka mbalimbali zilizoandaliwa na Zitto ama mawakala wake wakitumia vitambulisho bandia katika mitandao ya mawasiliano ya kijamii kwamba mkakati wa kukibomoa chama umeandaliwa na kutekelezwa kwa muda mrefu.

Alisema mkakati huo ulihusisha pia hujuma dhidi ya chama kwa kuwaengua wagombea wake katika chaguzi mbalimbali kama ilivyotokea katika majimbo ya Mpanda Mashariki, Musoma Vijijini na Singida Mjini ambako alidai Zitto alishiriki moja kwa moja.  
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment