WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, August 13, 2012

TAFSIRI YA KUJIUZURU KATIKA UTENDAJI WA SERIKALI ZETU:


JE KUJIUZULU KWA WATENDAJI WETU WA NGAZI ZA JUU NI SOLUHISHO LA TATIZO?





CHANGAMOTO KWA MHESHIMIWA RAIS JAKAYA M. KIKWETE NA DR.ALI MOHAMED SHEIN;

Taafsiri ya kujiuzulu  kwa maneno ya kawaida  ni kuacha (Dhamana) ya utendaji ambayo kiongozi ambaye amepata shinikizo la Kujiuzuru analazimika kuachia madaraka ikiwa ni sehemu ya  uwajibika wa pamoja kiserikali kutokana kushindwa kutekeleza majukumu ambayo kiongozi muhusika alitakiwa kuyatenda au kuyasimamia kulingana na kiapo chake cha kazi.

Katika nchi ambazo zimeendelea kiuchumi na kisiasa dhana hii ni jambo la kawaida na hutekelezwa bila shinikizo kubwa sana. Kinyume chake Katika  nchi nyingi za zinazoendelea  Tanzania ikiwamo tunajua utekelezaji wa dhana hii huwa mgumu sana na ukitendeka inakuwa baada ya shinikiza kubwa wakati mwingine kutoka kwa wananchi hii inatokana sana na kulindana kisiasa.

mheshimiwa edward lowasa alilazimika kujiuzuru

JE KUKIMBILIA KUJIUZURU NI SOLUHISHO LA TATIZO?

Kwa nchi yetu Tanzania Pengine kama wanazuoni wengi walivyowahi sema kuwa "Kukimbilia kujiuzulu siyo suluhu sana ya tatizo. Kwasababu kama ni hivyo, watu wanaweza kuharibu mambo kwa makusudi wakitegemea watajiuzulu na kukaa pembeni." Kwani dhana hii ya kujiudhulu haihusishi adhamu ya ya moja kwa moja kama ya kushitakiwa kwa utendaji huo mbovu uliobainishwa. Tatizo langu daima ubaki kuwa je tunapomshinikiza kiongozi kujiudhru tunakuwa tayari tumeshabaanisha tatizo, na hata akichaguliwa kiongozi mwingine kushika nafasi anajua anatakiwa kufanya nini? Je tatizo ni mtu au ni mfumo? Kama ni mtu basi ni sahihi kumshinikiza kiongozi mwenye dhamana kuachia ngazi; lakini kam tatizo ni mfumo wa utawala nina mashaka kama kweli kujizuru kunasaidia kuondoa tatizo linalopigiwa kelele kwa wakati husika.

Tatizo linalokabila taifa letu kwa sasa mfumo wetu wa utawala umevamiwa na ufisadi. Swali la kujiuliza ni moja tu je huu ufisadi ni utamaduni wetu? au ni ugonjwa tu umeingia ambao unatakiwa kutibiwa mara moja kwa njia ambazo wengi wamezisema na wengine kuzitumia ? tupende au tusipende inaonekana ni mfupa uliotushinda Jibu lipo wazi tunajua tatizo lakini hatujui chanzo cha tatizo

MHESHIMIWA DR.IBRAHIM MSABAA ALILAZIMIKA KUJIUZURU;

Mheshimiwa Mtei aliwahi sema kuwa “Nilifanya kazi Mwalimu Nyerere, alikuwa kiongozi ambaye hasiti kuwachukulia hatua viongozi waliokuwa wakimwangusha katika utendaji wake,” nafikiri itakuwa ni vyema kwa viongozi wetu wa ngazi za juu kama wataweza kuwachukulia hatua za uwajibikaji za haraka sana watendaji wote wabovu wanao haribu mfumo mzuri wa utawala, na hatimaye kulipeleka taifa letu katika nyia ambayo sisi hatuko tayari kwenda huko kwa manufaa yao binafsi.

TUKITAFAKARI SAKATA LA KUZAMA MELI MV.SKATIG JE TATIZO NI WAZIRI AU MFUMO MZIMA?


