WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, June 8, 2014

MSANII MZEE SMALL AFARIKI DUNIA..

1_e4ab8.jpg

MZEE SMALL
Muigizaji mkongwe nchini, Said Ngamba maarufu kwa jina la Mzee Small amefariki dunia usiku huu akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar. Mzee Small amefariki kwa ugonjwa wa presha baada ya kuugua kwa muda mrefu kabla ya kuzidiwa jana na kupelekwa Muhimbili. Mtoto wa marehemu aitwaye, Muhidin amethibitisha kifo cha Mzee Small
HISTORIA YA MAREHEMU MZEE SMALL


Marehemu Mzee Small akiwa na mkewe Bi. Fatuma.
Jina lake ni Said Ngamba maarufu kwa jina la Mzee Small (58). Amezaliwa mwaka 1955. Alikuwa msanii mkongwe wa vichekesho na maigizo hapa Bongo.
Mzee Small (kushoto) akiwavunja mbavu JB, Mzee Mbizo na Richie.
Mzee Small alipata elimu ya msingi katika Shule ya Mingumbi huko Kilwa mkoani Pwani. Mbali na kuwa mkongwe, Mzee Small kila ulipozungumza naye alikuwa na kawaida ya kutamba kuwa yeye ndiye msanii wa kwanza kabisa Tanzania Bara kuchekesha runingani.
Mzee Small alianza sanaa hiyo yapata miaka 30 iliyopita na alipata kufundishwa na mwigizaji Said Seif ‘Unono’ (kwa sasa na yeye ni marehemu).
Mbali na kushiriki sanaa katika vikundi mbalimbali, Mzee Small ametumika katika vikundi vya…

source: global publisher

No comments:

Post a Comment