WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, January 27, 2014

bunge la katiba kizungumkuti


arioba_28998.jpg

Dar es Salaam. Sheria ya Mabadiliko ya Katiba bado ina upungufu ambao utaathiri utendaji wa Bunge Maalumu, ambalo huenda likaanza Februari 11 mwaka huu, mjini Dodoma.
Sheria hiyo Namba 8 ya 2011, imeishafanyiwa marekebisho mara mbili yakiwamo ya Februari 2012 na Novemba 2013, lakini mabadiliko hayo yameacha kasoro ambazo zinapaswa zifanyiwe tena kazi, kupitia Bunge. (JM)

Kasoro zipo katika Kifungu cha 22 kinachohusu uchaguzi wa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum, pamoja na kifungu cha 24 kinachozungumzia Katibu na Naibu Katibu wa Bunge hilo wanavyoanza kutekeleza wajibu wao.

Kupitia Sheria ya Marekebisho (Na:2) ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 2013, Bunge katika mkutano wa 12, liliwapa mamlaka Katibu wa Bunge na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, 'kufanya maandalizi muhimu kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Bunge Maalumu'.

Watendaji hao kwa mujibu wa sheria ndio watakaoteuliwa kuwa Katibu na Naibu Katibu wa Bunge Maalumu baada ya Rais kutangaza kuitishwa kwa Bunge hilo, lakini kiapo chao kitasubiri hadi pale watakapochaguliwa Mwenyekiti na Makamu wa Bunge hilo.

Sheria husika inaweka sharti kwamba ikiwa Mwenyekiti atatoka upande mmoja wa Muungano basi Katibu atoke upande mwingine na kinyume chake. Hivyo lazima wasubiri uchaguzi huo ili wajue ni nani Katibu na Naibu Katibu.

Kifungu cha 24 (2) kinasema: "Katibu na Naibu Katibu wa Bunge Maalumu, watashika nyadhifa zao kwa misingi kwamba, endapo Mwenyekiti atachaguliwa kutoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano basi Katibu wa Bunge Maalumu atatoka upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano".

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa tayari baadhi ya wataalamu kutoka Ofisi ya Bunge na ile ya Baraza la Wawakilishi (BLW) wameanza maandalizi ya awali katika moja ya hoteli za jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashililah mbali na kukiri kuanza kwa maandalizi hayo, hakuwa tayari kuzungumzia kwa undani suala hilo kwa maelezo kuwa lazima ashirikiane na Katibu wa Baraza la Wawakilishi.

Hata hivyo, kutokana na mkanganyiko mkubwa uliopo katika Sheria hiyo, ni dhahiri watendaji hao watapata wakati mgumu katika kuanza kutekeleza majukumu, hasa katika kuteua wajumbe wa sekretarieti ya Bunge hilo.

Uteuzi wa wajumbe hao kwa mujibu wa kifungu cha 24 (4) unapaswa kufanywa na Katibu kwa kushauriana na Naibu wake, nafasi ambazo hazitakuwapo hadi pale Mwenyekiti na Makamu wake watakapochaguliwa. 

CHANZO MWANANCHI

No comments:

Post a Comment