WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, July 22, 2012

KUZAMA KWA MV SKAGIT;


JE SERIKALI ZETU ( JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR) ZIMEGUNDUA NINI?


Kwa niaba ya Blogs ukadirifu na mungupamojanasi,  tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya ajali ya meli ya MV SKAGIT,iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar kuelekea Zanzibar, ambayo imesababisha watanzania wenzetu zaidi ya 40 kupoteza maisha yao na wengine wengi kujeruhiwa. Napenda kuungana na watanzania wote katika kutoa mkono wa pole kwa familia na ndugu zetu ambao wamepotelewa na wapendwa wao katika ajali mbaya na ya kusikitisha ya Mv. Skagit ambayo ilitokea tarehe 19 July 2012. Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema  tunaomba aendelee kuwafariji majererui wa ajali hii na kuwawezeshe kupona haraka ili waendelee na majukumu yao ya kulijenga Taifa.


Kama watanzania tutaendelea kumshukuru Mungu kwa ndugu zetu ambao wametangulia mbele ya haki kutokana na ajali hii pamoja na ukweli kuwa ajali hii ni uzembe mkubwa sana unaotokana na mikono ya baadhi ya watendaji na wasimamizi wa sheria za usalama wa abiria ambao wamekabidhiwa  Dhamana ya usimamizi wa sheria hii kwa masalahi ya Taifa; lakini kwa makusudi au katika kutimiza haja zao binafsi wanasababisha maafa makubwa kwa Taifa.

Ninajaribu kutafakari katika makala hii, matukio makubwa ya ajali za majini achana na ajali mbaya zinazohusiha barabara. Kama Mtanzania najaribu kujiuliza maswali mengi ambayo hayapati majibu; lakini swali langu kubwa ambalo litatawala makala hii ni hili:

Je baada ya tukio  baya ambalo lilikuwa kubwa na la kusikitisha sana ambalo lilihusisha Mv Bukoba May 21,mwaka 1996 ambapo zadi ya watu 800 walipoteza maisha, kwa nini sisi kama Taifa tumeruhusu ajali nyingine mbili mbaya kutokea katika pwani ya Zanzibar katika kipindi ambacho hakizidi mwaka mmoja?


Lakini kabla ya kufikiri kuwa sasa mambo yote ni sawa Hata mwaka haijapita  tangu ajali mbaya ya MV Spice Islander iliyozama pwani ya nungwi na kuua watanzania wenzetu zaidi ya 200. Na hata mwaka haujeisha wiki hii tumeshuudia kuwa  Mv. Skagit ambayo ilikuwa na abiria zaidi ya 200 nayo ikipatwa na ajali mbaya na kupoteza zaidi ya watanzania 40 katika pwani ya chumbe.

Tukijaribu kusahau ajali ya Mv. Bukoba takribani miaka kumi na tano iliyopita; pamoja na msemo wa Kiswahili usemao kuwa “ajali haina kinga” lakini ajali hizi mimi binafsi zinanirudisha katika kipengele kimoja kikubwa kuwa kama Taifa tumeshindwa kusimamia sheria zetu sihusuzo usala wa Raia wakiwa safarini; hapa mimi naweza kusema kuwa ninapima uwezo dhaifu wa wahusika ambao kama Taifa tumewapa dhamana ya kuzisimamia sheria zetu.

Tatizo nyingine kuna ugumu gani wa kutunza kumbukumbu za wasafiri ambao wanasafiri na chombo husika; tumekuwa Taifa ambalo hata takwimu za abiria ambao wamesafiri au wamehusika na ajali hazipo kama ziko haziko sahihi; Ajali ikitokea ndipo taarifa zinaanza kutafutwa; matokeo yake taarifa zinazotolewa zinatofautiana, na inakuwa ni aibu kubwa kwa pengine kuwaeleza wananchi taarifa ambazo sio sahihi:

Ama kweli ni aibu kubwa inakuwa kwa Waziri mwenye dhamana anapotamka takwimu ambazo sio sahihi na zinaendelea kubadilika kulingana na mazingira ya uokoaji; ni ikitokea kuwa mimi ni waziri mwenye dhamana na sina uhakika na usahihi wa takwimu hizo, sitaweza kutamka takwimu hizo kwani kwa kufanya hivyo tunaendelea kuimarisha mfumo mbovu  wa ukusanyaji wa takwimu za wasafiri.

  • Je vyombo vyetu vya majini hufanyiwa ukaguzi wa kina vinapoingizwa nchini wakati wa kusajiliwa, kubaini kuwa chombo kinafaa kwa matumizi ya kweli ya binadamu?


  • Je wakaguzi wa wizara hufanya nini au hukagua nini kabla ya chombo kuondoka?


  • Je usalama wa Taifa ambo wanakuwa katika bandari zetu wnafanya nini wananagalia nini yaani hata abiria wakijazwa wao hubaki kimya bila kutoa taarifa katika ofisi husika?


  • Kwa maneno mengine kwamba vyombo vyetu vinapoondoka bandarini havikaguliwi?


  • Watanzania wengi tunaendelea kujiuliza kwa nini meli ijaze kupita kiasi?


  • Ni nani msimamizi wa meli zetu na kwa nini meli zetu zisichukue watu kulingana na uwezo wake?


  • Sasa tufanye nini katika kuzuia ajali hizi zisiendelee kumaliza Taifa letu katika siku za usoni?


