WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, September 7, 2014

Dk Shein agoma kukutana na Ukawa Zanzibar


Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.PICHA|MAKTABA 

Zanzibar. Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ametupilia mbali maombi ya kumtaka kufungua mazungumzo na  viongozi wa Ukawa, ili kupatikana kwa mwafaka kwa wabunge wa Bunge la Katiba kutoka  Zanzibar na kurejea  bungeni.
Akizungumza na Mwananchi Katibu wa Kamati ya Kuwaunganisha wabunge kutoka Zanzibar, Mohamed Yussuf Mshamba amesema kamati yake imepokea barua maalumu kutoka Ofisi ya Rais ikiwataarifu kuwa Rais hayuko tayari kufungua mazungumzo hayo.
 “Tumepokea majibu kutoka Ofisi ya Rais, Ikulu  Zanzibar, tumeelezwa kuwa suala hilo ni vyema likabaki mikononi mwa Bunge  la Katiba na suala la usuluhishi imeshauriwa tufanye wenyewe ZIRPP,” alisema Mshamba.
 Aidha alisema kwamba kutokana na msimamo huo wa Rais Dk Shein, kazi ya kuwaunganisha wabunge wa Zanzibar imekuwa ngumu kwa vile  matarajio ya ZIRPP ilitegemea kazi hiyo ingerahisishwa na Rais na kuzika tofauti ya  kimsimamo.
 Mshamba alisema maombi yao waliyawasilisha Agosti mwaka huu  baada ya kamati ya kuwaunganisha Wazanzibari kukamilisha kazi ya kukusanya maoni ya wananchi kupitia kongamano la wazi juu ya nini kifanyike  na kuhakikiisha Wazanzibari wanamaliza tofauti zao na kutetea maslahi ya Zanzibar.
‘Kwa ufupi kazi ambayo tumekuwa tukijaribu kuifanya imekuwa ngumu, tunachowaomba wabunge wa Zanzibar waache tofauti za kiitikadi na kuweka mbele maslahi ya Zanzibar, njia pekee rahisi na mwafaka warudi  bungeni kushirikivikao,” alisisitiza Mshamba.
Alisema kimsingi kuna makosa yaliyofanyika tokea mwanzo,  ikiwa ni pamoja na utungaji wa sheria yenyewe ya Bunge la Katiba na kujikuta wakiingizwa wanasiasa kwenye Bunge hilo, badala ya kuwa la wataalamu na watu wengine wasiotokana na vyama vya kisiasa.
Mshamba alieleza kuwa kuanza kwa ‘mguu’ huo mbaya kumesababisha kuzuka kwa mivutano na mijadala yenye mitazamozaidi ya itikadi za kisiasa badala ya kuongozwa na nguvu ya hoja, ufahamu, upembuzi yakinifu na uzoefu wa wabunge wa Bunge hilo.
“Chadema pekee ndicho ambacho katika ilani yake iliahidi kuwa kikishika madaraka ya uongozi  kitabeba jukumu la kuandika katiba mpya, si CCM, NCCR-Mageuzi, TLP wala  CUF vilivyoahidi jambo hilo, sasa  inashangaza kuona vyama hivyo vimekuwa mstari wa mbele  kushupalia Katiba Mpya na kususia Bunge  la Katiba,” alisema Mshamba
source: mwananchi

No comments:

Post a Comment