WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, September 19, 2012

VYAMA VYA SIASA NA DHANA YA KUWAPOKEA WANACHAMA WAPYA KWENYE MIKUTANO YA HADHARA;



  • Kwa nini kadi hizo zisirudishwe kwa vyama husika katika matawi yao ili waweze kuhakiki wananchama wao?


  • Vyama vya siasa vinahakiki vipi wanachama wake?


  • Kwa nini mikutano mingi ya hadhara ya vyama vya siasa agenda kubwa ni kuwapokea wanachama wapya?


Nashindwa kuelewa pamoja na vyama vyetu vya siasa kumiliki wataalamu wa uchambuzi wa mambo ya siasa na uchumi, bado wameshindwa kutumia taaluma yao hii nyeti kuwashauri wenyeviti wa vyama vyao kuwa kuweka agenda ya kuwapokea na wanachama wapya katika mikutano yao ya siasa ni matumizi mabaya ya muda na ruzuku itokanayo na rasilimali ya Taifa letu. Muda huo ungeweza kutumika katika kufafanua agenda mbalimbali zahusizo   maendeleo ya wananchama wao  au hata kuwapa elimu mbadala juu ya haki zao ili waweze kujikwamua kutoka katika wimbi kubwa la umasikini.


Kama nilivyouliza hapo juu: Nafikiri ingekuwa ni busara kama kadi hizo zingerudishwa na kutolewa katika matawi ya vyama vyao;lakini nafikiri huu ni ufinyu wa uelewa wa demokrasia na kushindwa kuthubutu kwa viongozi wetu wa vyama; na kubwa zaidi ni kutafuta  umarufu wa kichama; je tunauhakika gani kama wanachama hao sio wa chama hicho hicho? Je hao wanaorudisha hizo kadi sio mamluki wa kisiasa; ambao kwa upeo na uelewa wa ukuaji wa demokrasis ndani ya vyama vyetu viongozi wetu wanafikiri kuwa matukio kama haya yanawaongeza wananchama kumbe nafikiri wanongeza kero ndani ya vyama vyao kwa kuwapata wananchama wa msimu ambao wengi wao huishia kuwa mamluki wa kisiasa wanaohama tuko chama kimoja kwenda kingine.

Na kubaliana na mwana zuoni ambaye aliwahi sema kuwa “Inaelekea nyie hamuwajui waTanzania walivyo hawana chama permanent, kesho wakisikia CUF wako Jangwani watarudisha hizo kadi na kuingia CUF, keshokutwa ikirudi CDM watarudisha za CUF na CCM na kuingia CDM, na CCM wakirudi tena kufanya mkutano watarudisha hizo kadi na kuchukua za CCM Kwa kifupi siasa za Bongo ni sawa na makampuni ya simu watu hununua simcard za makampuni mbali mbali kulingana na msimu”

Vyama vya siasa Tanzania hata chama kikongwe CCM wana tatizo la kutojua wana wanachama wangapi ambao ni hai na ambao wanaweza kukisaidia chama katika kukiletea maendeleo na kukipigia kura wakati wa uchaguzi, vyama vingi vinapumbazwa na halaiki ya watu wakati wa mikutano yao ya wazi; hebu mkumbuke Mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema mwaka 1995 alivyoweza kukusanya wafuasi wengi bali hawakuwa wananchama; na alijihakikishia kuwa anashinda kutokana na umati wa watu kila alipokuwa akihutubia mikutano; matokeo ya uchaguzi kwa njia ya kura yalipohitimishwa hakuamini kabisa macho na kile alichokiona;
Vyama vijitahidi kuondoa hii kasumba ili iwasaaidie wakati wa  wa uchaguzi ili waweze kuwa na uhakika walao wa aslimia 75% ya wanachama wao ambao ni hai na watakupigia kura chama chao katika mazingira yeyote yale.

  • Je kazi ya idara ya uenezi ya chama ni nini?


