WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, November 22, 2011

MAENDELEO YA TASNIA YA FILAMU TANZANIA NA SHEHERE YA MIAKA 50 YA UHURU




Katika kelekea kusherekea miaka hamsini ya uhuru  kama wadau wengi walivyowahi kusema kuwa  "ANGALAU sasa Watanzania tunaweza kujivunia muvi (filamu) za nyumbani”

Kanumba aliwahi kusema kuwa “Filamu za kitanzania zina historia ndefu tofauti na wengi wanavyofikiria. kuliwahi kuwepo na filamu kama vile Fimbo ya Mnyonge (1974), Harusi ya Mariam(1983) na Yomba Yomba(1983) na nyinginezo ambazo ziliwahi kutamba sana enzi hizo. Baadaye idara ya filamu ikapotea kabla ya kupigwa kikumbo na sanaa ya maigizo” aliendelea kusema kuwa      

"Mabadiliko yapo,tena makubwa sana.Kwanza utaona kwamba mimi nilipoanza nilianzia kwenye kucheza tamthiliya na hivi sasa nimeacha kucheza tamthiliya na badala yake nacheza filamu peke yake. Hivi sasa ili aone ninachofanya inabidi ununue filamu”.

Maneno haya ya Msanii maarufu wa tasnia ya filamu Tanzania Kanumba yanaukweli ndani yake na yanaashiria kuwa kumekuwapo kwa maendeleo ya ukuaji wa tasinia ya filamu kutoka hatua moja hadi nyingine katika kipindi hiki cha miaka 50 ya uhuru;  

Wasanii wote wa Filamu wa hapa Nyumbani wake kwa wanume wanahitaji kupongezwa, kwa kuthubutu katika kufanikisha ukuaji wa tasnia ya filamu Tanzania; wasanii kama Steve Kanumba, Vincent Kigos (Ray), Blandina Chagula (Johari), Emmanuel Myamba (Pastor), Jacob Stephen (JB), Aunti Ezekiel, Steve Mangere (Nyerere), Irene Uwoya, Jackline Wolper Wema Sepetu Monalisa nimewataja baadhi na wengine wote ambao wanaendelea kukuza fani hii ya filamu Tanzania. Binafsi ninafahamu ugumu wa technolojia na mazingira ambayo yana mchango mkubwa sana katika ubora wa tasnia hii ya filamu. kweli kazi ni ngumu.Pia nawapongeza si kwa sababu eti wanatengeneza film nzuri ,Hapana ,ni kwa sababu wachache waliojitokeza katika fani hiyo wamethubutu katika kuleta  mapinduzi makubwa sana ya tasnia hii;


Tasnia ya filamu Kwa taifa linaendelea kuwa ni kioo cha jamii, basi kuna kila sababu ya   Serikali kuangalia namna ya kuwasaidia wasanii ambao ndiyo kioo cha jamii yetu; Nia ya wasanii ni kufikisha ujumbe kwa jamii,ujumbe ambao utaibadilisha jamii, utaielimisha kwa kupitia maudhui hayo ya  kuburudisha.  Ujumbe ambao utaleta mabadiliko chanya kwa jamii na siyo mabadiliko hasi, ambayo yanaliengua taifa katika mhimili wa kujisifu kupitia tamaduni zetu wenyewe.

Sina uhakika kutika kipindi hiki cha miaka 50 Wasani wetu wa tasnia ya filamu wameshawahi kujiuliza maswali  haya

