WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, April 1, 2012

"KUDADADEKI" NA UCHAGUZI MDOGO ARUMERU YA MASHARIKI


TUMEJIFUNZA NINI KUTOKANA NA UCHAGUZI MDOGO ARUMERU MASHARIKI?


  • Siasa zisizo na mvuto wa maendeleo ya kuwakomboa watanzania;

  •  siasa za kupakana matope badala ya kunadi sera za kuwakomboa watanzania.

  • Kampeni zilizojaa matusi au maneno yasiyofaa kwa tija ya maendeleo ya mtanzania

  • Malumbano, vijembe, matusi na kashfa kati yamiongoni mwa vyama vinavyoshiriki.

  • Tumeona aina ya viongozi wabunge ambao tunawategeme watuvushe kwenye maisha bora na kutujengea mazingira ya maisha bora katika karne ya teknolojia na sayansi kwa mwendo huu ni ndoto kufika huko.

KAMPENI NI NINI?

Kwa kifupi, Kampeni zilianza zamani. Katika vitabu tumesoma kuwa zilianza enzi za wanafalsafa mahiri duniani Socrates na wenzake.

Wakati huo ilikuwa ni njia mbadala ya kumwondoa madarakati kiongozi asiyefaa.

Katika Tanzania yetu tunaweza kujifunza jinsi Mwalimu Nyerere alivyofanya kampeni ya kudai uhuru kwa kuunganisha nguvu za watanzania wote kuonyesha na kuwashawishi wananchi wazawa kukubali kuwa mkoloni mtawala wa wakati huu alikuwahafai kwa maendeleo yetu na kwa uhuru wetu. Kwa mtazamo chanya hizo zilikuwa kampeni kwa vile zilihusisha kuwashawishi wananchi kuunga mkono juhudi za wapigania uhuru kumwondoa mkoloni. 

Kampeni kama wengi walivyowahi sema ni wakati ambao vyama vinavyowania uongozi katika ngazi yeyote ile vinatakiwa kunadi sera za vyama vyao kwa ajili ya maendelo ya mwananchi wa kawaida; kwa maneno mengine ni fursa njema kueneza sera bora za Kujinadi kunajumuisha kutaja sifa zako na uwezo wako kwa nini utakuwa kiongozi bora kuliko mpinzani wako na hivyo unastahili kura zao


Kujinadi pia kunajumuisha kutaja mapungufu ya mpinzani wako kwa nini hana sifa ya kuwa kiongozi bora na hivyo hastahili kura yao.

Busara ya kawaida inatueleza kuwa watu wanahitaji taarifa za msingi kuhusiana na msimamo na sera za mgombea. Wanahitaji kampeni yenye taarifa nyingi za kuelewesha kwa kina masuala muhimu yanayogusa vipaumbele na kero zao.

Tatizo ni nini? Kwa nini kama taifa tunaendlea na kampeni chafu kila wakati?

Vyama vingi vya siasa vinafikiria kuwa siasa chafu matusi ni tiketi bora ya ushindi; vyame vingi vya siasa ushindani wao wanajipima kwa kupiga kampeni chafu badala ya kueneza sera na kuwaacha wananchi wapime.

Viongozi wengi wa vyama wanashindwa kujenga hoja za kweli kuhusu mapungufu ya chama kingine; wanakosa vielelezo vya hoja zao; namna gani atatekeleza ahadi za kumkwamua mwananchi wa kawaida na kivipi anaona  mapungufu ya kiutekelezaji na uwezo mdogo wa kiongozi anayeshindana naye?

kampeni nyingi zinazofanyika ni si za kupata viongozi bora bali bora viongozi.  Uthibitisho wa hoja hii kampeni hazizingatii maadili, na uadilifu wa kiongozi mtarajiwa maana yake mtu yeyote anaweza kuwa kiongozi.


Je nini tumejifunza katika Mwelekeo wa kampeni Arumeru Mashariki?

Jambo la kwanza linalosikitisha kwa wengi walioshiriki kufanya kampeni ni  vyama ambavyo vinadadi wagombea wake ktutumia muda mwingi sio katika kunadi sera zenye tija kwa wananchi wa Arumeru bali vinatumia na kupoteza muda mwingi kuendeleza malumbano yasiyo na maana, na kwa msingi huu ni kumnyima haki ya msingi ya kujua na kutafakari sera ambazo angeweza kuziona pengine zitaweza kufaa katika kumsaidia kumletea maendeleo. Katika hilo kwa kweli tunahitaji viongozi ambao wangekuwa (great thinkers) kwa maendeleo ya wananchi sio viongozi ambao wanaweza kusimama kwenye jukwaa na kudadi maneno kama “kudadadeki”


Vyama vya siasa nchini vinashindwa kuelewa kuwa siasa sio ugomvi wala sio vita, siasa ni nguvu ya hoja; siasa ni mchezo wa masumbwi na unatakiwa ufuate sheria za mchezo na sio kucheza kinyume cha utaratibu. Na jambo moja kubwa katika siasa ni mchezo ambao unafanyika chini ya demokrasia. Kinachoendelea Arumeru mashariki sijui ni democrasia gani inatumika, iliyokosa maadali ya kunadi sera: 

Kampeni za matusi zinajenga misingi ya  vurugu na mwisho wa siku kura zitapigwa sio kwa kupima sera bali upenzi wa vyama kitu ambacho kama tutakuwa wakweli kinarudisha nyuma maisha bora kwa kila mtu: je hilo ndilo tunalolitamani liendelee katika nchi yetu?

