WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, December 25, 2015

NGUVU YA UTUMBUAJI MAJIPU NA FALSAFA YA MPE KAISARI YALIO YA KAISARI:



Swali la msingi ambalo najiuliza sana hivi sasa hii dhana ya utumbuaji wa majipu ambao umelipatia sana hasara taifa letu asili yake wapi na kwa nini tumefikia hapa ambapo tumefika leo hii kama taifa tukiwa tumepoteza mapato mengi sana ya taifa kwa muda mrefu na taifa kukosa mwelekeo.

Jambo la msingi ambalo halipingiki ni kuwa viongozi wa taifa letu ambao walipewa dhamana ya kutuongoza walikuwa wakitekeleza dhana ya uongozi bora kwa tafsiri binafsi. Dhana ya uongozi inatakiwa ianzie wapi?

Dhana ya uongozi wa namna yeyote ile unafaa uanzie nyumbani kwa kila mtu  uongozi ni uwezo wa kuweza kuyakabili kwanza matatizo  yako mwenyewe na kufanya maamuzi sahihi bila kushawishiwa na mtu mwingine yeyote yule.

kwa kufanya hivyo utakuwa umefanikiwa kuyatawala maisha yako kulingana utaratibu ambao wewe mwenyewe umejiwekea kuanzia ndani ya familia yako;  ukifanikiwa hili unakuwa umefaulu katika mtihani huu wa kwanza wa uongozi ndipo jamii inapoanza kukuona kuwa hata ukipata nafasi ya  kuwaongoza wao pia utaweza kufanya maamuzi sahihi. 

 Kwa maneno mengine ni uwezo au njia ya kuweza kuwashawishi watu ili waweze kufanya kitu au kufikia lengo fulani la kikundi kwa ridhaa yao wenyewe. ili uongozi uwe bora ni lazima kuwe na kiongozi anayeongoza kundi fulani la watu au jamii husika kwa usahihi na kufuata maaadili ya uongozi yanayozingatia uaminifu, ukweli na uadilifu.

Katika kila jamii kuna umuhimu wa kuwa na kiongozi kunatokana na ukweli kwamba watu wanapaswa kuwa na namna ya kuunganisha nguvu zao ili kufikia malengo yao. Katika  kila jamii, ni lazima kuwepo na mikakati ya kuunganisha nguvu, vipaji, uwezo na stadi mbalimbali za wana jamii. 

Wajibu wa msingi wa kiongozi yoyote ni kusaidia kuunganisha uwezo wa watu, kuratibu, kusimamia shughuli za watu, na kila inapobidi aonyeshe njia itakayosaidia kufikia lengo. Hii ndio dhana ya serikali ya awamu ya tano chini ya Dr. John Magufuli ambaye ameonyesha utayari wa kufanya kazi na viongozi ambao wataonyesha uadilifu katika kazi zao za kuwatumikia watanzania ili kuwakwamua  kutoka katika wimbi la umasikini na kuwawajibisha viongozi wote wabadhilifu ambao wamehujumu uchumi wa watanzania.

Kwa dhana ya Plato uongozi ni dhana  au taaluma inayompa muhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale wanaoongozwa kuunganisha nguvu, stadi na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia malengo ya Taifa lao ili kujikwamua kutoka katika tabaka kandamizi ambalo linawasumbua. Kuongoza ni kujua lengo la wale wanaoongozwa na njia ya kufikia lengo lao.

Uongozi bora una mchango mkubwa sana katika uimara wa jamii. Lakini tufahamu kuwa Ubora wa kiongozi unachangiwa na vitu vingi lakini tusisahau kuwa vile vile uongozi au kiongozi bora hutoka kwa Mungu. Kama rais wa awamu ya tano alivyowahi sema kuwa serikali yake ina kazi na dhamana nzito wa kuwajengea uchumi wa kati jamii ya watanzania kwa kuelewa kuwa  wakiwatendea watanzania ndivyo sivyo adhabu yao itatoka pande mbili kwa Mungu na kwa jamii iliyowachagua.

Ikumbukwe kuwa viongozi wetu waelewe kuwa ni viongozi muhimu sana ambao wataingia katika vitabu vya kumbukumbu ya Taifa hili kuhusu ubora au ubaya kwa Taifa letu.  

swali la kuwauliza Viongozi wetu wa awamu ya tano Je watendaji wake watampa Kaisari yaliyo ya Kaisari  ili kutimiza yale waliokuwa wamehaidi wakati wa kampeni ili kubadilisha maisha ya watanzania?

Je Viongozi wa awamu ya Tano chini ya mwitikio wa Hapa Kazi Tu chini ya DR. Magufuli   wanafahamu ukubwa na umuhimu wa maamuzi yao kwa jamii ya Tanzania?

