WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 14, 2012

JAJI MSTAAFU JOSEPH SINDE WORIOBA NA JAHAZI HILI UTALIVUSHA SALAMA?


TUME YA KURATIBU KATIBA MPYA YAAPISHWA RASMI NA MHESHIMIWA Dr. JAKAYA MRISHO KIKWETE.


Safari ya mchakato wa katiba mpya yanazidi kuendelea vizuri, baada ya tume ambayo ilikuwa imetangazwa na Rais wa Jamuhuri ya Tanzania kukamilisha viapo vyao na kukabidhiwa dhana rasmi za kazi zao.

Kama ilivyowekwa bayana na Rais Jakaya Kikwete akiunda Tume ya Katiba ambayo ndiyo itakayoratibu maoni ya wananchi kasha kuyapeleka kwenye Bunge la Katiba.


Wajumbe hao wa tume ya mabadiliko ya Katiba walioapishwa na Rais Kikwete ni pamoja na Mwenyekiti wake Jaji mstaafu Joseph Warioba, Makamu Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji mstaafu Augustino Ramkadhani pamoja na wajumbe wake ambao ni Profesa Mwesiga Baregu, Riziki Shahari Mngwali, Dk. Sengodo Mvungi, Richard Lyimo , John Nkolo, Alhaj Said EL- Maamry, Jesca Mkuchu, na Profesa Palamagamba Kabudi. Wengine ni Humphrey Polepole, Yahya Msulwa, Esther Mkwizu, Maria Kasonda, Al-Shaymaa Kwegyir na Mwantumu Malale pamoja na Joseph Butiku.

Wengine ni Dk.Salim Ahmed Salim, Fatma Said Ali, Omar Sheha Mussa, Raya Suleiman Hamad, Awadh Ali Said, Ussi Khamis Haji, Salma Maoulid, Nassor Khamis Mohammed, Simai Mohamed Said, Muhammed Yussuf Mshamba, Kibibi Mwinyi Hassan, Suleiman Omar Ali, Salama Kombo Ahmed, Abubakar Mohammed Ali, Ally Abdullah Ally Saleh. Pamoja na Katibu wa tume hiyo Assaa Ahmad Rashid na Naibu Katibu wake Casmir Sumba Kyuki.


Macho ya watanzania kwa sasa yanaelekezwa kwao, katika kuivusha salama Tanzania katika kulipatia taifa katiba Bora itakoyoweza kudumu kwa kipindi kirefu bila malalamiko, kwa msingi huu naungana na wanahabari wengine walio wahi kuandika kuwa “Sina shaka na Jaji Warioba hasa kutokana na uzoefu wake katika masuala ya sheria na utendaji wake katika tume kama hizo”.
Kama mheshimiwa Rais Kikwete, alivyosema “pamoja na kazi hiyo wamewataka Watanzania kutambua kuwa kazi ya tume hiyo ni kuratibu maoni ya Katiba mpya, na sio ya kujadili kuwepo au kutokuwepo Muungano ila ni mchakato wa kupata katiba bora itakayoendesha Taifa la Tanzania. Itafanya kazi ya kukusanya maoni kuhusu katiba na maslahi ya Wananchi wa pande mbili zinazounda muungano”.

  • “Kuzinduliwa rasmi kwa tume hii ya kuratibu maoni ya kupata katiba mpya ya nchi ni ishara tosha ya Taifa letu kuingilia katika historia iliyotukuka kwa kuanza safari mpya ya kuelekea kuzaliwa kwa Katiba mpya itakayotokana na maoni ya Watanzania wenyewe”.


  • “Mwalimu Julius K. Nyerere, alisema mawazo hayapingwi kwa rungu bali hujibiwa kwa mawazon yaliyobora zaidi. Ni vema mtambue kuhamaki si jibu ila jambo jema ni kutoa mawazo yako yaliyobora zaidi. Kama Watanzania tutaifanya kazi hii kwa moyo tutafanikiwa kupata katiba iliyo bora itakalolilea Taifa letu katika miaka 50 ijayo,”


JUKUMU LA WANANISHI NI LIPI?

  • Kuhakikisha kuwa kila mmoja kwa uwingi wetu tuhakikishe tunatoa maoni kwa faida ya vizazi vyetu;


  • Huu sio wakati wa kununuliwa na wana siasa katika ushawishi usio na faida kwa jamii ya Mtanzania


  • Tuhakikishe kuwa maoni yetu yanasikika na yanatekelezwa Kama tume haitafanikiwa kuwafikia huko mliko msibweteke tafuteni njia mbadala wa kuhakikisha kuwa maoni yenu yanasikia.


KAZI YA TUME  NI IPI

  • Kazi ya tume ni moja tu kufanya kazi hii katika maadili ya kweli bila upendeleo wa chama Fulani cha siasa au kikundi Fulani chenye uwezo au matakwa ya dini Fulani; tume iwatumikie wananchi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.


JUKUMU LA VYAMA VYA SIASA

  • Wakati huu wa mchakato wa kuratibu maoni vyama vya siasa vijitahidi kuacha kuwachanganya wananchi kwa kuwachakachua kimawazo ili kuhari au kudhoofisha nia njema ambayo iko ndani ya utaratibu mzima;


  • Vyama vya siasa viwahamasihe wanachama wao katika kujumuika kutoa maoni na kuwaelimisha zaidi umuhimu wa kuchangia katika kutoa maoni.


  • Ni matumaini yangu kuwa tume itaweza kukusanya maoni kwa kwa mapana na kwa uwezo wa hali ya juu kutoka na jinsi tume hiyo ilivyoundwa na umahili na uzoefu wa wajumbe wa tume hiyo.


MUNGU IBARIKI TANZANIA NA IWEZESHE KUPATA KATIBA BORA KWA MAENDELEO YA WANANCHI WAKE

No comments:

Post a Comment