·        Mimi ni nani?
·        Thamani yangu ya usanii katika tasnia ya filamu  inatokana na nini?
·        Je ni mambo gani ambayo yamejitokeza katika kipindi hiki cha miaka 50 ya uhuru na maendeleo ya filamu Tanzania
·        Ugumu wa soko la filamu katika kipindi hiki umekuwaje?
·        Je wasanii wa filamu wamekabiliwa na Ukosefu wa   creativity katika filamu zao?
·        Je namna gani kama wasanii mnakuza vipaji vyenu au mnabaki kuutafuta umaarufu baada ya kutafuta njia ya kujiendeleza na kukuza vipaji vyenu ili kazi zenu ziwe bora zaidi kwa faida yenu na taifa kwa ujumla wake?
·        Kwa nini  wasanii wetu wanakuwa wagumu wakianza kufanikiwa  wakatenga pesa na kwenda kujiendeleza kama Chuo cha sanaa bagamoyo? 
·        Ni kweli kuwa  Wasanii wengi hujibweteka na vipaji vyao wanapoanza kufanikiwa na kuanza kufanya anasa nyingi  na kuanza kujidhalilisha na kuanza kupoteza utu wao na fani yao na hatimaye "kufulia"


Kama wasanii wetu watafanikiwa kuyajibu maswali haya, hii itawasaidia kutambua kwamba thamani ya mtu haitegemei watu wengine wala wanavyosema, hata si umbo alilo nalo, bali ni hali ya ndani. Thamani ya mtu ipo ndani ya utu wake, yaani nafsini mwa mtu mwenyewe. 


Je ni ushauri gani wasanii wetu wanatakiwa waufuate ili kuimarisha sanaa zao na maendeleo yao?

·  shauri wajiendeleze kimasomo na kuijishughulisha na maswala ya maendeleo kuliku ubishoo usiokuwa na maana.


·  Suala la kuigiza uhalisia mimi naamini ni kitu kinachowezekana


·   Ni vema kuiga hekima na busara za waliondelea na kuacha yale yasiyofaa


·        Ili filamu iuze nakala nyingi siyo lazima wahusika wavae nusu uchi au waonyeshe matendo ya aibu, bali ni umahiri wa kuigiza,kipaji na nidhamu katika uigizaji.


·     Wasanii wetu wanatakiwa kukuna vichwa sana na kubadilika kulingana na dunia inavyokwenda.


·        Kupunguza matendo ya ambayo yanakiuka maadili  na kuacha tabia za uhuni kwa wasanii wote wa kike na wa kiume heshima ya kila mtu sio uhuni ni maadili mema, na kuwajibika kwa ajili ya mafanikio yao binafsi.

ni ukweli kuwa katika kipindi hiki cha miaka 50, Mimi nafikiri kosoro ambazo zimeelezwa, waigizaji wetu na waongazaji wa filamu wazichukue kama changamoto.  Ni kweli kuwa kwa sasa Soko limetanuka bado lakini Safari bado ni ndefu japo kwa wasanii angalau inatia moyo. Kwa hili pengine ushahidi tunao kutoka kwa Kanumba na Ray ambao wamewashukuru wateja wao kwa kuwawezesha  kumiliki usafiri wa gharama kubwa kupitia kazi zao.





Wasanii wote wakumbuke kuwa maendeleo yao yataendelea kupatikana tu kama watakuwa tayari kubadilika; tunazipenda kazi zenu lakini lazima ziwe katika kiwango bora cha kuangaliwa kulingana na maudhui ya kufundisha na sio kuwa kazi ambazo kila siku wanatuonyesha kitu kimoja chenye maudhui yanayofanana.


Kuelekea miaka 50 ya uhuru ni vyema wanafilamu wetu mkabadilika kwa masilahi yenu wenyewe na taifa kwa ujumla; mbembwe nyingi ambazo hazina tija hazitawasaidia sana kujinasua kwenye ugumu wa maisha ya kisanii bali creativity katika utendaji  na uandaaji wa filamu zenu ndio silaha pekee ya mafanikio yenu;

MUNGU IBARIKI TASNIA YA FILAMU TANZANIA IENDELEE KUSONGA MBELE

2 comments:

  1. This blog very interesting but you can also try these ..www.jigambeads.com and ..www.tanzaniakwetu.com for popularity and more advert to advertise. Thanks

    ReplyDelete
  2. Asante sana kwa ushauri niaitahidi kufanya hivyo bado wewe kama unanafasi ya kunitangaza basi nitashukuru sana ili wengi wanufaike nashukuru sana kwa ushauri huu mzuri

    ReplyDelete