Je viongozi wetu wa awamu ya tano  wametawaliwa na maadili gani katika utendaji wa kazi yaokuendesha serikali? Ni ukweli usio fichika kuwa ili waweze kufanikiwa katika kutumiza maendeleo ya wananchi
ni lazima wazingatia maadili ya msingi ya kufanikisha  na kusimamia kwa weledi mkubwa falfasa ya Mpe kaizari yaliyo ya kaizari hasa katika kipengele ya ukusanyaji kodi ili kuimalisha mfuko wa serikali kwa maendeleo ya Taifa.

Mheshimiwa Rais Dr Magufuli ameonyesha nia dhabiti katika kutekeleza falfasa hii kwa kuanza kutumbua majipu na kupaisha makusanyo ya kodi katika mwezi huu wa December 2015. Kama taifa tunafarijika kuwa timu nzima ya serikali kwa nia nzuri sasa wanawajibika na kuwawajibisha wale wote ambao walikuwa wanakwenda kinyume na falfasa hii ambayo Yesu aliwambia wafarisayo kuhusu dhana ya kutoa kodi.

Tunaendelea kufarijika kila siku njisi watendaji wakuu wa serikali wanavyowajibika sasa na kuruduisha imani kwa Watanzania masikini kuhusu mabadiliko ya maisha yao na jamii nzima. Hivyo ni vyema waendelee kutimiza wajibu badala ya kujali maslahi yao binafsi yatokanayo na itikadi au faida ambayo wanafikiria wao tu watanufaika nayo na sio taifa;

Daima Rais wetu ameendelee kusisitiza kuwa Tanzania niyetu sote na rasilimali ambazo tumejaliwa ni zetu sote na sio mali ya kikundi Fulani tu. Na ameendelea kusisitiza kuwa  anafafahamu wananchi wanatamani nini; wanatamani watoto wao wapate elimu bora ndio maana sasa serikali imerudisha tena elimu bure kwa watoto wetu;

Anajua watanzania wanataka umoja  ndio maana anaendelea kuhubiri na kuwaomba  wananchi kuendelea kudumisha amani iliyopo katika pande zote mbili za jamuhuri ya Muungano;

Hebu tujikumbushe Busara za Baba wetu wa Taifa  Mwalimu Nyerere alipozungumzia dhana ya uongozi, Mwalimu Nyerere alisema, “uongozi ni kuonyesha njia.” Kwa maana hiyo, viongozi shurti wafahamu vyema matokeo ya uongozi wao. Wasome imani za wanaowaongoza na nyakati zilizopo ili kutambua matumaini ya umma kimaisha.

VIONGOZI GANI TUNAWAHITAJI?

Amabao hawawezi jisahau wamepewa dhamana ya  kushika hatamu ya uongozi la msingi hapa ni kuwa kiongozi amabye yuko tayari kuongoza na  na ajuwe anabeba jukumu la kubadilisha hali za watu kuwa nzuri. Atumie stadi za uongozi mwema kuonyesha njia. Mheshimiwa Dr. Magufuli ameweza kulionyesha hili kuwa kiongozi ambaye anajali Taifa na sio kukitumikia kikundi Fulani.

Wanaepuka kutumia stadi za uongozi kusimamia haki za waliowa wafikisha hapo hasa wanyonge. Wajikumbushe kuwa kupewa uongozi ni kuchukua ahadi ya kutenda kwa haki. Ukitaka kulitendea haki jipu lazima ulikamue na ulikamue vizuri na kuhakikisha kuwa kiini kimetoka ili kumpa nafuu mgonjwa. Ugonjwa ambao kama taifa tunao kwa sasa ni uchumi wetu ambao hauendani na maisha ya wananishi wetu. Tunashkukuru majipu haya sasa yanaendelea kutumbuliwa na mgojwa wetu uchumi anaendelea kuimarika.


Mwalimu Nyerere aliandika miongozo mizuri katika Azimio la Arusha miongoni mwao  akisema kwamba ili tuendelee tunahitaji Siasa Safi na Uongozi Bora. Alitambua mchango wa mambo hayo katika maendeleo ya mwanadamu. Kupitia siasa safi kila kitu cha kunufaisha wananchi hupatikana. Bali ni muhimu viongozi wanaotarajiwa kufanikisha ustawi wa wanadamu, wapatikane kwa njia ya haki. Watokane na ridhaa ya watu wenyewe wanaotaka kuongozwa. Na wakisha chaguliwa anatende kazi kwa uadilifu na ustadi mkubwa. Waweze kukusimai uchumi wetu kwa kuhakikisha kuwa yaliyo ya Kaizari anapewa Kaizari kwa faida ya Taifa nzaima.


Watendaji wetu timizeni wajibu wenu ili muweze kumsaidia rais wetu katika kufanikisha adhima ya kulijenga taifa letu kiuchumi kwa faiada ya vizazi vyetu

Mungu ibariki Tanzania

No comments:

Post a Comment