WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, December 4, 2015

NIMEKUJA KIJIFUNZA KAULI YA WAZIRI MKUU MAJALIWA KASSIM MAJALIWA.



Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa ni waziri mkuu wa awamu ya Tano ambaye anaendana na kasi ya utendaji wa kazi wa Rais wa awamu ya tano Mheshimiwa Dr. Magufuli katika kurudisha uwajibikaji na matumizi mazuri ya fedha za watanzania katika idara za serikali na mashirika ya umma.

Katika hiki kipindi kifupi akiwa kama waziri mkuu ameweza kuonyesha nia dhabiti ya kuwatumikia watanzania wanyonge ambao kwa kipindi kirefu sasa wamekuwa masikini katika taifa lao ambalo lina utajiri mkubwa ambao ulikuwa ukiishia amikanoni mwa wachache.

Ameanza kazi kwa kutembelea au kufanya ziara za ghafla katika idara nyeti za serikali ambazo ni nguvu ya uchumi wa Taifa na daraja pekee katika kuondoa umasikini wa watanzania wanyonge . kauli ya ambayo alitoa hivi karibuni kuwa amekuja tu kujifunza bila kuhitaji maelezo zaidi ilikuwa ni nzito ambayo kwa kweli watendaji wa serikali na idara zake wanatakiwa kuizingatia na kuwa tayari kuwajibika mara moja.

Mheshimiwa Majaliwa ameonyesha ujasiri wake wa kujifunza nini kinaendelea katika utendaji wa watumishi wa serikali na uma na tayari ameanza kuyapa mgongo mazoea ya kale.  Kwa mhesjimiwa majaliwa ambaye hakuwa maarufu sana katika siasa za Tanzania sasa kwa kushirikiana na mhemishimiwa Rais Magufuli kwa pamoja wameamua kuhakikisha wanabadilisha mifumo ambayo ilikuwa inawanyima watanzania kaktika kuyafikia maendeleo kammili, Lengo kubwa la serikali ya tano chini ya Rais, Magufui, Makamu wa rais Samia Suluhu Hassan na Waziri mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa ni kuona kuwa wanabadilisha mifumo yote mibovu  ili kuifanya Tanzmi kuifanya inakuwa bora zaidi kwenye masuala ya uchumi, utawala na maisha ya watanzania masikini.
Waziri Mkuu kwa kushirikia na Uongozi wa awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli wana kila nafasi sasa ya kuandika historia kwa kutumia kauli mbio ya hapa kazi tu na kuhakikisha wanabadilisha mifumo yote mibovu ya kuendesha nchi kwa fiada ya watanzania  
Tukubali kuwa Tanzania ya leo inaweza kuwa tofauti sana na ya jana, na ya kesho ikawashangaza hata watu wa dunia.  Kama Mheshimiwa Majaliwa katika nafasi yake ataweza kuhakikisha kuwa anajenga mfumo ambao, hata kama yeye hatakuwepo madarakani, bado Tanzania na Watanzania watafuata na kuheshimu mifumo mipya itakayowekwa. Ndio maana kauli yake “ nimekuja kujifunza tu ni muhimu sana kwa taifa hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko. Kwa nchi kama ya kwetu, lililo muhimu kwenye mifumo ni kwa wenye kukiuka sheria, kanuni na taratibu zitakazowekwa kuadhibiwa, punde tu wanapokosea.

Je Mheshimiwa Majaliwa amejifunza nini? Na atakuja na somo gani au fundisho gani kwa hao aliowatembelea? Je ataweka mifumo mipya, yenye kutanguliza maslahi ya nchi na si ya watendaji binafsi ambao wameamua kutumia pesa katika kujilipa wao wenyewe? Je hili litakuwa anguko jingine kwa watendaji wabovu ambao wanajali sana masilahi yao na sio ya taifa?,

Kama wengi ambavyo wameseama kuwa kitendo chochote cha kupunguza matumizi yasiyo na lazima, na kutumia fedha kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania lazima kiungwe mkono kwa hali na mali.  Waziri Mkuu Majaliwa anastahili sifa kwa hilo na tumwombee Mungu amlinde ampe nguvu na aweze kutuletea mabadiliko ya kweli. 