Kisiasa, kampeni ni jitihada au mpangilio maalumu unaofanywa na chama au vyama kwa lengo la kushawishi mchakato wa utoaji maamuzi katika kundi fulani. Katika nchi zinazofuata mifumo ya kidemokrasia, kampeni za kisiasa mara nyingi humaanisha kampeni za uchaguzi.

Je ni chombo gani kinachosimamia maadili ya kampeni wakati wa chaguzi?

Je ni kweli kuwa chaguzi zetu zimetawaliwa na hujuma na chama chenye nguvu ndicho daima kinachoshinda?

Je ni kweli kuwa wakati wa chaguzi hakuna uwanja sawa wa kisiasa kutoka kwa vyombo vya kusimamia na kuratibu uchaguzi?
Ndipo tunapofika kwenye hoja ya msingi na kufikiria kuwa utawala wa sheria katika chaguzi ni dhaifu na:

Je vyombo hivyo havina meno binafsi na haviko huru vya kutosha?
Kwani tunasikia malalamiko daima kuwa chaguzi zinatawaliwa na rushwa na hujuma nyingine miongoni mwa vyama husika?
Je tume ya uchaguzi na msajili wa vyama wanawezaje kuimarisha demokrasia ya kweli katika kufanikisha kampeni huru na zenye tija kwa wananchi?

Tukururu inawajibikaje katika mazingira haya ina msaada wowote au inaangalia upepo unavyovuma?

WAJIBU WA MWANANCHI WA KAWAIDA KATIKA KIPINDI HIKI NI NINI?

Nafikiri kama nilivyowahi kuandika katika moja ya makala yangu wananchi wanahitaji sana elimu ya uraia, ili waweze  kuepuka hujuma na sera uchwara zinazotolewa na wanasiasa kwa faida zao binafsi nakuwa na uwezo wa  kuzidhibiti kampeni za matusi na sinazoweza kuhatarisha amani ya nchi.


Elimu ya uraia itawasaidia kuwajengea wananchi uwezo wa maamuzi na kwa uwezo huu wananchi watakuwa na nguvu na kuwashikisha adabu wanasiasa uchwara wasio na hoja, ili vyama vinapokuja kwenye uchaguzi vijipange.  Ndio maana wakati mwingine naashiria kusema kuwa hata kinachoendelea bungeni wakati mwingine chimboko lake ni hili wanasiasa wetu wanakosa hoja za nguvu za kumkwamua mwananchi hawajipangi sawa sawa ni sawa na hoja zinazo kurupushwa kutoka usingizini. 

Je makapeni manager vya vyama wanakazi gani katika kuhakikisha kuwa wanadadi sera zinazotakiwa?

Katika kampeni nyingi nafikiri wamekuwa wakifanya kazi za uenezi zaidi na sio kuvisaidia vyama vyao katika ushindani wa hoja nzuri na nzito nz zenye mvuto wakati wote wa kampeni;

Kampeni manager ndio dira ya kutumainiwa katika chaguzi yeyote; ni viongozi ambao wanatakiwa watembee mbele zaidi kimawazo, kifikra na kimwelekeo; wao ndio marubani wa ushindi;

Katika nchi za wenzetu kutokana na ushindani wa hoja makapeni manager wanakuwa makini ukiaukwaji wa maadili, lugha za matusi automatically zitamwajibisha kichama na kuachia nafasi yake yenye heshima kubwa;


Tumeona katika chaguzi zetu nao hushindwa kuzuiaa na kuratibu mchakato mzuri unaofaa wa uelezaaji wa sera bora kwa jamii.
Kampeni yaweza kuwa ni kuwaelezea wananchi mambo utakayowafanyia na namna utakavyotekeleza. Hii ni pamoja na kueleza ilani yavyama vyao, vipaumbele vyao, huduma za afya na utakavyokomesha rushwa na maisha bora kwa mtanzania

Makapeni Manager wa vyama “Pengine” wanafikiria zaidi kuwa  kuzungumzia mabaya ya wenzao badala ya sera ndiyo kufanikisha mchakato mzuri na utakaowezewsha chama chao katika mbio za uchaguzi ambao unaoshindaniwa.   

KAMA TAIFA NINI KIFANYIKE KUEPUSHA HALI KAMA HII KUENDELEA KUJITOKEZA TENA NA TENA?

Kwa ujumla, suala hili la kampeni linahitaji msukumo mkubwa na labda mapinduzi fulani kwa sababu hivi sasa Watanzania hawamchagui kiongozi wala chama kwa sababu ya sera zake au uchapakazi wake bali wanafuata ushabiki tu. Kwa msingi huu wananchi watendelea kubariki na kushangilia matusi kwa vile tu yanakikashifu chama na watendaji wa chama tofauti hata kama hakutakuwa na tija yeyote katika maisha yao, kama Mheshimiwa waziri Mkuu mstaafu Jaji
Warioba alivyowahi sema kuwa “Siasa nyingine zinajenga chuki, siasa za kinafiki siwezi kuziunga mkono, tufikie wakati tutofautishe mambo binafsi na mambo ya umma,”
Kama taifa hakuna kisichowezekana katika kuleta mageuzi ya kweli ya kufanya kampeni za kiustaarabu, zenye maadili na zenye tija kwa Taifa tuwe  wazalendo wa kweli kukubali kuwa tunaweza kufanya kampeni ambazo hazitahusisha matusi, BALI KAMPENI ZILIZOJAA NGUVU YA HOJA NA USHINDANI WA KWELI KWA MAENDELEO YA TAIFA.

1 comment:

  1. bravo men nimeipenda hii kazi na uchambuzi stahiki, ni kweli kama taifa tunahitaji kubadilika kwa maendeleo ya Taifa na sio kikundi kidogo cha watu. keep it up

    ReplyDelete