WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, August 30, 2012

VIONGOZI WAJADILI NAMNA YA KUKABILI TATIZO LA AJALI ZA BARABARANI NCHINI


  • JIBU NI MOJA TU WANAWEZA KUSIMAMIA SHERIA IPASAVYO?

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uthibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA),akifafanua jambo katika mkutano wa kujadili namna bora ya kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani,Kulia kwa Mkurugenzi wa SUMATRA ni Mkurugenzi wa Idara ya Usalama na Mazingira Wizara ya Uchukuzi,Bi. Tumpe Mwaijande.Kulia kwa Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe.Pereira Ame
Silima (aliyevaa suti nyeusi)ni Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Dkt. Harrison G. Mwakyembe na kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe. Dkt. Emmanuel J. Nchimbi(Mb).
 Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi,Said Mwema akichangia jambo katika Mkutano uliowakutanisha Waziri wa Uchukuzi,Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe(Mb) aliyevaa suti nyeusi,na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe. Dkt. Emmanuel J. Nchimbi(Mb) aliyevaa suti ya kaki.Mkutano huo ulifanyika Wizara ya Uchukuzi na kuwakutanisha SUMATRA,Jeshi la Polisi,Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji(NIT), Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na viongozi mbali mbali wa Wizara ya Uchukuzi lengo likiwa kujadili namna ya kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani Nchini.
Waziri wa Uchukuzi,Mhe Dkt. Harrison G.Mwakyembe(Mb),akisisitiza jambo kwenye mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.Kulia kwa Waziri Mwakyembe (aliyevaa suti ya kaki) ni Waziri huyo wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe. Dkt. Emmanuel J.Nchimbi(Mb),kulia kwa Waziri Nchimbi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Bw. Mbarak Abdulwakil  na kulia kwa Katibu Mkuu wa Mambo ya Ndani ni Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi Said Mwema.

habari kwa Hisani ya Michuzi Blog

No comments:

Post a Comment