WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, December 7, 2011

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE NA SHEREHE YA MIAKA 50 YA UHURU WA NCHI YETU TANZANIA;



·        NINI MAONI YAKO kuhusu uongozi wake?

·        JE NI KIONGOZI AMBAYE AMEANDIKA HISTORIA KAMA ILIVYOKUWA KWA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE?

·        UONGOZI WAKE TUNAWEZA KUUELEZA VIPI NI HASI AU CHANYA?


Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ndio rais wa awamu ya nne wa serikali ya Muungano wa Tanzania. Kwa maneno rahisi sana Kikwete  ndiye nahodha wa meli ya taifa ambaye amepewa mamlaka ya kuhakikisha kuwa analivusha na kulifikisha salama katika nchi ya ahadi ambayo imejaa maziwa na asali.

Rais kama kiongozi wa juu wa serikali anatakiwa kuwa na mbinu mbadala kuhakikisha kuwa ana sera ambazo zitamsadia yeye na chama chake kuhakikisha kuwa anasimamia utekelezaji sera zake kwa manufaa ya wananchi wote bila ubaguzi.

Rais anatakiwa kuwa ni mtu ambaye anajua kuwa taifa linakwenda wapi na litafika lini pale  ambapo wananchi wanataka kufikia kwa ustawi wa maisha yao; Katika kufanya hivyo, Rais anatakiwa kutoa maagizo, kuyafuatilia na pale ambapo mambo hayaendi ipasavyo na kuwawajibishawatendaji wake.


Rais wetu anatakiwa kuwa na nadharia ya “uchumi” hata kama hana shahada ya uchumi lakini kupitia washauri wake ambao wanatakiwa wamweleze ABC ya uchumi wa ulimwengu. Afahamu nini madhara ya mfumuko wa uchumi  ili wananchi wanapolalamika maisha magumu aweze kuwaelewesha na kuwapa majibu ya kuwaeleza nini kinachoendelea.

Rais wetu aweze kuona na kuuchukia mfumo na utawala wa watendaji wake wanaoendekeza ufisadi; tunajua kuwa ufisadi  unawaumiza na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwacheleweshea maendeleo ya Taifa letu;

Je Dr, Jakaya Mrisho Kikwete anaweza kujivunia mafanikio gani katika kipindi hiki kuelekea miaka 50 ya uhuru wetu?

·    Ameleta  mageuzi makubwa katika mfumo wa elimu hakuna mtoto wa Tanzania anayeshindwa kuingia sekondari kama ameshinda mtihani kwa sababu sasa nafasi zinatosheleza mahitaji kwa  Kuongeza majengo ya shule za msingi na sekondari na vyuo vikuu?


·   Amefanikiwa kuwapa wanawake nafasi za uongozi  ikiwemo nafasi ya Spika wa kwanza  mwanamke Mheshimiwa  Ana Makinda?


·   Amewezesha kuwaruhusu wananchi kuzungumzia kero za za muungano   hata kusaidia kuondoa  kero ya kulipa kodi  VAT mara mbili?

·        Amefanikiwa kuwaeleza viongozi wa dini waache biashara wa dawa za kulevya wakiwemo kwa kufanya hivyo wanaleta mfano mbaya kwa jamii wanayoifundisha kuhusu maadili mema ambayo Mwenyezi Mungu anawataka wawafundishe waumini wao?

·  Amefanikiwa kuongeza idadi ya wanawake katika uongozi kuanzia ngazi mbali mbali za uongozi serikalini?

· amefanikiwa kulifanya Taifa liwe na Kiongozi wa kwanza Mwanamke kama Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr Rose Asha Migiro?




·   Amendelea kuboresha  KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA 


·   KWA UPANDE WA VYUO  VIKUU amefanikiwa kuongeza idadi ya Wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu vilivyopo nchini Tanzania waliongezeka kwa Kuweza kujenga chuo kikuu cha Dodoma chenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 40,000 kwa mwaka?

·  Serikali yake imefanikiwa kuongeza Idadi ya vyuo vikuu imeongezeka kutoka vyuo vikuu kutoka 23 had zaidi ya  31

·        Aliingia madarakani kwa kishindo kwa asilimia karibia 80.23 ya kura zote, hiyo ikiwa ni asilimia kubwa toka uchaguzi wa vyama vingi uanze hapa nchini mwaka 1995.

·        Ameendelea kuruhusu  uhuru wa habari kwa kiasi kikubwa na kuongoza nchi chini ya utawala bora na kufuata haki za binadamu.  Katika uongozi wake ameendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa kuruhusu viongozi waandamizi wa serikali kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka.

CHANGAMOTO AMBAZO ZIKO MBELE YAKE;

MFUMUKO WA BEI



Maisha bora kwa kila mtanzania bado imekuwa ni ndoto kwani umasikini bado umeshika kasi kwani maisha ya mtanzania yakiwa yanaendelea kupanda kutokana na mfumuko wa bei yakimgusa mwananchi wa kawaida kabisa na kuporomoka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania.

