WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 28, 2012

UADILIFU NA UWAJIBIKAJI NI SILAHA PEKEE YA AMANI YETU



Kikwazo kukubwa sana cha uadilifu na uwajibikaji ni matumizi mabaya ya ofisi kwa masilahi ambayo hayagusi maisha ya wananchi, rushwa na matumizi mabaya ya pesa ni miongoni mwa malalamiko makubwa katika hoja hii.



Rushwa ni miongoni mwa matatizo yanayoikabili dunia nzima kwa ujumla. Mataifa mengi yamekuwa yakipambana na tatizo la rushwa ingawa nchi zinatofautiana katika viwango vya rushwa. Tatizo la rushwa linaigusa jamii katika viwango tofauti na katika mazingira tofauti. Rushwa na matumizi mabaya ya ofisi yako katika viwango vyote vya maisha ya binadamu. Kwa sasa taifa letu linaangalia sana rushwa katika ngazi ya viongozi wakubwa na waandamizi wa serikali ambao kwa kiasi kikubwa ndio wanaoongoza na kutegemewa sana kwa kuwaletea wananchi maisha bora.

Serikali ya Tanzania  imekuwa ikichukua hatua mbalimbali katika kupambana na hali hii mara baada ya Uhuru mwaka 1961 ni:- Mwaka 1966 Serikali iliunda Tume ya Kudumu ya Uchunguzi ikiwa na lengo la kuhakikisha viongozi wa Serikali hawatumii vibaya madaraka waliyokabidhiwa na umma kwa manufaa yao binafsi. Mwaka 1971, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga Sheria ya Kuzuia Rushwa Na.16/1971. Kutungwa kwa sheria hii kulifuatiwa na kuundwa kwa Kikosi cha Kuzuia Rushwa mwaka 1975, ili kuimarisha zaidi mapambano dhidi ya rushwa, Bunge iliifanyia marekebisho Sheria ya Kuzuia Rushwa Na. 16 ya 1971, mwaka 1991 ikaundwa Taasisi ya Kuzuia Rushwa kwa lengo la kuzuia vitendo vya rushwa. Mwaka 2007 baada ya kutungwa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na 11/2007 na kufutwa Sheria ya Kuzuia Rushwa Na. 16/1971 jina la taasisi lilibadilika na kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Hivyo TAKUKURU ilianzishwa rasmi Julai, 2007 na kurithi kazi zilizokuwa zinafanywa na chombo hiki kwa majina ya awali.”




Pamoja na upango huu mzuri wa serikali katika maandishi na katika kimantiki tatizo liko wapi kwa vilio vya wananchi kuhusu matumizi mabaya ya ofisi za viongozi wetu waandamizi? Je mazingira haya mazuri ya sheria ya kumlinda mwananchi na mali zake ni sawa na uamuzi ambao hauna usiammiaji mzuri?

Je tatizo ni serikali au usimamiaji wa sheria husika? 

Je ofisi husika hazina meno ya kutosha kutenda kazi?

Au ni tatizo la kulindana sana kwa masilahi binafsi?

Tatizo ni watu  au mfumo uliopo ambao unatoa fursa kwa viongozi na watendaji kuwajibika kwa waliowateua


Watanzania wengi leo hii wanajiuliza hivi taifa hili sasa linao viongozi wanaojua wanatakiwa kufanya nini?

Au vyeo ambavyo watu wanavyo wamepeana tu kwa “ MUHALI” na kwa msingi huu haiwasumbui nini kinachoendelea  hivyo hawawajibiki  kwenye nafasi katika kuwasaidia Watanzania.

Hoja na matukio ya kujikanganya kutoka watendaji serikali waandamizi mawaziri na manaibu mawaziri pamoja na repoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali  kama waandishi wengine walivyowahi andika na kuelezea huko nyuma linalifikisha taifa katika ombwe la uongozi.

Ukiwa na chombo baharini kinapita katika dhoruba kali, halafu nahodha na mabaharia wanajshughulisha na mambo mengine lile la hatari lililoko mbele yao hawalijali, chombo hicho ni lazima kiseree na kupotelea majini”.


Viongozi wetu wanapaswa kujifunza  katika nchi za wenzetu kasoro zinapojitokeza katika wizara yako kama tuhuma hizo ni za kweli au la wajibika kwanza kupisha uchunguzi huru wa tuhuma hizo kwa vile wewe mwenyewe umeshindwa kuwajibika na umekaribisha zengwe hivyo wajibika.

Uwajibikaji wa viongozi wetu ni tatizo nakumbua Raisi Mstaafu Mkapa aliwahi waita mawaziri ni sawa na "askari wa miavuli"; siamini mawaziri wetu ni askari wa miavuli hawaziwezi dhoruma za angani pengine hawana ustadi wa kuruka kwa kutumia miavuli wao; askari wa miavuli lazima ajue utaratibu mzima wa kutumia huo mwavuli ukikosea tu unakupeleka ndiko siko wengi wnaishia huko.

Nafikiri zile kongamano ambazo serikali imekuwa ikiwafanyia kuwanoa ubongo hazijawa effective kwa mawaziri wote kwani wengi wanalalamikiwa kwa utendaji wa uwajibikaji wa chini ya kiwango.

Kipimo kimoja kikubwa cha uongozi bora ni uwezo wa kusimamia rasilimali za wananchi, uadilifu, uwajibikaji, uzalendo na kumcha Mungu; kiongozi akiwa na vitu hivi huzaa hekima ua uwajibikaji wa kweli na uzalendo wa kupenda nchi yako na kusimamia rasilimali zake kwa faida ya Taifa.
Inaoneka kuwa  baadhi ya viongozi wetu kutumia nguvu zao  sio kuondoa umasikini bali kuongeza umasikini kwa mtanzania wa kawaida.

Kweli naamini madaraka matamu, watu wanayatafuta kwa gharama pengine ili kukizi masilahi binafsi, ndio yanafuata masilahi ya taifa.

Amani yetu ambayo tunamshukuru Mungu kwa zawadi hii pekee kwa ambayo watanzania wamejaliwa kwa misingi mizuri ya waasisi wetu Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Maheremu Mzee wetu Abeid Aman Karume kwa uadilifu wao na mapenzi yao kwa taifa la Tanzania, tusipikuwa makini tuaipoteza kutoka na baadhi ya viongozi wa sasa ambao wanatumia vyeo na madaraka kwa masilahi binafsi ambayo inajenga chuki miongoni mwa wananchi.


Changamoto ya amani yetu ni kwa watendaji wote wa serikali hasa 
watendaji waandamizi kuwa wakweli ili waweze kusikia  sauti ya wanyonge,  na kupitia rasilimali za taifa wasaidie katika kujenga jamii inayozingatia na kuheshimu haki msingi za binadamu. Kashafa ufisadi, rushwa, uzembe na kutowajibika mesomo hii tuweze kuipunguza katika midomo ya wananchi na katika maandiko yetu. Hilo linawezekana kama viongozi wetu watakuwa wakweli  kulingana na viapo vyao kabla ya kuingia katika ofisi husika. Kwa kufanya hivyo tutaweza kuondoa ombwe la uongozi.

1 comment:

  1. tunahitaji tanzania ambayo iko tayari kwa mabadiliko kutoka hasa kwa viongozi wetu , viongozi wasifanye Tanzania yetu kuwa shamba la bibi. tumechoka tumechoka

    ReplyDelete