  • Je idara hii kichama kwa jinsi vyama vyetu vinavyofanya kazi hivi sasa ina mapungufu gani?


Kwa tafsiri yangu, nafikiri moja ya  upungufu wa kada ya uenezi ya chama husika ni kujikita zaidi katika kukizungumzia chama kwenye vyombo vya habari  na kusahau kazi yake ya msingi ya kujenga uadilifu na maadili ya viongozi wake na wanachama wake; vyama vyetu vinamwelekeo wa kukosa sifa ya  siasa safi na uongozi bora ndani ya chama husika. Siasa ni zaidi ya ushabiki wa mpira; siasa safi zenye tija litawezesha taifa lolote lile kusonga mbele;

Kwa msingi huu vyama vinatakiwa vianze kujiandaa katika kujiletea mapinduzi ya kifikra dhidi ya kujenga fikra kwa wanachama wao na sio dhana ya kuhamasisha wanachama wao kuhama hama kwa lengo la kutafuta umaarufu; Leo hii Taifa tumetawaliwa zaidi na ushabiki wa kisiasa ambao kwa ujumla hamsaidii kabisa mwananchi wa taifa hili katika kumwondoa katika umasikini unaomzunguka; viongozi wetu wajue kuwa sera za kuwashawisha wananchama kuhama hama haisaidii kabisa kukifanya chama kuwa imara. kuhamia chama kingine bila kuwa na dhamira hii ni upotoshaji na pengine kusiwe ni kujijengea umaarufu kusikuwa na tija.

  • Je viongozi ambao walikuwa na dhamana wanapohamia


  • vyama vingine tunajifunza nini? 


  • Wanakuwa wamekosa nini? 


  • Je kuhamia chama kingine ni suluhisho?


Kwa jibu la haraka kwa wahamiaji katika vyama vingine wenye dhama wanatukumbusha kuwa  hakuna wanasiasa  ni watu wanataka nafasi na kujineemesha wenyewe. Kama ameshindwa kubadilisha maisha ya watu katika dhamana ambayo alikuwa nayo kwenye chama chake cha zamani atawezaje kutumia nafasi hii katika chama kipya? Kwa uchungu kabisa nasema kuwa Wanasiasa wanaendelea kutudanganya na kwa ufinyu wa uelewa wetu wanatumia nafasi hii kufanikisha malengo yao.

Ushauri wangu viongozi wetu wa vyama wangeweza kutumia muda huu wa kugawa kadi za kujiunga na chama kwa kuwashauri wananchi na wanachama wao kuwapa elimu ya kuondoa umasikini; Kama mwandishi mmoja alivyowahi sema kuwa “Watanzania wengi mna maisha magumu, lakini sehemu ya ugumu huo wa maisha yenu umetokana na kasumba ya uvivu wa kutofanya kazi kwa bidii
Nakumbuka sana maneno ya Hayati Baba wa Taifa Julius Nyerere ili nchi iendelee inahitaji: watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Ni bahati mbaya kwamba wengi wa wanasiasa wetu wa leo si bora na wala hawaendeshi siasa safi, na hali hii inatupeleka kubaya! Ushindani wa siasa unapandikiza chuki ndani ya nchi, na kusababisha vurugu ambazo hazina masilahi kwa wanyonge ili inawatengenezea njia wachache namna ya kujiimarisha zaidi kimasilahi kwa siasa ambazo hazina Tija;


Wakati nu huu kwa wananchi kuanza kuwauliza viongozi wa vyama wanakusaidiaje wewe mnyonge ambaye huna dawa, huna maji safi na salama, huna barabara ambayo inaweza kupitika mwaka mzima, huna shule bora kwa ajili ya watoto wetu, huna uhakika na maisha yako ya kesho; nafikiri lazima tukubali kubadilisha ushabiki wa kisiasa ambao hauna tija kwa walalahoi:

No comments:

Post a Comment