Kwangu mimi leo kauli ya “nimekuja kujifunza” ina maana kubwa sana sisi kama taifa tunao wajibu wa kujikomboa kimawazo ili tuweze kufikiri sisi wenyewe, katika kuyapa thamani maamuzi yetu ya utendaji badala ya kusubiri ziara za ghafla za viongozi wetu ili watufundishe jinsi ya kutumia nyazifa zetu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Haiingia akili kwa watendaji wa mashirika ya umma pamoja na bozi zake kutumia pesa nyingi ili walipane mishahara na malupulupu binafsi na kuliona shirika linaendelea kudidimia na wafanyakaza na likishindwa kujiendesha. Tuwe na vichwa timamu vya kutuwezesha kuyatafakari masuala sisi wenyewe. Tunapaswa tujijengee huu msingi ili tuweze kuitathmini dhana ya maendeleo, tuweze kujiuliza maendeleo ni nini?

Katika kufanya hivyo, tunapaswa kuchukua jukumu na wajibu wa kujitungia vigezo vyetu na kuvitumia. Lazima tujenge utashi wa kujiamini na kujiamulia mambo yetu wenyewe kwa manufaa  ya taifa letu.  Ni uongo kudhani kuwa hakuna nchi ambayo imesimama tu na haibadiliki. Kosa tunalofanya ni kutozingtia ukweli huo na badala yake kuziona nchi za Ulaya na Marekani kama nchi zilizoendelea na sisi kutumia rasilimali zetu vibaya tukiendelea kusaidiwa na nchi hizo kama sisi ni mataira wa kufikira na hatujui kutenda kazi ipasavyo isipookuwa ni kufikira kuiba tu . Kwa mtindo tulio nao sasa tutabaki na hii dhana ya kujidunisha, na watu wetu kuendelea kuwa masikini miaka yote. Kwa kweli tunatakiwa Kujifunza ili tuweze badilisha huu msimamo tegemezi.

Mheshimiwa Majaliwa anatuonyesha kuwa tuna takiwakuwajibika kujikomboa kifikra, tuweze kujiwekea vigezo vyetu wenyewe. Pasipo kuwa na vigezo vinavyozingatia haki ya  uwajibikaji. Uadilifu na kumwogopa Mungu dhana ya mabadiliko na maendeleo itaendelea kuwa ndoto. Asante awamu ya Tano sasa mmeanza  

kutoondolea dhana hii. Inatubidi tubadili fikra; tukatae huu mkondo uliopo sasa wa kuitwa au kujiita sisi ni masikini wakati watu wachache ambao wamepata nafasi serikalini katika mashirika ya umma kwa sababu zao binafsi wanarudisha maendeleo yetu nyuma.

Dhana ya Maendeleo ni mabadiliko katika kitu au hali yoyote, katika nyanja mbali mbali za maisha, mabadiliko ya manufaa kwa mujibu wa mazingira husika. Katika jamii au nchi, maendeleo yanaboresha maisha ya binadamu, yanahifadhi au kuboresha mazingira, na yanaendana na heshima, utu, na haki. Maendeleo yanatokana na msukumo wa jamii au nchi husika, kwa mujibu wa mahitaji yake halisi, na kwa mujibu wa maamuzi na matakwa ya jamii hiyo, maamuzi yatokanayo na fikra huru na tambuzi, zenye mwelekeo wauwajibikaji na uadilifu. Maendeleo hayatakiwi yalete matabaka miongoni watanzania.

KWA KWELI NIMEKUJA KUJIFUNZA mimi imenifundisha kuwa tukitaka kufanikiwa katika hii safari ya kuondoa umasikini wa Taifa letu tunatakiwa kuendelea kuitekeleza kauli mbiu ya Ya Hapa Kazi Tu kwa vitendo katiaka kujiletea  maendeleo yetu na sisi kama wazalendo wa taifa hili lazima kwa umoja wetu tusiwaonee haya mafisadi, wla rushwa wazembe katika kusukuma gurudumu la nchi yetu mbele , na tuondoe dhana ya kungojea misaada kutoka nchi za nje hii haiwezi kusaidia maendeleo bali inatufanya tuendelee kuwa tegemezi zaidi .