Lazima tukubali kuwa kujifunza kutokana na ajali hizo kuwa vyombo vingi vya usafiri vibovu ambavyo vinanunuliwa kuletwa kwetu baada ya kutumika sana katika nchi husika na kisha hupakwa rangi na kufanyiwa matengenezo madogo ka msingi huu vimekuwa vimepoteza sifa ya kusafirisha abiria na mizigo yao; kwa sababu ya ubovu wa vyombo hivyo na kwa sababu ya ukiukwaji wa sheria ambao huwafanya wamiliki kupakia abiria wengi kuliko uwezo wake nap engine ikitokea hali ya hewa mbaya (upepo ambo utasababisha mawimbi makubwa) chombo kama hicho hakiwezi kuhimili kishindo itaishia kukosa mwelekeo na hatamaye kupinduka tu.

Wengi tunajiuliza ilikuwaje mamlaka zinazohusika zikaruhusu meli iliyobeba abiria zaidi ya uwezo wake ikaruhusiwa kusafiri?  Au pengine wahusika wa usalama wa abiria bandari walipokea chochote ndipo wakaruhusu meli kuondoka? Lazima tukubali kukosolewa ajali hizi zote sababu yake kubwa ni uzembe wa utendaji kazi wetu;  uzembe huu ulisababisha yaliyotokea Mv Bukoba, mv spice islander na sasa Mv Skagit bado tumekuwa wagumu wa kujifunza.

Je Professionality ya manahodha wetu iko wapi?  Ningekuwa mimi    nahodha  ningethubutu kusema hatuondoki hapa mpa abiria wapunguzwe. Vile vile katika hali mbaya ya hewa ninge sitisha safari kwa usalama wa Watanzania wenzangu. Tumeyaona haya katika nchi za wenzetu ambao wanaheshimu sheria za usalama wa abiria:

Je Concord baada ya ajali ziko wapi? Nimeshangaa tu kwa nini mnjanja mmoja hajezinunua na kuzileta kwetu kwenye nchi ya majaribio ya vitu chakavu na vyema matatizo ya kiufundi:

Ni aibu kubwa sana kwa wataalamu ambao ndio wanatumaliza kwa tamaa zao binafsi ambao wanashindwa kuwashauri wamiliki wa meli aina gani ya meli wanunue wameshindwa kutumia  maadili ya kazi zao katika kuwasaidia wamiliki kufanya uamuzi sahihi. Sasa fikiria taarifa za kuwa Mv. Skagit kabla ya kuja kwetu; Undani wa ajali ya meli hii ni kama ifuatavyo: Meli iliponunuliwa ilikuwa tayari imekwishatumika. Meli hii ina miaka zaidi ya 35 ya uhai wake sasa mmiliki wa chombo hiki alipata ushauri kabla ya kununua chombo hiki au alipuuzia ushauri?

Tunaomba serikali zetu ziangalie zaidi katika Viwango (standards)  za meli zetu hapa naendelea kujiuliza kuwa je kweli tuna meli zenye viwango kulingana na bahari Zetu?


Wataalamu wetu naamini kabisa wanao uwezo uwezo wa kuangalia mambo haya kisayansi na kuyaelewa na kuja na mapendekezo ya kisayansi  yanaweza kutunaweza kuondokana kwa kiasi kikubwa cha ajali hizi kama tutafanikiwa kuandaa utaratibu wa Usimamiaji wa sheria za usalama wa abiria kwa msingi wa maadali yake; pamoja na kuzingatia Usimamiaji na ubora wa vyombo vya usafiri na ukaguzi wa kuona kama vinafikia kiwango kinachostahili
Je sisi watanzania ni kweli wavivu wa kufikiri na  kufanya maamuzi sahihi kama abiria kwani chombo cha usafiri kikijaa tunalazimishwa kupanda?


Jamani kwani sisi kama wananchi huru tunakuwa tayari kupanda chombo wakati tunaona hali ya chombo? Na wala sio shetani kama tunavyojiambia na tunayaweka maisha yetu rehani tena kwa makusudi na lolote baya likitokea tunaanza kulaumiana.

baada ya matukio haya yoye pengine ni wakati muufaka kwa serikali kufikiria ununuzi wa meli kubwa kama ilivyokuwa huko nyuma ambayo inaweza kukidhi haja ya watanzania wanyonge. Pengine kwa njia hii tunaweza kujenga msingi madhubuti kuhakikisha uzembe wa aina yoyote ule unaepukwa kulinda isije kutokea ajali kama hizi.

Kama mheshimiwa Raisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Shein ambaye alisema kuwa “Nimesikitishwa sana na msiba huu, Katika wakati huu si vema tukaanza kulaumiana jambo la muhimu hivi sasa  ni kuokoa maisha ya watu”  maneno haya ni mazito lakini hatutatenda haki kama hatutaendelea kuwakumbusha watendaji husika umuhimu wa kurekebisha vyanzo vya ajali  kama nilivyoainisha hapo juu ili kuliepusha taifa hili kuwa na wasimamiaji wabovu wa sheria na kuiepusha nchi yetu nzuri Tanzania katika majanga ya ajali za kila siku;

Nina amini kuwa kama nchi (Tanzania); ni nchi ambayo wananchi wake wanaishi sio katika nchi inayotawaliwa na sheria za msituni, bali hutawaliwa na sheria halali na tuliepushe Taifa hili na mbinu za wenye nguvu ndio wanaofaidika kwa nguvu zao na kufanya chchote wanachotaka kwa faida binafsi. Kama Taifa wakati umefika wa sisi kama wananchi kuamka na kujitambua. 


MUNGU IBARIKI TANZANIA

No comments:

Post a Comment