WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 21, 2012

JE WATANZANIA TUMEKUWA NI WATU WA KUOGOPA MABADILIKO?


Maggig Mjengwa aliwahi andika huko nyuma kuwa “Watanzania leo tumekuwa ni watu wa kulalamika tu hata kwa yale ambayo kimsingi ni wajibu wetu wananchi kuyafanya. Kwa tunavyoenenda, hata aje malaika kutuongoza, bado naye atapatwa na  wakati mgumu”.
Ninapata wakati mgumu sana kutafakari na kuielewa dhana hii, je tumeingiliwa na mdudu wa aina gani katika fikara zetu na katika maisha yetu ya kila siku? Kama ni kweli hii ina maana kuwa tunatawaliwa na maisha ambayo hayana matumaini.
Swali ambalo je woga huu wa mabadiliko ni kwa watanzania wa kawaida tu au hata viongozi wetu? Je ndugu yangu mjengwa alikuwa ameyaongelea mabadiliko gani? Ilinifikirisha zaidi pale aliposema hivi “Tumekuwa kama watu wa taifa la kusadikika ... “Wasadikika wana desturi ya kutafuta fimbo baada ya kuumwa na nyoka… Tumekwisha umwa na nyoka wa  matendo yetu mabaya ya zamani”.

Kumbe woga wetu wa mabadiliko unatokana na kutokujiamini kwetu kwa sababu ya matendo yetu mabaya. Ni matendo gani ambayo yanatupa sisi wananchi wa Tanzania wakati  mgumu wa kuamua kubadilika?
Jambo hili la mabadiliko ya matendo yetu nakubaliana nawe kuwa kwa kweli lazima itamfanya mtu kuogopa mabadiliko kwa kufikiria masilahi binafisi kwani akifanya mabadiliko yanaweza kumweka katika wakati mgumu. Mara nyingi maba

Uadilifu na uaminifu. Kwamba mtu ukiamua kuisimamia “ndiyo”, basi aisimamie bila kutetereka, na akiamua kuisimamia “siyo” vile vile aisimamie bila kuyumba. Na kwamba mtu akiisimamia “ndiyo” ukijua kwamba ni “siyo” ni unafiki na uovu. Vilevile akiisimamia “siyo” ukijua kwamba ni “ndiyo” ni unafiki na uovu!
Mtu mwenye msimamo, uadilifu na uaminifu daima anakuwa mbali na unafiki na uovu. maana ina msingi chanya wa kuendesha maisha katika jamii yoyote ile.

Jamii fulani na kuishi akizungukwa na historia, utamaduni na desturi za watu wake. Privatusi karugendo aliwahi kuandika katika moja ya makala zake kuwa “Katika familia zetu, katika jamii zetu na katika taifa letu, tunahitaji msimamo, uadilifu na uaminifu. Hatuwezi kujenga familia, jamii na taifa imara bila kuwa mbali na unafiki na uovu. Bila kujenga utamaduni wa “ndiyo” kuwa ni “ndiyo na “siyo”  kuwa ni “siyo”, hatuwezi kupiga hatua ya maendeleo bila kuizingatia falsafa hii”. Kwa msingi huu kuwa ni kweli kuwa bado tunakazi kubwa kuyakubali mabadiliko kutokana na ualisia wa maisha yetu na jamii inayotuzunguka.



Je woga wa kuogopa mabadiliko unatokana na sisi kama taifa kuwa waoga wa kufikiri? Au ni uvivu wa kusoma na kujua nini kinaendelea ndani ja jamii yetu. Lakini katika hili la kutokukubali mabadiliko linanipa wakati mgumu sana pale ninapoona na kuelewa kuwa hata waandishi wetu wa habari “ media crew” pale wanaposhindwa kuhimili wimbi hili ukizingatia kuwa wao ndio walitakiwa kuwa viongozi wa kuwaelimisha watu kuhusu namna na mbinu za kuyakubali mabadiliko,

Katika siku za karibuni kumekuwa na malalamiko ya wanahabari kuegemea jamii Fulani na kuisaidia iendelee kuogopa mabadiliko; lazima tufike mahali tuweze kuiambia jamii yetu kuwa umesahau kuvaa nguo.Kutokana na jamii inayotuzunguka hakuna mtoto mwenye ujasili ambaye atamwambia mama yake leo “ mama angalia mfalme hajevaa nguo” kwani hata watoto wetu wadogo wameshaambukizwa woga wa kuogoma mbabadiliko;