MIGOMO MASHULENI


Kushindwa kutoa jibu lenye matumaini ambalo linapingana na nia ya kila mtoto au kijana ambaye amefaulu kuendelea na shule Migomo ya vyuo vikuu inaendelea kutikisa serikali yake kwa kushindwa kuwapatia mikopo wahitaji dhidi ya kufaulu na lupata sifa za kujiunga na vyuo vikuu. Nafikiri tatizo hapa sio uwezo ni kushindwa kwa bodi kubuni mbinu mbadala wa kukidhi malengo ya Rais elimu kwa kila mtu ambaye anasifa.

sheria ya mkopo kuwa kila atakayekidhi vigezo vya mkopo ikiwa na maana ya kupata usajili wa chuo na kuhakikisha kuwa hana uwezo wa kujisomesha, atapatiwa mkopo. Hii inapigana na maisha bora kwa kila mtanzania tukizingatia kuwa elimu ndio zawadi pekee kwa vijana wa taifa hili; Baba wa Taifa aliliona hili ndio maana sisi wengi tuko katika nafasi mbalimbali leo kwa kujitoa muhanga kwake kuhakikisha vijana wa kitanzania wa wakati wake wanapata elimu wakiwa na sifa zinazotakawa na shule.


Serikali kushindwa kulifanyia kazi swala hili litakuwa linapingana na nia yake njema ya kuanzisha kwa shule za sekondari za kata, itakuwa ni ukosekanaji wa vision kwa nini uanzishe shule nyingi za sekondari wakati huna uwezo wa kuwasaidia kutimiza ndto zao za elimu ya juu tukizingatia kuwa shule hizo za kata wanafunzi wengi wanasoma Shule hizi nyingi hazina walimu wala vifaa, mwanafunzi anayepata daraja la tatu au la pili katika shule za aina hii anao uwezo mkubwa wa kujifunza kuliko wanafunzi wengi wanaosoma katika shule za ambazo zinafaulisha vizuri.

Taifa limeendelea kukabiliwa na changamaoto nyingi kama ajali za barabarani, ajali za meli ambazo zimechangia vifo vya watanzania wengi: je Rais wetu msimamo wake ni upi katika vifo hivi vinavyoendelea kutokea? Je sheria zetu ni “ double standar”?


Tatizo la ukosefu wa wataalam na madawa katika hospitali zetu na zahanati hasa kwa wananchi wanaoishi vijijini bado safari ni ndefu, je tutawezaje kutatua tatizo hili? Je tutawamotisha vipi wahusika ili wawe tayari kukaa akatika mazingira magumu ili kuwatolea huduma watanzania walio wengi?






Pamoja na ujenzi wa shule nyingi za sekondari za kata tatizo ambao taifa bado inakabiliana nalo ni ubora wa shule hizo, ukosefu wa wataalam na vifaa vya kiada na makazi bora ya walimu; Hili tutalitatua vipi?



TATIZO LA UKOSEKANAJI WA MAADILI MIONGONI MWA WATENDAJI WA SERIKALI;


Changamoto kubwa nyingine ni hasa uzalendo na uwajibikaji wa viongozi walio chini yake ukitia shaka machoni mwate kama Baba wa Taifa alikuwa anasema kuwa "ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora" Siasa safi ya uwajibikaji, sio siasa ya kulindana hata pale wanaposhindwa kuwajibika. Uongozi bora utumishi na uadilifu kama rais Kikwete alivyowahi sema kuwa Sheria ya sasa inawachunguza viongozi pekee, lakini pia tunataka na watumishi wa umma ambao sio viongozi  waanze kumulikwa kwa kuwa wengi wanamilki mali nyingi tofauti na vipato vyao halali

JE KIKWETE AMEANDIKA HISTORIA GANI PAMOJA NA MAPUNGUFU YA UONGOZI WAKE;

· Kusaidia kumaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar na kufanikisha uundwaji wa serikali ya Umoja wa Kitaifa


·        Kuanzisha mchakato na kusainiwa kwa sheria ya kuandikwa kwa katiba mpya ya serikali ya muungano wa Tanzania






·        Kusherekea miaka 50 ya uhuru wa Taifa letu katika hali ya amani na utulivu


Tusherekee kwa pamoja popote ulipo miaka hii 50 ya uhuru wa Taifa letu na kuzidi kumwomba Mwenyezi Mungu kuendelea kuvumiliana pale tunapotofautiana katika mazingira yeyote yale na tuendelee kukumbuka wosia wa Baba wa Taifa alitukumbusha kuwa “Tusipopambana vikali na rushwa, wananchi watakosa imani na Serikali yao. Ni lazima tupigane na adui rushwa kwa nguvu sawa na zile tunazozitumia katika kupingana na adui wakati wa vita”.

No comments:

Post a Comment