Tunaona mfano wa nchi kama CUBA ile haifuati njia za uchumi kama nchi nyingi duniani ina uchumi wake unaokuwa kila siku , angalia uchina na mipango yao na mao ni serikali ya kikomunisti ndio lakini walikuwa na malengo ikazaa mikakati hii tunayoiona sasa hivi ni dira ya china na kufikia mwaka 2030 iwe super power; au tuangalie nini walifanya south Korea  iaka ile ya 1960s.  
Kwahiyo tuwekeze katika rasilimali ambayo tunajua inaweza kututoa hapa tulipo kwenda hatua mbili au 3 zaidi mbele bila kutegemea msaada kutoka nje. ,

Tunaweza kuendeleza mawazo ma-pya, na kuyakusanya, kuyachuja, kuyaangalia na kuyaunganisha. Hivyo, maendeleo ni hatua ambayo husonga mbele na yenye mabadiliko. Maendeleo yanajumu-isha utendaji ufuatao malengo.  Viongozi wetu wengi wanajiona wao pekee ndio wenye wajibu wa kufaidi utajiri wa nchiyetu, kupitia hulka zao za RUSHWA NA UFISADI.

Sisi kama wananchi wazalendo wa taifa letu tuko tayari kushirikiana na viongozi wa awamu ya tano katika kuyachoma magugu ambayo mengine yalikuwa yameota sugu na kuwa msitu mkubwa ambao umekuwa tishio kwa wachomaji na walulima ambao wako tayari kulisafisha pori hili. Tumeamua kuwaunga Mkono Mheshimiwa Dr. Magufuli Rais wetu na Mama Samia Makamu wa Rais na Waziri Mkuu Majaliwa msitoke jasho peke yenu katika kufyeka msitu huu. Nasi tjuko tayari kutoa ili shamba letu liweze kutoa mazao bora na sio tene kuitwa shamb la BiBi. Tunafahamu kuwa Shamba la Bibi ni letu sote kila mtu anamchango wa kulifanya listawi na kutoa mazao bora kwa faida ya wajukuu na watoto wote wa Bibi.

 
Kwa kweli nimekuja kujifunza na kugundua kuwa UFISADI NA RUSHWA unatengeneza kikundi cha watu...wenye kusimamia maslahi yao kwa faida yao UFISADI NA RUSHWA Inaunda uwepo wa vikundi visivyo rasimi kisheria kwa ajili ya kupinga/kuzuia/kufanya lobbing na kufanikisha mambo ambayo wao walio kwenye kundi husika Watafaidika nayo;

UFISADI NA RUSHWA Inapanua wigo wa Rushwa kwenye jamii na kufanya baadhi ya watu kwenye jami wasiweze kuguswa na sheria kwa sababu ya uwezo wao kwenye fedha. UFISADI NA RUSHWA Inaleta usumbufu kwenye utendaji wa Serikali kwa kuwa baadhi ya raia wanakuwa na nguvu ya fedha hivyo umma wa raia wa kawaida unatengeneza hofu ya kuogopa watu wao wenye ukwasi.

UFISADI NA RUSHWA Inavunja na kuharibu mfumo wa HAKI kwa kuwa wenye UKWASI huo wa kifisadi wanatumia ukwasi huo kuvulugu HAKI inapotafutwa. UFISADI NA RUSHWA Uzalisha kiburi/Jeuri za watu wenye ukwasi dhidi ya Watumishi wa Umma na kuwafanya waonekane si kitu mbele ya sura za jamii UFISADI NA RUSHWA Uchochea kwa kasi kubwa ongezeko la kukosekana kwa maadili ya umma na maadili ya Viongozi wa umma.Hivyo kuongeza mpasuko wa kuwa Taifa lina mmomonyoko wa maadili.

UFISADI NA RUSHWA Usababisha woga wa kitaifa hata uwezo wa kitaifa kukemea mambo yasiyostahiki utegemea ujasili wa mkemeaji. UFISADI NA RUSHWA Pia utengeneza ushawishi wa wageni kuona sehemu za kupenyeza mambo yao kwa kuwa utafuta milango ya kuingia kwa namna ambayo wao wanaona kuna njia ama upenyo. UFISADI NA RUSHWA Uchafua pia mfumo wa uendeshaji wa siasa na Serikali kwa kujalibu kuweka mapandikizi yake. 

MUNGU IBARIKI TANZANIA KATIKA AWAMU HII YA TANO HAPA KAZI TU 



No comments:

Post a Comment