Tatizo hata wasomi wetu katika hoja zao hata kwenye forum zinaonyesha kuwa  “wakati mwingine” zinaogopa mabadiliko hivyo wataendelea kungangania au kushabikia hoja Fulani za mtu au kikundi Fulani cha watu hata kama mwisho wa siku hazina mwelekeo wa mabadiliko ambayo yatalisaida taifa katika mabadiliko na maendeleo ya jamii.
Kama mwandishi mmoja alivyowahi kuandika kuwa             “jamii imeshatambua kwamba mito,maziwa,bahari,mabwawa,madini, ardhi ni vyanzo vya kuletea maendeleo kwa jamii yao lakini jamii hiyo haitumii rasirimali hizo kujiletea maendeleo, basi tatizo ni udhaifu wa kufikiri uliomo kwenye jamii husika”.



Taifa letu kwa sasa kiuhalisia liko kwenye mtikisiko mkubwa sana kuanzia kwenye maadili ya kijamii hadi kwenye nyanja kuu ya siasa. Mtikisiko huu kwa kiasi kikubwa unasababishwa na kukosekana kwa misingi sahihi ya wapi jamii yetu inaelekea. Pamoja na hilo hata watendaji wetu katika nyadhifa mbalimbali wamekuwa na ufinyu na mwelekeo wa ubinafsi zaidi na utumiaji wa madaraka kwa manufaa binafsi na hawako tayari kuwajibika na kukiri kuwa wamekosea. Daima wanajiona nje ya mzingo wa matatizo haya yanayoikabili jamii yetu,hivyo wanafanya hujuma kwa kudhani wao wako sehemu salama,Lakini hali halisi inaonesha wanajidangaya. Wanasafiria katika chombo kwa nje wao wenyewe wanakiona kuwa ni salama sana lakini wamesahau kuwa “Taifa ni kama chombo cha safari baharini,kikizama hakuna kinachosalia, wakati mwingine hata waogeleaji hodari na mahiri hunaswa na wadudu bahari”.

Taifa letu kwa hivi sasa limekumbwa na tatizo na  viongozi wetu ambao wamepewa dhamana ya kuongoza idara za serikali kwa kushindwa kuishi kulingana na viapo vyao vya kazi na kuishia kuwa ni sehemu ya Ufisadi amboo unatafuna nchi yetu. Katika mjadala huu mkuu na mzito ambao baadhi ya wabunge wamekasirishwa na tabia hizi za hawa watendaji wakuu na kuwataka wajiudhuru, kwa kukiuka maadili ya uongozi “matumizi mbaya ya pesa za walipa kodi” kama mbunge wa Njombe alivyosema Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM)



Hili likifanikiwa tutakuwa tumeanza kuondoa woga wa mabadiliko, kama mawaziri watajitafakari kuwa ni mchwa na wamekosa maadili yamekumbwa na wimbi la rushwa basin a wakaamua kujiuzuru hata kama wataona wanaonewa lakini wakaamua kukaa pembeni ili uchunguzi ufanyiki itakuwa ni dalili njema ya mabadiliko.
Wasipowajibika bunge linataka kumuwajibisha Mtoto wa Mkulima “ waziri Mkuu Mheshimiwa  Pinda atawajibishwa na bunge kama taratibu zitatimia.  

Je kweli tatizo ni Waziri Mkuu? Au Tatizo ni jamii ambayo imetulea? Je tatizo kulipa fadhila baadaya uchaguzi kwa wale waliotoa msaada? Au tatizo na ukosekanaji wa Maadili ya uongozi kwa watendaji wetu? Au tatizo ni viongozi wetu kuto mwanini Mungu hivyo kukosa kabisa ubinadamu? Je tatizo ni umasikini wa viongozi wetu kabla ya kuingia madarakani hatima ya uroho na ulafi wanaishi kuwa mafisadi?

Nini hasa tatizo letu na kuogopa mabadiliko? Chama kingine kikishika madaraka nitafungwa au kunyogwa? Je jibu la maswali haya ni lipi?


Nafikiri ujasiri utatusaidia sisi kuweza kufanya maamuzi sahihi ya mabadiliko; hivyo tunamwomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kuwa MKALI katika utendaji wake na kama mheshimiwa Pinda  atapigiwa kura naungana na Maggig Mjengwa kuwa “kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda”.

No comments:

Post a Comment