WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, December 17, 2011

VITA YA VIJANA DHIDI YA WAZEE KATIKA UONGOZI WA NCHI


Kwa nini tunahitaji uongozi wa vijana sasa?


·        Je Ni kweli kuwa vijana ndio nguzo na uhai wa chama chochote kiwacho?

·        Je ni kweli  kuwa  Vijana wanafaa kutumikia taifa lao kwa ajili ya nguvu walizo nazo zaidi hata kama hawana elimu ya kutosha ya uongozi?

·  Je vijana wanaelewa matatizo ya vijana wenzao  na wataweza kuwasaidia  haraka katika kujinasua katika atope zito la maisha magumu pindi wapatapo nafasi ya uongozi?
Kwani nini wazee hawafai kwa sasa?



·  Hivi sasa wazee ndio chimbuko la matatizo ndani ya vyetu vya siasa?

·        wazee  kwa wakati huu  wamechoka kuongoza chama kwa umri wao na mawazo yao mgando?

·        wazee hawaoni wala hawasikii hoja zote vizuri;

·        wazee ni wazito kufanya maamuzi;

·        wazee wana huruma kupita kiasi

hoja ya wazee dhidi ya uongozi wa vijana




·     Ni kweli kuwa vijana hawana uwezo kuongoza siasa za nchi zetu?

·     ni kweli kuwa vijana hawana hekima ya kutosha katika kufanya maamuzi makubwa ya kitaifa.

· vijana wana nmatatizo bado ya kuongelea integrity (uadilifu) wa utendaji wa vyama vyao kwani wengi bado wamejiegemeza kwa kundi fulani;


· Ni ukweli kuwa maamuzi mengi ya vijana yana mwelekeo wa jazba na uharaka usio na maana?




· Ni kweli kuwa vijana wote  wanaoingizwa katika shughuli za siasa  na kushiriki katika ngazi za maamuzi, lazima wawe na back-up ya nguvu kabisa ya wazee.

Prof. Issa Shivji aliwahi kusema katika moja ya mijadala ya vijana kuwa yeye ni kijana kutokana na kuwa upeo wake wa kufikiri bado una nguvu na hutenda kazi zaidi ya ambavyo vijana kwa mujibu wa umri wao wangeweza kufanya. Tafsiri hii ya Prof. Shivji  inakuja na maswali mengi ya kujiuliza, je ujana tuuangalie katika upeo gani? Wa umri au katka uwezo wa kuamua mambo? Kwa upande wa Prof Shivji yeye anaangalia zaidi katika upande wa maamuzi; hata kama umri wako ni mkubwa lakini bado uwezo wake wa kufikiri na kufanya maamuzi  ni mkubwa; kwa tafsiri hii ya Shivji basi Mzee wetu Kingunge Kombale Mwiru kama bado anao upeo mzuri wa maamuz ni kijana;

Kwa tafsiri yangu mimi nafikiri bado Umri uchukuliwe kama ni kigezo kikubwa cha ujana;  ujana pamoja na udogo wa umri vile vile unahusisha ukakamavu, uwajibikaji wa muda mrefu hata kufikiri vizuri kwa ufasasaha kwa hiyo bado umri ni kigezo muhimu;

Kwa nini vijana wengi hutumika sana wakati wa kampeni au shughuli zote zinazohitaji utendaji imara wa muda mrefu? Kwa nini wazee wasiwe mstari wa mbele katika kampeni? Kuna tofauti kubwa kati ya mwenye umri wa miaka 45 na 70 katika kila Nyanja.  Pamoja na hoja kuwa ujana sio umri, ujana ama kijana ni upeo wa fikra pevu. Upeo wa fikra pevu ndio unaotofautisha maendeleo ndani ya nchi.

Upeo wa fikra pevu ndio utakao wafanya vijana kuwa “nguvu ya mabadiliko”. Bongo za vijana ndio chachu ya mabadiliko, na ndio chemchem ya fikra mpya na mbadala zinazotarajiwa kulitoa Taifa katika usingizi mzito wa kifikra kwa kuwa umri wao wa ujana.