MHESHIMIWA HAMAD MASOUD ALILAZIMIKA KUJIUZURU KUFUATIA AJALI YA MELI MV.SKATIG

Katika sakata hili wanazuoni wengi wamebainisha tatizo ambalo tunakabiliwa nalo kama taifa sio swala la kujiuzuru kwa viongozi, tunatakiwa kwanza tuimarishe mfumo wetu wa utendaji kwa maneno mengine mfumo ambao tunao wa kiutawala ni dhaifu. Na kielezo kimoja kati ya vingi ni pale viongozi wetu wanaziona nyadhifa zao ni sawa na hati milikizao! Hivyo kwao  hawawajibiki kuishi au kuongoza kulingana na maadili ya uongozi. Wamesahau kabisa kanuni za uongozi kuwa “Cheo ni dhamana, sitakitumia cheo changu kwa faida yangu binafsi au kwa faida ya familia yangu”.

DR.Bana,Mallya na Prof. Mpangala kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam waliwahi sema kuwa tunatakiwa kubadilisha mfumo hasa kwa kujenga utamaduni wa kujiuzuru Bali kuimarisha  maadili ya kazi na uongozi kwa watumishi wa serikali na pale kosa linapofanyika wahusika  wafikishwe mahakamanimara moja.

Emmanuel Mallya alisema licha ya kuwa mabadiliko yamefanyika lakini sio suluhisho kutokana na nchi kuwa na mfumo mbovu wa utawala.  
Alisema mawaziri  waliokumbwa na kashfa mbalimbali walitakiwa kusimamishwa kazi ili wachunguzwe na kama ingebainika hawana hatia wangerudishwa kazini.  “Kama wangekutwa na hatia wangefunguliwa mashitaka, hii ingewafanya wengine kuogopa kutafuna mali za umma kwa kuhofia kuwa watasimamishwa kazi na kuchunguzwa”

Dk Bana alishawahi sema kuwa dawa ni kubadilisha mfumo mzima wa utawala.  

Katika kufanikisha kuboresha mfumo bora wa utawala mti ukigolewa ungolewe wote pamoja na mizizi yake; watendaji wote katika kila ngazi wanatakiwa kuchukuliwa hatua kwa kufanya hivi tutaweza kukomesha tabia ya ubinafsi inayoota mizizi ndani ya Taifa letu na kuleta kichefuchefu katika kuimarisha maadili ya kazi na maadili ya uongozi. Kwa msingi huu tunarudi pale pale kuwa “Kujiuzulu siyo utatuzi wa tatizo”,

Pamoja na kauli ya waziri wa uchukuzi wa jamuhuri ya Muungano mheshimiwa Dk Mwakyembe kuhusu ajali kuwa “Watanzania hawana sababu ya kumtafuta mchawi wa ajali hiyo kwani imetokea kwa bahati mbaya… Tukubali kwamba ajali hii ni bahati mbaya. Maofisa wetu wametuthibitishia bila kuwa na shaka kwamba meli ilikuwa nzima na haikuzidisha abiria, kujiuzulu siyo suluhisho, tushikamane katika kipindi hiki kigumu.”

Lakini je anakubali kuwa meli hiyo ilikuwa sio chakavu na kama kiongozi wa ngazi ya juu anatoa ushauri kuwa ilikuwa sahihi kwa taifa kutumia meli ambayo ilishasimamishwa kufanya kazi huko marekani? Na hivyo usajili wake ulukuwa sahihi? Na kama hivi ndivyo kwa nini Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeisimamisha meli pacha nyingine ambayo haikuhusika na ajali?

Nakubaliana sana na maelezo ya  Kepteni Magamba alisema kuwa anayepaswa kulaumiwa katika ajali hiyo ni kiongozi wa safari za meli. Kiongozi huyo (Port State Controller) hupokea taarifa kutoka mamlaka ya hali ya hewa na kuruhusu meli iondoke au isiondoke. Kiongozi huyo husimamia usalama wa meli ndani na nje ya bahari kwa kushirikiana na eneo meli inapoelekea. “Meli kabla ya kuondoka lazima ifuate taratibu zote, nahodha hupata kibali kutoka Sumatra (clearance) na kuipeleka kwa ‘Port State Controller’ ambaye tayari anakuwa ameshapata taarifa za hali ya hewa,” alisema Magamba.

