WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, June 28, 2014

SIMBA SC YAWAALIKA WANACHAMA, WANAHABARI KUONA MAENDELEO YA UWANJA BUNJU

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

AZAM FC pekee ndio klabu ya Tanzania yenye uwanja wake wa kisasa kwa ajili ya mazoezi, mechi za ligi kuu na michuano yote inayosimamiwa na shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
Katika historia ya soka la Tanzania, Azam fc haiwezi kunusa ukongwe wa klabu mbili za Simba na Yanga.
Hizi ni klabu zenye mafanikio ndani na nje ya uwanja. Ni klabu zenye mashabiki kila kona ya nchi hii.

Lakini licha ya kukaa miaka mingi katika soka la ushindani nchini Tanzania na michuano ya Kimataifa, Yanga na Simba hazijawahi kumiliki viwanja vyake vya mazoezi na mechi za ligi kuu.
Kwa miaka mingi sasa viongozi wanaopita katika klabu hizo wanakuja na ndoto za kujenga viwanja, lakini zinayeyuka kutokana sababu mbalimbali ikiwemo kuendekeza siasa kuliko vitendo.

Kwasasa mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ana mkakati kabambe wa kujenga uwanja wa klabu hiyo maeneo ya Jangwani, wakati huo huo, naye mwenyekiti wa Simba, Alhaj Ismail Rage akipambana na mpango kama huo maeneo ya Bunju jijini Dar es salaam.

Kwa miezi miwili sasa, Uongozi wa Simba unaendelea na ujenzi wa uwanjao wake na sasa umefikia hatua nzuri ya kuanza kutumika kwenye mazoezi ya klabu hiyo ikiwa ni mara ya kwanza kumiliki uwanja katika historia yake.

Kutokana na maendeleo hayo,uongozi wa Simba umewakaribisha wapenzi na wanachama wake kesho  Jumamosi katika Uwanja wao Bunju kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mazoezi wa klabu.

Katibu mkuu wa Simba sc, Ezekiel Kamwaga amesema ujenzi huo ulioanza miezi miwili iliyopita, unakaribia kukamilika na utakuwa uwanja wa kwanza rasmi wa mazoezi wa klabu katika historia yake.
Vyombo vya habari navyo vinaalikwa katika tukio hilo litakaloanza saa tano kamili asubuhi.

source: matukiotz.com

No comments:

Post a Comment