Hata katika hali ya sasa ya maendeleo ya teknologia luninga, internet n.k vijana wanapata taarifa haraka, za kina na bila kuchujwa. Jambo hili limewafungua vijana kuelewa zaidi haki zao, kutambua matamanio yao na kuanza kuona kuwa na wao wanaweza kufanya vitu vinavyofanyika sehemu nyingine duniani.


·        Tatizo la mfumo wetu ni huu kwamba wazee hawa wako kwenye umri wa kustaafu lakini hawawapi vijana nafasi kwa visingizio uzoefu;

·        vijana hawana uzoefu, mtu atapataje uzoefu asipopata pa kuapitia huo uzoefu?

Kwa nini wazee wasianze kuandaa utaratibu wa kuwaandaa vijana kupata uzoefu mapema  kwa kuwaandaa katika fani za uongozi kupitia elimu na taaluma itakayowawezesha kumudu changamoto zakiuungozi bila unafiki. Pale ambapo wazee huamua kutowasaidia vijana kupata uzoefu na kuwaacha  Kujiingiza katika siasa bila elimu ya kutosha ni sawa na kujiingiza katika jambo ‘kichwakichwa’.


Nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara. Kwanini viongozi wa kisiasa hawaoni haja ya kuwaendeleza kielimu vijana wanaowasafishia njia ya ushindi wao? Kwanini vijana wanabebeshwa mizogo mizito ambayo haina maslahi kwao wakati wa kampeni kwa kisingizio cha kuwa ni mkereketwa wa chama husika;
· Nafikiri kwa upepo huu vijana wanatakiwa kujitambua kuwa wao ndio kundi lenye watu  wenye nguvu na kutumia nguvu hizo ziwe na manufaa kwa jamii. 

Hebu tumwangalie  mheshimiwa Zitto Kabwe toka CHADEMA kijana msomi, mahiri wa kuzungumza na mwenye nguvu za hoja na mpigaji hodari kwa ajiri ya wananchi na maendeleo yao ndani ya Tanzania;


Ni ukweli mtupu kuwa vijana ni nguzo muhimu katika taifa letu. Hakika vijana wanaona na wanafikiri. Vijana hawa ambao wengi ni wasomi  wa hali ya Juu na hata wale wa kawaida wana uwezo wa kuchambua baina ya kauli tupu na utendaji wa kauli hizo. Vijana kama mheshimiwa Zitto Kabwe; Mheshimiwa Halima Mdee, Marehemu Amina Chifupa,  Nape Mnauye, Benno Malisa, mheshimiwa Godbless Lema, mheshimiwa January Makamba,James Mbatia, Mheshimiwa David Kafulia na wengine wengi; Naamini, endapo kweli tukiwa tunatambua nguvu, thamani na mchango wa vijana kama uliotolewa katika kipindi cha chaguzi zetu nchini,  tunaweza kuthubutu kimaendeleo kwa kuwapa nafasi za uongozi na wazee washuke katika basi la uongozi na sasa iwe zamu yao kulisukuma kutoka nje na sio ndani ;



HEBU TUWAPE NAFASI YA UONGOZI NA TUONE MAFANIKIO YAO


NUKUU ZA MWALIMU NYERERE KUHUSU KANSA YA UONGOZI TANZANIA:

·        “Viongozi wetu hivi sasa wanaogopa kutumia nguvu za hoja ili kufikia maamuzi muhimu.  Kwa sasa wanatumia hila zaidi kuliko hoja; vitisho kwao ni mbinu rahisi zaidi kuliko adha ya kutumia akili na kupata hoja safi ya kumjibu mpinzani katika mjadala “Viongozi hawa wakipewa nafasi watatumia hoja ya nguvu tu; hawatakuwa na haja ya kutumia akili.  Kichini chini baadhi yao tayari wameanza kutumia hoja ya vitisho.

·        “Kama tukiacha utamaduni wa woga ukazagaa, tutakuwa tunakaribisha udikteta. Uhuru hauji wala haudumishwi bila kuwa tayari kulipa gharama zake; na vitu vyote vyenye thamani kubwa, gharama yake ni kubwa.

No comments:

Post a Comment