KWA NINI KAMA TAIFA BADO TUKO KWENYE MFUMO MBOVU WA UWAJIBIKAJI?

Kama alivyowahi sema Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba aliitaka Serikali kuangalia upya uwajibikaji, utendaji na mwenendo wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) akidai kuwa taasisi hiyo imeshindwa kuwajibika ipasavyo kudhibiti vyombo vya usafiri.

Mwenyekiti wa APPT Maendeleo, Peter Mziray alisema: “Lipo tatizo katika uingizaji, ukaguzi na usajili wa vyombo vya usafirishaji wa majini… Serikali na mamlaka zinazohusika na usajili hazifanyi kazi kwa kuzingatia umuhimu wa kazi waliyopewa na matokeo yake ndiyo kuruhusu vyombo vibovu kubeba roho za watu.”


Lazima tukubali kuwa tuko katika mfumo mbovu wa uendeshaji wa shughuli za serikali mfumo mzima ni mbovu (the whole system is dysfunctional). Na kama tukigundua hivi kama taifa tutakuwa tumefanikiwa kuondoa tatizo la utendaji katika shughuli za serikali. Mimi binafsi bado nafikiri kuwa watendaji wetu wakuwa kwa namna moja au nyingine wanatakiwa kuwa kama Marehemu Park Rais  wa Korea ya Kusini ambaye alikuwa anahakikisha kuwa watumishi wote ambao wamepewa dhamana lazima watekeleze wajibu wao na kama wakishindwa wanawajibishwa mara moja. Mfano mwingine tusiende mbali wanatakiwa kuwa kama Marehemu Baba Wa Taifa Julius Nyerere au Marehemu Sokoine ambao walikuwa hawana mchezo na maadili ya watumishi ambao wako chini yao; tukiiga mifano yao tunaweza kama taifa kubadilisha kabisa mfumo wa uwajibikaji.




Viongozi wetu wengi hivi sasa uwajibikaji wao ni wa maneno tu, ni mahodari wa kusema lakini ni wabovu wa vitendo kwa kiasi kikubwa. Kama alivyo wahi sema baba wa Taifa Hayati mwalimu Nyerere kuwa kwa nchi ili iweze kuendelea inahitaji: Ardhi, siasa safi na uongozi bora; hivi vitatu vikikamilika tunazungumzia uwajibikaji wa kweli na sio wa kuoneana aibu; kwa sasa taifa letu au linakosa viwili kati ya hivyo vitatu na mafanikio yetu yanabaki kuwa ngonjera;

Kama tutafanikiwa kubadilisha mfumo wa utawala na usimamizi wa shughuli za kila siku za serikali hata inapotokea kiongozi ambaye amepewa dhamana anawajibishwa italeta tofauti ya uwajibikaji; kwa hivi sasa kijiuzuru kwa viongozi wetu inabakia katika nadharia ya siasa zaidi ambayo bado haibadilishi mwelekeo wa uwajibikaji wa kweli;


Nafikiri ni wakati muafaka kwa viongozi wetu wa juu 
kufikira zaidi jinsi ya kurekebisha mfumo wa uendeshaji wa serikali kwa manufaa ya wananchi wake.

MUNGU IBARIKI TANZANIA

1 comment:

  1. nakubaliana na mawazo yako kwa hivi sasa tanzania inahitaji viongozi walio komaa kimaadili, kwani ukiwa unajua wajibu wako hasa kwenye dhamana ambayo unayo na kuto kuoneana haya na kubebana kisiasa na fikra za kukosa kura wakati wa uchaguzi tutaifikisha nchi yetu kwenye nchi ya ahadi iliyojaa maziwa na asli kwa wananchi ambao wengi ni wanyonge hata hawajui kesho watakula nini.

    ReplyDelete